Vitabu vya Ndalichako na TIE "vilivyoboreshwa" ni zaidi ya janga! Wabunge kusuka au kunyoa

Naumia sana kusikia darasa lenye wanafunzi 100 wa darasa saba kwamba wamefaulu wote, Jambo hili huwa linaniumiza mno.
 
Nikiukumbuka mtaala wetu kipindi kile,
Nikiikumbuka elimu yetu kipindi kile,
Mtu aliyekuwa anafaulu darasa la saba kwenda kidato cha kwanza, Lazima mmuogope kipindi hicho, Lazima atazamwe kwamba si wa kawaida kipindi hicho, Kuukomboa mtaa au kijiji lazima mwanafunzi atazamwe kama mfalme au malikia kipindi hicho.
ELIMU YETU JAMANI, MTAALA WETU JAMANI!
 
Kuna andiko limeandaliwa na wadau linalochambua vituko (sio dosari bali ni janga) vilivyopo katika vitabu vinavyodaiwa kuboreshwa na TIE baada ya vile vya awali kuchomwa moto.

Dosari na vituko hivyo havielezeki kabisa kwa lugha ya kawaida. Ni janga, mizaha na vichekesho ambavyo vinaonyesha kuwa wenye dhamana ya kuandaa vitabu wanafanya mizaha au hawawezi.

Baadhi ya makosa ni kufundisha alama za taifa ( kama bendera na nembo) ambazo si za Tanzania na kudai ni za Tanzania.

Kwa mujibu wa taratibu za kupitisha vitabu, Waziri ndIye mtu wa mwisho, je hakuona haya?
Siku ya leo na kesho kwa Wabunge wanaojali mustakabali wa Elimu naamnini Ndalichako watamtundika msalabani.

NB: Atakayetaka andiko lote ani- pm tafadhali.
Mkosoaji nae ...Bendera anaiita ramani......

Yawezekana nae ni matokeo ya hivyo vitabu
 
Unaumia tena...!!?

Kwahiyo ulitaka wafeli...
Ndiyo, Naumia!
Wafaulu angalau robo tatu yake, Kufaulu wote darasa ni kuburuzwa, ndiyo hao wanafanya upasuaji wa kichwa badala ya miguu, Au miguu badala ya kichwa, Ndiyo hao wanajaza mashairi ya diamond ktk mitihani ya necta, Ndiyo hao hawawezi kuandika barua ya kuomba kazi au cv, Wanashindwa hata kujielezea physical appearance zao.
 
Iyo mrembo ya bibi na bwana yenye ringi uwa naiona sana mahakamani hasa kwa yale majengo ya mahakama ya zamani.
 
Labda kwenye bendera hapo ndo wameweka light blue lakini nembo ya taifa sijaona dosari labda nioneshe

Hiyo nembo ya kwenye Kitabu ina Bendera ya Tanganyika sio Tanzania

Angalia hii ya kwenye Kitabu
image.jpg


Na hii halisi
image.jpg
 
Lengo la kukana na kutoa vitisho ni ili watu waache kujadili huu ujinga, na wamefanikiwa.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom