"VITISHO VYA JK NA SIMBA WA KUCHORA" - Rais Kikwete atoa Waraka

S. S. Phares

JF-Expert Member
Nov 27, 2006
2,138
82
Rais Kikwete atoa waraka wa mwisho kwa majamabazi

* Atangaza operesheni mpya, aonya serikali isije ikalaumiwa

Na Midraj Ibrahim, Muleba

Rais Jakaya Kikwete ametangaza rasmi kuanza upya operesheni ya kusaka majambazi nchini mwezi ujao.

Aliwataka majambazi kujisalimisha na wananchi wanaowaficha kutoa taarifa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama kabla ya operesheni kuanza.

Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Muleba jana, rais Kikwete alisema operesheni mpya haitajali mtu na hakutakuwa na huruma.

"Napenda kuwaarifu mwezi ujao tutaanza operesheni kubwa nchini ya kusaka majambazi," alisema Rais Kikwete na kuongeza akiseama : "mtalaumu sana, lakini mtajilaumu wenyewe kwa kuwa ujambazi unafanya binamu, mtoto wa mjomba, lakini mnawaficha, watoeni kabla operesheni hiyo haijaanza."

Rais Kikwete alisema tangu serikali yake iingie madarakani, hakuna jambo gumu lililowashinda na kwamba sasa watachukua hatua zinazotahili lakini serikali isije ikaluamiwa.

Alisema hivi sasa vumbi la majambazi limetulia, wakibuni mbinu mpya na kwamba, kabla hawajaibuka watateketezwa na salama yao ni kujisalimisha.

Akzungumzaia kuchelewa kukamila ujenzi wa wa barabara ya Kagoma-Lusahunga alisema watambana mkandarasi ili akamilishe kulingana na mkataba.

Alisema suala la ulinzi na usalama halina mjadala ni jukumu la serikali na aliwaahidi wananchi kuwa majambazi hawataachwa watambe.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo, Mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi, alimsifu Rais Kikwete kwa ujasiri wake wa kupambana na mafisadi wakubwa.

"Umeonyesha mfano, umeanza na mafisadi wakubwa wewe endelea, sisi tutawashughulikia hawa wa chini ili tukutane katikati, wewe endelea kaza uzi!" alisema Masilingi.

Masilingi alisema hawatakubali fedha za umma kufujwa na wachache na kuongeza kuwa watapambana nao, wakishindwa wataomba msaada ngazi za juu.

Akiwa wilaya ya Chato juzi, Rais Kikwete aliwashukuru wananchi kwa kumchagua John Magufuli ambaye alisema ni msaidizi wake muhimu kutokana na utendaji wake mzuri.
 
Duh!!! Huyu Mzee ndugu Rais namna gani ? Yaani alikubali maneno ya Masilingi na sifa zake ?
 
Rais Kikwete atoa waraka wa mwisho kwa majamabazi

* Atangaza operesheni mpya, aonya serikali isije ikalaumiwa


"Napenda kuwaarifu mwezi ujao tutaanza operesheni kubwa nchini ya kusaka majambazi," alisema Rais Kikwete na kuongeza akiseama : "mtalaumu sana, lakini mtajilaumu wenyewe kwa kuwa ujambazi unafanya binamu, mtoto wa mjomba, lakini mnawaficha, watoeni kabla operesheni hiyo haijaanza."

Majambazi mmepewa ruksa na mkuu wa nchi kufanya kweli wiki hii.


Kwa hivi hapa mheshimiwa raisi anawapa green light majambazi waendelee kutesa hadi mwezi ujao. Yaani wananchi waendelee kushuhudia majambazi wanatanua hadi mwezi ujao??? what is wrong dealing with majambazi right now??? Does the police force needs seminar at ngurudoto to deal with this issue???what is so special in february???
 
Admin please merge na ile ya Mzee Mwanakijiji aliyoitoa hapa siku za nyuma kuwa JK na MIKWARA YAKE ni sawa na SIMBA WA KUCHORA asiyetisha hata sungura...

Mwisho wa Mwaka tuangalie ni mikwara mingapi alifanya kweli na mingapi alitoa porojo.
 
Katoa muda kwa kuwa wachangiaji mapesa ndani ya CCM ndiyo akina Nyali mshikaji wake na JK ambao ni majambazi so anataka kuwapa nafasi warudi wakatulie ili wakamatwe ambao siyo ama hata wapinzani wa CCM then waitwe ni majambazi .
 
mama weeeeeeeeee!!! nadhani wakati umefika wa kupigia saluti tai na kuachana na twiga..!!

Bwana weee mwanakijiji we acha tu. Yaani unamtangazia adui yako kwamba ebwanaeeee sasa jiandaee!!!Nakuja!! Huyu JK nadhani hata zile kozi za kivita alizofundiswa kule monduli hakuzielewa vizuri kama si kwamba ameshazisahau!!
 
Alipewa majina na vyeo vya Kijeshi Kichama lakini hana mbinu wala kozi za kijeshi Momnduli alikuwa anakazana na siasa tu .
 
Hizi ni njama za kudhoofisha ujambazi ufanywao na SISIEMU.

SISIEMU wakiiba fedha za umma(BOT) ili washinde uchaguzi wanaua malaki kwa mkupuo:
Tangu lini Chama kilichoshinda kwa kutumia Fedha ya wizi kikawajibika kwa wananchi?

Uliwahi ona wapi ibilisi mmoja anachukua ufagio kumfagia ibilisi mwingine?

Kwanza majambazi wengi wa kutumia Bunduki ni Polisi na wanajeshi ambao wanalinda wizi wenu wa mabilioni na wao kuendelea kuishi kwenye nyumba za FullSuit ya mabati huku ninyi mkiendelea kutanua kuliko hata Wafalme wenyewe.

Kwanini asitangaze tarehe ambayo yeye binafsi atajifikisha kizimbani pamoja na wezi wenzie ili tujue kwamba ana uchungu na nchi?

Mimi nilidhani huyu ni Rais Kijana angekuwa na uchungu na wenzake na kujenga uchumi kumbe ni nduli!
 
Wanavyomsifu JK siku hizi sasa. Tena walewale waliokuwa wakiolalamika kama nchi imeingia shimoni vile. Siasa za hii nchi bana....headache
 
Back
Top Bottom