Vitabu 31 vya kusoma mwaka 2021 ili maisha yako yawe bora zaidi

Nina softcopies zaidi ya 600+,Naishia kuangalia macover tu,
Siwezi kumaliza page 5 nifanyaje?
Bora kusoma kimoja na kukifanyia kazi kuliko kutiririka wee
... utakuwa kama mwanafunzi ambaye kamwe hagraduate, yani husoma tu.
Maisha hayatutoshi kujua kilakitu, changua field moja kama ni kilimo, au bishara ... Soma vitu vinavyohusu iyokitu bobea huko... Vingine utalipia huduma. Mfano sheria, Afya nk huwezi kujua kilakitu huko ni kutangatanga...

Angalia manabii flanflan wameikariri bible tu wanapiga ela..
 
Inapokuja kwenye mafanikio, kila mtu ana maana yake.

Lakini kwa ujumla, mafanikio ni pale mtu anapokuwa bora zaidi ya alivyokuwa huko nyuma.

Kifedha kama ulikuwa na kipato kidogo na kikaongezeka, umefanikiwa.

Kimahusiano kama ulikuwa na hali ya kutokuelewana na wale wa karibu na ukaitatua, umefanikiwa.

Mwaka 2020 ulikuwa mwaka wa mengi, wengi walikuwa wanaomba uishe na kuanza mwaka 2021.

Lakini wale wote waliokuwa wanausubiri mwaka 2021 kwa hamu, wakiamini utakuwa tofauti na 2020, wamepigwa na butwaa, kwani mwaka 2021 unaonekana kuwa na changamoto zaidi ya 2020 na zimeanza mapema kabisa.

Kitakachobadili maisha yako siyo mabadiliko ya kalenda, bali mabadiliko yako binafsi.

Na mabadiliko yako binafsi hayatakuja kwa kuendelea vile ulivyo sasa, lazima ubadilike, swali ni unabadilikaje?

Ipo kauli inasema; unavyofikiri ndivyo unavyotenda, unavyotenda ndivyo unavyokuwa na unavyokuwa ndiyo hatima ya maisha yako.

Kumbe kama unataka kubadili maisha yako, basi sehemu ya kuanzia ni kwenye fikra.

Na njia rahisi ya kubadili fikra zako, ni kujifunza vitu tofauti, vitu vyenye manufaa, vitakavyokupa maarifa na hamasa ya kufanya makubwa zaidi.

Mwaka 2020, kupitia channel ya SOMA VITABU TANZANIA tulipata chambuzi za vitabu mbalimbali vya maendeleo binafsi.

Hapa nimekuchagulia vitabu 31 muhimu kwako kuvisoma (kwa kuanza na chambuzi zake) ili uweze kubadilika na kufanya makubwa 2021.

Karibu ujue vitabu hivyo na kwa kifupi unachokwenda kupata, kisha kama itakupendeza nikukaribishe kujiunga na channel ya SOMA VITABU TANZANIA, ili upate chambuzi zake kwa lugha rahisi kabisa ya Kiswahili.

Twende kwenye orodha.

1. Man’s Search For Meaning - Viktor E Frankl


Hitaji la kwanza na muhimu kabisa kwenye maisha yako ni kujua kusudi la wewe kuwa hapa duniani. Hapo ndipo wengi wanakwama na kujikuta wakiendesha maisha ambayo hawayaelewi.

Kupitia kitabu hiki, Viktor Frankl anashirikisha yale aliyopitia kwenye makambi ya mateso kwenye utawala wa NAZI wakati wa vita ya pili ya dunia. Kupitia uzoefu wake na wengine, Frankl aliweza kugundua njia tatu za mtu kujua kusudi la maisha.

Soma kitabu hiki, ujue kusudi la maisha yako na uanze kuliishi mara moja bila ya kuchelewa.

2. The 4-Hour Workweek - Timothy Ferriss

Unaweza kuwa unafanya kazi sana, uko bize kweli kweli, kila siku unachoka lakini mwisho wa siku hakuna matokeo makubwa unayozalisha. Na hata kipato unachoingiza bado hakikidhi mahitaji yako.

Tim Ferris kupitia kitabu hiki, anatuonesha jinsi ya kuweka vipaumbele vyetu vizuri, kuchagua kufanyia kazi yale yenye matokeo makubwa na kunufaika pia.

Fikiria kama ungeweza kupunguza muda wako wa kufanya kazi huku kipato chako kikiongezeka! Soma kitabu hiki na ujue jinsi ya kufanikisha hilo.

3. The Almanack of Naval Ravikant by Eric-Jorgenson

Kuna kauli maarufu kwamba fedha haiwezi kununua furaha, huku matajiri wakionekana kuwa na kila wanachokitaka lakini hawana furaha.

Hali ilikuwa hivyo kipindi cha nyuma kwa sababu wengi walipata utajiri wao kwa mchezo wa kupata na kukosa (zero sum), yaani ili mtu atajirike, ilibidi achukue kwa wengine, kupitia kuiba au kuwanyonya.

Lakini zama zimebadilika, sasa unaweza kuwa tajiri bila kuwaibia au kuwanyonya wengine. Teknolojia imekua sana kiasi kwamba unaweza kutajirika kwa kuwatajirisha wengine, kitu kitakachokupa utajiri na furaha.

Naval Ravikant anatushirikisha falsafa hiyo ya utajiri na furaha kupitia kitabu hicho, kisome kitakufanya uwe wa tofauti kabisa.

4. Principles - Life and Work - Ray Dalio

Huwa tunahangaika sana kwenye maisha na kazi kwa sababu hatuna misingi tuliyojiwekea na kuiishi, hasa wakati wa kufanya maamuzi.

Ray Dalio, kupitia uzoefu wake kwenye uwekezaji, anatushirikisha jinsi kuwa na misingi unayoifuata kunavyorahisisha kazi na maisha kwa ujumla.

Kitabu muhimu mno kusoma kwa kila anayetaka kujenga kampuni au biashara inayoweza kujiendesha bila hata ya uwepo wako huku ukiacha alama kubwa duniani.

5. The Alchemist - Paulo Coelho

Huwa tunahangaika kwenda mbali kutafuta hazina ya maisha yetu, wakati hazina hiyo ipo pale tulipo sasa.

Coelho kupitia riwaya hii anatuonesha maisha ya kijana aliyesafiri masafa marefu kutafuta hazina yake, mwisho wa siku akaikuta pale alipoanzia. Lakini kwenye safari nzima, alijifunza mengi kuhusu maisha.

Kila unalopitia kwenye maisha ni funzo na kabla hujaenda mbali kutafuta unachotaka, hebu anzia hapo ulipo sasa. Soma kitabu hiki, ni mwongozo wa kiroho na maisha kwa ujumla.

6. Atlas Shrugged - Ayn Rand

Kuna wimbi la mataifa mengi duniani kuona mfumo wa ubepari siyo mzuri na kujaribu kurudi kwenye mfumo wa ujamaa. Wimbi hili siyo jipya, limewahi kujaribiwa huko nyuma na matokeo yake hayakuwa mazuri, kwani watu wengi mno walikufa.

Ayn Rand, kupitia riwaya ya Atlas Shrugged anaonesha jinsi taifa linavyoanguka kama litapinga mfumo wa ubepari na soko huru na kukumbatia mfumo wa taifa kudhibiti kila kitu.

Ameonesha kitu anakiita mgomo wa kiakili, ambao wale wenye uwezo mkubwa na wanaozalisha wanakataa kukandamizwa na serikali huku wasio na uwezo wala kuzalisha wakibebwa.

Riwaya hii inatupa tahadhari kubwa ya jinsi mambo yanavyoanza kuharibika kidogo kidogo. Ni muhimu sana kwa zama tunazoishi sasa.

7. High Output Management - Andrew S. Grove

Kama umejiajiri au umeajiriwa, matokeo unayozalisha yanaathiriwa sana na aina ya usimamizi uliopo. Usimamizi unaweza kuchochea matokeo au ukayadidimiza.

Andrew kwa kutumia uzoefu wake anatuonesha jinsi tunavyoweza kupata matokeo makubwa kwenye kazi tunazofanya kwa kutengeneza usimamizi mzuri. Soma kitabu hiki, kuna mengi ya kujifunza kuhusu mahusiano ya kikazi.

8. The Innovator's Dilemma - Clayton M. Christensen

Ugunduzi wa teknolojia mpya umekuwa unayaweka makampuni makubwa njia panda. Na yanaposhindwa kuchukua hatua sahihi, yanakuja kuangushwa na vikampuni vidogo.

Kama upo kwenye kampuni au taasisi yoyote kubwa, unahitaji kujua jinsi ya kutumia teknolojia mpya kupiga hatua. Na hata kama uko kwenye taasisi ndogo au unaanzisha biashara yako, unapaswa kuwa na mkakati wa kutumia vizuri teknolojia kwa ukuaji, kitabu hiki ni muhimu kusoma.

9. Tao Te Ching - Lao Tzu

Wanaoongea sana hawajui, na wanaojua hawaongei sana, ni moja ya fundisho kubwa linalopatikana kwenye kitabu hiki.

Kitabu kinafundisha falsafa ya kiroho ya China ya kale, falsafa ya Tao ambayo inatufundisha kuishi kulingana na sheria za asili.

Kitabu ni kifupi na mafunzo yake yanagusa kila eneo la maisha, kisome.

10. The Fountainhead - Ayn Rand

Ayn Rand tena, hapa anaonesha vita iliyopo kwenye jamii kati ya kuwa tofauti na kufuata kundi.

Jamii inakupenda pale unapofanya kile ambacho wengine wanafanya na kimezoeleka, lakini hapo utalazimika kujipendekeza ili upate upendeleo, kitu kinachokuja kukuangusha baadaye.

Lakini ukichagua kuwa tofauti, ukichagua kufanya yale ambayo hayajazoeleka, jamii itakupiga vita, utakutana na vikwazo vingi, lakini kama utasimama imara, mwisho utapata ushindi mkubwa.

Niseme kama mtu umejiajiri au uko kwenye biashara au ndiyo unapanga kufanya hivyo, basi soma riwaya hii, misingi na misimamo ya Howard Roark itakusaidia sana, hasa kwa zama tunazoishi sasa.

11. Poor Charlie’s Almanack - The Wit and Wisdom of Charles T. Munger - Charles T. Munger

Charlie Munger ni mshirika wa Warren Buffet katika uwekezaji, wamekuwa pamoja kwa miaka 50 na wamekuwa wawekezaji wenye mafanikio makubwa.

Mafanikio yao yako kwenye kitu kimoja, kusoma vitabu. Munger ambaye ana miaka 90 anatumia asilimia 80 ya muda wake kusoma vitabu.

Kwenye kitabu hiki anatushirikisha hekima alizojifunza na kuzitumia kufanikiwa kwenye uwekezaji, anatuonesha makosa ya kuepuka wakati wa kufanya maamuzi ya kifedha.

Kama unafanya biashara au uwekezaji, Munger ni mtu unayepaswa kumsoma, maana anatufundisha jinsi ya kutengeneza mfumo wa kiakili wa kufanya maamuzi (Mental Modal).

12. The Black Swan - The Impact of the Highly Improbable by Nassim Nicholas Taleb

Kwa sababu tukio halijawahi kutokea, haimaanishi kwamba haliwezi kutokea. Hilo ndiyo kosa kubwa ambalo binadamu huwa tunafanya, tunaishi kwa mazoea na linatokea jambo ambalo hatujajiandaa nalo na linatusumbua.

Taleb kupitia kitabu hiki anatufundisha jinsi ya kuwa tayari kwa yale ambayo hayajawahi kutokea. Kila mtu anapaswa kusoma kitabu hiki.

13. Dune by Herbert Frank

Maisha, siasa, uongozi, dini na sayansi ni vitu vinavyojenga jamii yetu, vitu ambavyo vina mwingiliano mkubwa.

Kupitia riwaya ya Dune, Herbert ametuonesha jinsi mambo hayo yanavyoingiliana na madhara yake iwapo hayatafanyika vizuri. Herbert ameonesha hatari ya jamii pale inapokuwa chini ya kiongozi shujaa, kwani huwa hayaoni madhaifu yake na yanakuwa angamizo.

Kikubwa kabia kwenye riwaya hii, ni sala ya kuishinda hofu, sala inayokupa nguvu ya kukabiliana na chochote kile. Soma kitabu hiki, kinaendana sana na zama tunazopitia sasa.

14. The War of Art_ Winning the Inner Creative Battle by Steven Pressfield

Kama unafanya kazi yoyote ya kibunifu, iwe ni kuandika, kuchora, kutunga, kuandaa programu mbalimbali na mengine, unajua vita kubwa ambayo huwa inaendelea ndani yako.

Kila unapopanga ukae chini kwa ajili ya kazi ya ubunifu, kunatokea kitu cha kukushawishi uahirishe. Kupitia kitabu hiki, Pressfield anatupa mbinu za kushinda vita ya ndani yetu na kuweza kuzalisha kazi bora kabisa za kibunifu.

15. A Journal of the Plague Year by Defoe Daniel

Mwaka 2020 dunia ilijikuta ikisimama kwa sababu ya mlipuko wa Covid 19. Mwanzoni watu walikuwa na matumaini kwamba ni kitu kitakachopita na mambo yatarudi sawa tu. Lakini sasa tupo 2021 na hakuna dalili za mambo kurudi sawa.

Unaweza kufikiri hili ni jipya, kwamba ndiyo mara ya kwanza dunia inapitia hali kama hii. Lakini siyo kweli, kwani kwenye karne ya 16, mji wa London ulipatwa na mlipuko kama huu na cha kushangaza, makosa yaliyofanyika kipindi hicho, ndiyo tunayarudia sasa.

Dunia inapitia kipindi kigumu kutokana na mlipuko huu, ambapo matumaini yaliyokuwa yamepatikana kutokana na kugunduliwa kwa chanjo haraka, yamezimika ghafla kwa kuja kwa aina mpya ya kirusi cha ugonjwa huo ambacho hakizuiliki kwa chanjo zilizopo sasa.

Kwa kusoma kitabu hiki, tunajifunza makosa ya kuepuka ili kuweza kuvuka janga hili salama.

16. Zero to One - Notes on Startups, or How to Build the Future by Peter Thiel, Blake Masters

Kuna njia mbili za kuiboresha dunia, Ugunduzi na Utandawazi. Ugunduzi ni pale unapoanzia sifuri na kuja na kitu ambacho ni kipya kabisa. Utandawazi ni kuhamisha kile ambacho kimefanya kazi eneo moja na kufanya eneo jingine.

Kama unataka mafanikio makubwa, basi unapaswa kuwa mgunduzi, kwa kuanzia sifuri kwenda moja.

Peter Thiel, bilionea mwekezaji ambaye alianzia sifuri kwenye mengi, anatushirikisha jinsi ya kuweza kuja na ugunduzi utakaoibadili dunia na kutupa mafanikio makubwa.

17. The Hard Thing About Hard Things - Building a Business When There Are No Easy Answers by Ben Horowitz

Sheria ya kwanza kwenye mafanikio kupitia biashara na ujasiriamali ni kwamba hakuna sheria moja inayowafaa watu wote.

Hivyo pamoja na kujifunza kutoka kwa wengine, bado unapaswa kufanya maamuzi magumu wewe mwenyewe.

Horowitz, kupitia uzoefu wake kwenye kuanzisha na kukuza biashara mbalimbali, anatuonesha jinsi maamuzi yalivyo magumu na jinsi ya kufanya maamuzi sahihi. Kama upo au unapanga kuingia kwenye biashara, hiki ni kitabu ambacho unapaswa kusoma, kitakuandaa vizuri sana kukabiliana na ugumu wa safari.

18. The plague by Albert Camus

Kitabu namba 15 hapo juu kimeonesha maisha wakati wa mlipuko, hasa kwa wananchi wa kawaida, namna walivyokuwa wanapambana na hali ya mlipuko. Kitabu hicho kina matukio mengi ambayo yalikuwa ya kweli kabisa.

Albert Camus yeye aliandika riwaya iliyoelezea maisha wakati wa mlipuko, hasa kwa upande wa wapambanaji. Ni riwaya inayotuonesha wakati mgumu wanaokuwa nao wale walio mstari wa mbele katika kupambana na mlipuko. Kuanzia viongozi wa kisiasa, vingozi wa dini na wahudumu wa afya.

Wapo ambao wanaamua kusimamia ukweli na wapo wanaoukataa ukweli. Riwaya hii inatuonesha madhara ya yote hayo, inatuonesha jinsi mlipuko wa majanga unavyogusa kila eneo la maisha, hasa eneo la kiroho.

Kama unapata wakati mgumu wa kufanya maamuzi mbalimbali kipindi hiki cha mlipuko wa Covid 19, soma kitabu hiki, kitakupa msingi wa kufanya maamuzi sahihi.

19. How to Win Friends and Influence People by Dale Carnegie

Chochote unachotafuta kwenye maisha, kipo kwenye mikono ya wengine. Ukiwanyang’anya kwa nguvu hutakifurahia, lakini ipo njia ya kuwashawishi wao wenyewe wakupe unachotaka tena wakiwa wanafurahia.

Carnegie ametupa ufungu wa kuingia kwenye mioyo ya watu na kukubalika. Ametupa siri nyingi, moja wapo ni kutumia jina la mtu kwa usahihi.

Kitabu hiki ni cha kusomwa na kila mtu, kwa sababu kila mmoja wetu kuna kitu anataka kwa mwingine, ukiwa na ushawishi mzuri, utapata kila unachotaka.

20. Thinking, Fast and Slow-Farrar - Daniel Kahneman

Ubongo wetu una mifumo miwili ya kufikiri, wa kwanza ni wa haraka na unaotumia hisia, wa pili ni wa taratibu na unaotumia mantiki.

Makosa mengi tunayofanya kwenye maisha ni kwa sababu tunatumia zaidi mfumo wa kwanza kuliko wa pili.

Kahneman ameichambua vizuri mifumo hiyo miwili na kutuonesha jinsi ya kuitumia kufanya maamuzi ambayo ni bora. Kama umekuwa unafanya maamuzi kwa mhemko na yanakugharimu, soma kitabu hiki.

21. Bird by Bird - Some Instructions on Writing and Life - Anne Lamott

Kwa waandishi, unapokuwa na kazi kubwa ya kuandika ni rahisi kuahirisha kuliko kukaa chini na kuandika.

Mfano makala hii yenye vitabu 31 vya kusoma, kila mara nimekuwa najiambia nitaiandika, lakini naona mpaka nimalize vitabu vyote 31 itachukua muda.

Lakini nikakumbuka ushauri wa Lamott, kwamba kama una kazi kubwa ya kuandika, nenda kipande kwa kipande.

Kitabu hiki ni kozi fupi ya uandishi, tangu kupata wazo, kuandika, kuhariri mpaka kuchapa. Kama ni mwandishi au unataka kuandika, kitabu hiki ni muhimu kukisoma.

22. Fahrenheit 451 by Bradbury Ray

Riwaya nyingine inayoendana na zama tunazoishi, unaweza kuona orodha hii ya vitabu ina riwaya (novel) saba, na zote zinaendana mno na zama tunazoishi sasa.

Msingi wa riwaya ya Fahrenheit 451 ni jamii inayoangamia kwa sababu imeacha kusoma vitabu. Watawala wanafurahia hilo, kwa sababu watu hawafikiri tena, muda wote wanaangalia tv huku wakijazwa propaganda. Kikosi cha zimamoto kimepewa kazi ya kusaka na kuchoma vitabu vyote vilivyosalia.

Umeshaona jinsi inaendana na zama hizi? Iko wazi, watu kwa sasa hawasomi tena vitabu, ila muda wote wapo kwenye mitandao ya kijamii, wanajazwa propaganda nyingi na hawawezi tena kufikiri kwa usahihi.

Tushukuru bado vitabu havijapigwa marufuku, lakini hatujui siku zijazo, huenda sisi wasomaji tukaonekana ndiyo kikwazo na vitabu vikaanza kupigwa marufuku. Hivyo tusome vitabu, tufikiri kwa akili zetu na kuyaishi maisha yenye maana kwetu na siyo kufuata tu mkumbo.

Soma kitabu hiki kama unataka kuwa na maisha huru, kufikiri kwa akili yako na kufanya maamuzi yako mwenyewe.

23. Surely Youre Joking, Mr. Feynman (Adventures of a Curious Character) by Richard P. Feynman, Ralph Leighton

Kuna watu huwa wanachagua kuyaishi maisha yao na kwa namna wanavyoyaishi, wengine wanahamasika kuchagua kuishi maisha yao pia.

Mmoja wa watu hao ni aliyekuwa mwanafizikia Richard Feynman, huyu alifanya kazi ana kwa ana na akina Albert Einstein, Niel Bohr na wanasayansi wengine wakubwa ambao tumesoma nadharia zao kwenye vitabu.

Feynman alikuwa ni mtu mwenye udadisi mkubwa, ambaye hakuwa anakubaliana na kitu kwa sababu wengi wanakubaliana nacho, badala yake alikuwa anajaribu kila kitu yeye mwenyewe.

Kuna mifano mingi mno ya jinsi alivyojaribu mambo na kugundua watu walikuwa hawapo sahihi, soma kitabu hiki, kitakuhamasisha kuchagua kuyaishi maisha yako na kuwa na msimamo sahihi.

24. High Growth Handbook - Elad Gil

Kuna aina mbili za ukuaji wa biashara, ukuaji wa awali, pale kampuni inapotoka wafanyakazi chini ya kumi mpaka kufika wafanyakazi makumi. Halafu kuna ukuaji wa kasi wa baadaye, kutoka wafanyakazi makumi kwenda maelfu.

Mikakati ya ukuaji haifanani katika vipindi hivyo. Vitabu vingi vya biashara vinaelezea ukuaji wa awali, lakini ukuaji wa kasi wa baadaye huwa hauelezewi kwa kina na hapo ndipo wengi hufanya makosa yanayoangusha kabisa biashara.

Kama upo kwenye biashara, hiki ni kitabu muhimu kusoma, pia kama upo kwenye taasisi yenye malengo ya kukua zaidi, soma kitabu hiki, utapata madini ya kuisaidia taasisi kitu kitakachofanya uthaminiwe zaidi.

25. Give and Take; A Revolutionary Approach to Success - Adam M. Grant Ph.D.

Watu wamegawanyika katika makundi matatu, watoaji, wachukuaji na wabadilishanaji.

Watoaji ni wale wanaotoa kwa wengine bila kuangalia wanapata nini. Wachukuaji hawa huangalia wanapata nini bila kujali wengine wanapata nini. Wabadilishanaji ni wale wa nipe nikupe, nikune nikukune.

Katika makundi hayo matatu, wanaopata mafanikio makubwa sana ni watoaji. Unaweza usielewe, lakini mwandishi ameeleza vizuri nguvu ya utoaji kwenye mafanikio. Soma kitabu hiki, kitakusaidia mno katika kujenga msingi utakaokufikisha kwenye mafanikio makubwa hata kama unaanzia chini kabisa.

26. Siddhartha - Hermann Hesse

Riwaya ya kiroho, inayoelezea maisha ya kijana aliyechoshwa na imani ya mazoea kwenye jamii yake na kwenda kutafuta imani mpya na yenye maana. Katika safari hiyo anapotea, anaanguka kwenye maisha ya anasa za dunia, lakini baadaye anapata uamsho na kurudi kwenye njia sahihi.

Maisha yana njia mbalimbali za kututega na kutuangusha, kibaya siyo kuanguka, bali kuanguka na kutokuinuka tena. Maisha ya Siddhartha yanatufundisha mengi, kuanzia kukataa kuishi kwa mazoea, kuwa na kitu chenye thamani ndani yako na kutokusahau kile kilicho ndani yako.

Soma riwaya hii, itakupa nguvu ya kukabiliana na magumu ya maisha.

27. Mindset - Changing The Way You think To Fulfil Your Potential by Carol S. Dweck

Kuna mitazamo miwili ya kiakili, mgando (fixed) na ukuaji (growth).

Wale wanaofanikiwa kwenye maisha ni wenye mtazamo wa ukuaji na siyo mtazamo wa mgando.

Kupitia tafiti mbalimbali, Dweck anatuonesha kwa nini inakuwa hivyo.

Kikubwa sana ambacho utajifunza kwenye kitabu hiki, ni kulea watoto wenye mtazamo wa ukuaji na siyo mgando.

Kuna kauli ambazo ukizitumia kama mzazi zinamjengea mtoto mtazamo mgando na kuwa kikwazo kwake. Mfano mtoto akifaulu ukamwambia ana akili au akifeli na kumwambia hana akili, hapo unamfanya awe na mtazamo mgando, aamini ana akili au hana. Lakini ukimwambia mtoto amepata matokeo aliyopata kutokana na juhudi alizoweka, anakuwa na mtazamo wa ukuaji, ambao utamsukuma aweke juhudi zaidi na afaulu zaidi.

Kama ni mzazi, mwalimu, kocha au kiongozi wa aina yoyote ile, kitabu hiki ni muhimu mno kusoma.

28. Influence - the psychology of persuasion by Cialdini, Robert B

Kitabu namba 19 hapo juu ni cha kukusaidia uwe na ushawishi mkubwa kwa wengine kwenye mahusiano binafsi. Kitabu hiki cha namba 28 kinakusaidia kuwa na ushawishi mkubwa kwa wengine kwenye biashara au uongozi.

Mwandishi ametumia tafiti mbalimbali kuelezea silaha kuu sita za ushawishi, silaha ambazo zina nguvu ya kumshawishi mtu kuchukua hatua fulani.

Matangazo yoyote ya biashara unayokutana nayo kila siku, yanatumia sana misingi ya kitabu hiki.

Kama unataka kuwa na ushawishi kwa watu, hata ambao hawakujui, basi soma kitabu hiki. Kama upo kwenye biashara au kazi yako inahusisha masoko na mauzo, hii inapaswa kuwa biblia yako, zijue silaha sita za ushawishi na jinsi ya kuzitumia kupata matokeo mazuri.

29. Can't Even - How Millennials Became the Burnout Generation by Anne Helen Petersen

Kuna kitu kimoja nimekuwa nakiona kwenye kazi yangu ya utabibu, sehemu kubwa ya watu wenye miaka kati ya 25 mpaka 45 wanaokuja hospitali hawaumwi chochote, ni uchovu tu.

Mtu atakuja akionekana yuko hoi, kila kiungo cha mwili kinamuuma, vinafanyika vipimo mbalimbali na vyote vinaonesha hakuna tatizo. Watu wengi walio kwenye hilo kundi (ukiondoa wajawazito na wenye magonjwa sugu) huwa wako kwenye afya njema kabisa, ila uchovu ndiyo unawasumbua.

Kwa kuwa siku hizi kazi nyingi tunazofanya ni za kutumia akili kuliko mwili, mtu anakikuta anafanya kazi muda mrefu na hapati muda wa kutosha wa kupumzisha akili, kinachotokea ni akili kuulazimisha mwili upumzike, hilo ndiyo linafanya mtu aone anaumwa wakati hana ugonjwa wowote.

Petersen kupitia kitabu hiki anaonesha kwa nini kizazi cha milenia (watu waliozaliwa kati ya mwaka 1981 mpaka 1996) kimekuwa kizazi cha watu wenye uchovu sana.

Anaonesha jinsi uchovu umeanzia shuleni ambapo tulikazaniwa kusoma sana ili tufaulu, ukaenda kwenye kazi ambapo kwanza hazipatikani na zikipatikana siyo zenye kipato kizuri. Na mbaya zaidi ni hii mitandao ya kijamii ambayo inafanya mtu kuwa bize muda wote.

Sina haja ya kukueleza zaidi kuhusu uchovu unaopitia, unaujua, soma kitabu hiki ili ujue hatua sahihi za kuondokana na uchovu ulionao sasa na kuwa na maisha tulivu.

30. The Four Agreements by Don Miguel Ruiz

Kuna maagano mengi ambayo unayaishi sasa, maagano ambayo yamekuweka kwenye kifungo na kujikuta ukiishi kama uko jehanamu. Maagano hayo yana nguvu kubwa ila huijui, kwa sababu jamii haitaki ujue, inataka uendelee kukaa kwenye maagano hayo ili ikutumie utakavyo.

Miguel kupitia kitabu chake anatushirikisha maagano mapya manne ya kuyaishi kwenye maisha yako, ambayo yatakufanya uwe huru na uishi mbingu ukiwa hapa duniani. Kwa kuyajua na kuyaishi maagano haya, hutakuwa tena kwenye utumwa wa kijamii, badala yake utakuwa huru kuyaishi maisha yako.

Huwezi kujua gereza ulilopo kama hujasoma kitabu hiki, hivyo kisome, maagano ni rahisi kabisa na hayakutaki ubadili chochote kwenye maisha yako isipokuwa fikra zako na namna unavyoyachukulia maisha.

31. The Psychology of Money - Timeless Lessons on Wealth, Greed, and Happiness by Morgan Housel

Inapokuja kwenye pesa, kila mtu anafanya maamuzi ambayo kwake anaona ni sahihi, japo kwa wengine yanaweza kuonekana ni ya ajabu. Haijalishi utawashauri nini watu kuhusu pesa, bado mwisho wa siku watafanya maamuzi ambayo huwezi kuyaelewa.

Hiyo ni kwa sababu maamuzi yetu ya kifedha huwa tunayafanya kwa hisia na siyo mantiki. Hivyo kilicho muhimu sana kwenye fedha ni saikolojia yetu. Tunashindwa kubadilika inapokuja kwenye fedha, kwa sababu hatujui jinsi ya kubadili saikolojia yetu kifedha.

Kwenye kitabu hiki, Morgan Housel anatupa masomo 20 kuhusu saikolojia ya fedha, jinsi tunavyosukumwa kufanya maamuzi ya kifedha na namna ya kufanya maamuzi bora.

Fedha ni eneo muhimu kwenye maisha ya kila mtu, hivyo hiki ni kitabu ambacho kila mtu anapaswa kukisoma ili aweze kufanya maamuzi sahihi kifedha.

Rafiki, hivyo ndiyo vitabu 31 vya kusoma ili mwaka 2021 uwe bora kabisa kwako.
Asante kwa hii orodha nutaifanyia kazi
 
Halafu mwaka tushaupiga nusu ujue,Mkuu uzi umecheleweshwa au tuupeleke mbele ili Iwe 2022.
 
Inapokuja kwenye mafanikio, kila mtu ana maana yake.

Lakini kwa ujumla, mafanikio ni pale mtu anapokuwa bora zaidi ya alivyokuwa huko nyuma.

Kifedha kama ulikuwa na kipato kidogo na kikaongezeka, umefanikiwa.

Kimahusiano kama ulikuwa na hali ya kutokuelewana na wale wa karibu na ukaitatua, umefanikiwa.

Mwaka 2020 ulikuwa mwaka wa mengi, wengi walikuwa wanaomba uishe na kuanza mwaka 2021.

Lakini wale wote waliokuwa wanausubiri mwaka 2021 kwa hamu, wakiamini utakuwa tofauti na 2020, wamepigwa na butwaa, kwani mwaka 2021 unaonekana kuwa na changamoto zaidi ya 2020 na zimeanza mapema kabisa.

Kitakachobadili maisha yako siyo mabadiliko ya kalenda, bali mabadiliko yako binafsi.

Na mabadiliko yako binafsi hayatakuja kwa kuendelea vile ulivyo sasa, lazima ubadilike, swali ni unabadilikaje?

Ipo kauli inasema; unavyofikiri ndivyo unavyotenda, unavyotenda ndivyo unavyokuwa na unavyokuwa ndiyo hatima ya maisha yako.

Kumbe kama unataka kubadili maisha yako, basi sehemu ya kuanzia ni kwenye fikra.

Na njia rahisi ya kubadili fikra zako, ni kujifunza vitu tofauti, vitu vyenye manufaa, vitakavyokupa maarifa na hamasa ya kufanya makubwa zaidi.

Mwaka 2020, kupitia channel ya SOMA VITABU TANZANIA tulipata chambuzi za vitabu mbalimbali vya maendeleo binafsi.

Hapa nimekuchagulia vitabu 31 muhimu kwako kuvisoma (kwa kuanza na chambuzi zake) ili uweze kubadilika na kufanya makubwa 2021.

Karibu ujue vitabu hivyo na kwa kifupi unachokwenda kupata, kisha kama itakupendeza nikukaribishe kujiunga na channel ya SOMA VITABU TANZANIA, ili upate chambuzi zake kwa lugha rahisi kabisa ya Kiswahili.

Twende kwenye orodha.

1. Man’s Search For Meaning - Viktor E Frankl


Hitaji la kwanza na muhimu kabisa kwenye maisha yako ni kujua kusudi la wewe kuwa hapa duniani. Hapo ndipo wengi wanakwama na kujikuta wakiendesha maisha ambayo hawayaelewi.

Kupitia kitabu hiki, Viktor Frankl anashirikisha yale aliyopitia kwenye makambi ya mateso kwenye utawala wa NAZI wakati wa vita ya pili ya dunia. Kupitia uzoefu wake na wengine, Frankl aliweza kugundua njia tatu za mtu kujua kusudi la maisha.

Soma kitabu hiki, ujue kusudi la maisha yako na uanze kuliishi mara moja bila ya kuchelewa.

2. The 4-Hour Workweek - Timothy Ferriss

Unaweza kuwa unafanya kazi sana, uko bize kweli kweli, kila siku unachoka lakini mwisho wa siku hakuna matokeo makubwa unayozalisha. Na hata kipato unachoingiza bado hakikidhi mahitaji yako.

Tim Ferris kupitia kitabu hiki, anatuonesha jinsi ya kuweka vipaumbele vyetu vizuri, kuchagua kufanyia kazi yale yenye matokeo makubwa na kunufaika pia.

Fikiria kama ungeweza kupunguza muda wako wa kufanya kazi huku kipato chako kikiongezeka! Soma kitabu hiki na ujue jinsi ya kufanikisha hilo.

3. The Almanack of Naval Ravikant by Eric-Jorgenson

Kuna kauli maarufu kwamba fedha haiwezi kununua furaha, huku matajiri wakionekana kuwa na kila wanachokitaka lakini hawana furaha.

Hali ilikuwa hivyo kipindi cha nyuma kwa sababu wengi walipata utajiri wao kwa mchezo wa kupata na kukosa (zero sum), yaani ili mtu atajirike, ilibidi achukue kwa wengine, kupitia kuiba au kuwanyonya.

Lakini zama zimebadilika, sasa unaweza kuwa tajiri bila kuwaibia au kuwanyonya wengine. Teknolojia imekua sana kiasi kwamba unaweza kutajirika kwa kuwatajirisha wengine, kitu kitakachokupa utajiri na furaha.

Naval Ravikant anatushirikisha falsafa hiyo ya utajiri na furaha kupitia kitabu hicho, kisome kitakufanya uwe wa tofauti kabisa.

4. Principles - Life and Work - Ray Dalio

Huwa tunahangaika sana kwenye maisha na kazi kwa sababu hatuna misingi tuliyojiwekea na kuiishi, hasa wakati wa kufanya maamuzi.

Ray Dalio, kupitia uzoefu wake kwenye uwekezaji, anatushirikisha jinsi kuwa na misingi unayoifuata kunavyorahisisha kazi na maisha kwa ujumla.

Kitabu muhimu mno kusoma kwa kila anayetaka kujenga kampuni au biashara inayoweza kujiendesha bila hata ya uwepo wako huku ukiacha alama kubwa duniani.

5. The Alchemist - Paulo Coelho

Huwa tunahangaika kwenda mbali kutafuta hazina ya maisha yetu, wakati hazina hiyo ipo pale tulipo sasa.

Coelho kupitia riwaya hii anatuonesha maisha ya kijana aliyesafiri masafa marefu kutafuta hazina yake, mwisho wa siku akaikuta pale alipoanzia. Lakini kwenye safari nzima, alijifunza mengi kuhusu maisha.

Kila unalopitia kwenye maisha ni funzo na kabla hujaenda mbali kutafuta unachotaka, hebu anzia hapo ulipo sasa. Soma kitabu hiki, ni mwongozo wa kiroho na maisha kwa ujumla.

6. Atlas Shrugged - Ayn Rand

Kuna wimbi la mataifa mengi duniani kuona mfumo wa ubepari siyo mzuri na kujaribu kurudi kwenye mfumo wa ujamaa. Wimbi hili siyo jipya, limewahi kujaribiwa huko nyuma na matokeo yake hayakuwa mazuri, kwani watu wengi mno walikufa.

Ayn Rand, kupitia riwaya ya Atlas Shrugged anaonesha jinsi taifa linavyoanguka kama litapinga mfumo wa ubepari na soko huru na kukumbatia mfumo wa taifa kudhibiti kila kitu.

Ameonesha kitu anakiita mgomo wa kiakili, ambao wale wenye uwezo mkubwa na wanaozalisha wanakataa kukandamizwa na serikali huku wasio na uwezo wala kuzalisha wakibebwa.

Riwaya hii inatupa tahadhari kubwa ya jinsi mambo yanavyoanza kuharibika kidogo kidogo. Ni muhimu sana kwa zama tunazoishi sasa.

7. High Output Management - Andrew S. Grove

Kama umejiajiri au umeajiriwa, matokeo unayozalisha yanaathiriwa sana na aina ya usimamizi uliopo. Usimamizi unaweza kuchochea matokeo au ukayadidimiza.

Andrew kwa kutumia uzoefu wake anatuonesha jinsi tunavyoweza kupata matokeo makubwa kwenye kazi tunazofanya kwa kutengeneza usimamizi mzuri. Soma kitabu hiki, kuna mengi ya kujifunza kuhusu mahusiano ya kikazi.

8. The Innovator's Dilemma - Clayton M. Christensen

Ugunduzi wa teknolojia mpya umekuwa unayaweka makampuni makubwa njia panda. Na yanaposhindwa kuchukua hatua sahihi, yanakuja kuangushwa na vikampuni vidogo.

Kama upo kwenye kampuni au taasisi yoyote kubwa, unahitaji kujua jinsi ya kutumia teknolojia mpya kupiga hatua. Na hata kama uko kwenye taasisi ndogo au unaanzisha biashara yako, unapaswa kuwa na mkakati wa kutumia vizuri teknolojia kwa ukuaji, kitabu hiki ni muhimu kusoma.

9. Tao Te Ching - Lao Tzu

Wanaoongea sana hawajui, na wanaojua hawaongei sana, ni moja ya fundisho kubwa linalopatikana kwenye kitabu hiki.

Kitabu kinafundisha falsafa ya kiroho ya China ya kale, falsafa ya Tao ambayo inatufundisha kuishi kulingana na sheria za asili.

Kitabu ni kifupi na mafunzo yake yanagusa kila eneo la maisha, kisome.

10. The Fountainhead - Ayn Rand

Ayn Rand tena, hapa anaonesha vita iliyopo kwenye jamii kati ya kuwa tofauti na kufuata kundi.

Jamii inakupenda pale unapofanya kile ambacho wengine wanafanya na kimezoeleka, lakini hapo utalazimika kujipendekeza ili upate upendeleo, kitu kinachokuja kukuangusha baadaye.

Lakini ukichagua kuwa tofauti, ukichagua kufanya yale ambayo hayajazoeleka, jamii itakupiga vita, utakutana na vikwazo vingi, lakini kama utasimama imara, mwisho utapata ushindi mkubwa.

Niseme kama mtu umejiajiri au uko kwenye biashara au ndiyo unapanga kufanya hivyo, basi soma riwaya hii, misingi na misimamo ya Howard Roark itakusaidia sana, hasa kwa zama tunazoishi sasa.

11. Poor Charlie’s Almanack - The Wit and Wisdom of Charles T. Munger - Charles T. Munger

Charlie Munger ni mshirika wa Warren Buffet katika uwekezaji, wamekuwa pamoja kwa miaka 50 na wamekuwa wawekezaji wenye mafanikio makubwa.

Mafanikio yao yako kwenye kitu kimoja, kusoma vitabu. Munger ambaye ana miaka 90 anatumia asilimia 80 ya muda wake kusoma vitabu.

Kwenye kitabu hiki anatushirikisha hekima alizojifunza na kuzitumia kufanikiwa kwenye uwekezaji, anatuonesha makosa ya kuepuka wakati wa kufanya maamuzi ya kifedha.

Kama unafanya biashara au uwekezaji, Munger ni mtu unayepaswa kumsoma, maana anatufundisha jinsi ya kutengeneza mfumo wa kiakili wa kufanya maamuzi (Mental Modal).

12. The Black Swan - The Impact of the Highly Improbable by Nassim Nicholas Taleb

Kwa sababu tukio halijawahi kutokea, haimaanishi kwamba haliwezi kutokea. Hilo ndiyo kosa kubwa ambalo binadamu huwa tunafanya, tunaishi kwa mazoea na linatokea jambo ambalo hatujajiandaa nalo na linatusumbua.

Taleb kupitia kitabu hiki anatufundisha jinsi ya kuwa tayari kwa yale ambayo hayajawahi kutokea. Kila mtu anapaswa kusoma kitabu hiki.

13. Dune by Herbert Frank

Maisha, siasa, uongozi, dini na sayansi ni vitu vinavyojenga jamii yetu, vitu ambavyo vina mwingiliano mkubwa.

Kupitia riwaya ya Dune, Herbert ametuonesha jinsi mambo hayo yanavyoingiliana na madhara yake iwapo hayatafanyika vizuri. Herbert ameonesha hatari ya jamii pale inapokuwa chini ya kiongozi shujaa, kwani huwa hayaoni madhaifu yake na yanakuwa angamizo.

Kikubwa kabia kwenye riwaya hii, ni sala ya kuishinda hofu, sala inayokupa nguvu ya kukabiliana na chochote kile. Soma kitabu hiki, kinaendana sana na zama tunazopitia sasa.

14. The War of Art_ Winning the Inner Creative Battle by Steven Pressfield

Kama unafanya kazi yoyote ya kibunifu, iwe ni kuandika, kuchora, kutunga, kuandaa programu mbalimbali na mengine, unajua vita kubwa ambayo huwa inaendelea ndani yako.

Kila unapopanga ukae chini kwa ajili ya kazi ya ubunifu, kunatokea kitu cha kukushawishi uahirishe. Kupitia kitabu hiki, Pressfield anatupa mbinu za kushinda vita ya ndani yetu na kuweza kuzalisha kazi bora kabisa za kibunifu.

15. A Journal of the Plague Year by Defoe Daniel

Mwaka 2020 dunia ilijikuta ikisimama kwa sababu ya mlipuko wa Covid 19. Mwanzoni watu walikuwa na matumaini kwamba ni kitu kitakachopita na mambo yatarudi sawa tu. Lakini sasa tupo 2021 na hakuna dalili za mambo kurudi sawa.

Unaweza kufikiri hili ni jipya, kwamba ndiyo mara ya kwanza dunia inapitia hali kama hii. Lakini siyo kweli, kwani kwenye karne ya 16, mji wa London ulipatwa na mlipuko kama huu na cha kushangaza, makosa yaliyofanyika kipindi hicho, ndiyo tunayarudia sasa.

Dunia inapitia kipindi kigumu kutokana na mlipuko huu, ambapo matumaini yaliyokuwa yamepatikana kutokana na kugunduliwa kwa chanjo haraka, yamezimika ghafla kwa kuja kwa aina mpya ya kirusi cha ugonjwa huo ambacho hakizuiliki kwa chanjo zilizopo sasa.

Kwa kusoma kitabu hiki, tunajifunza makosa ya kuepuka ili kuweza kuvuka janga hili salama.

16. Zero to One - Notes on Startups, or How to Build the Future by Peter Thiel, Blake Masters

Kuna njia mbili za kuiboresha dunia, Ugunduzi na Utandawazi. Ugunduzi ni pale unapoanzia sifuri na kuja na kitu ambacho ni kipya kabisa. Utandawazi ni kuhamisha kile ambacho kimefanya kazi eneo moja na kufanya eneo jingine.

Kama unataka mafanikio makubwa, basi unapaswa kuwa mgunduzi, kwa kuanzia sifuri kwenda moja.

Peter Thiel, bilionea mwekezaji ambaye alianzia sifuri kwenye mengi, anatushirikisha jinsi ya kuweza kuja na ugunduzi utakaoibadili dunia na kutupa mafanikio makubwa.

17. The Hard Thing About Hard Things - Building a Business When There Are No Easy Answers by Ben Horowitz

Sheria ya kwanza kwenye mafanikio kupitia biashara na ujasiriamali ni kwamba hakuna sheria moja inayowafaa watu wote.

Hivyo pamoja na kujifunza kutoka kwa wengine, bado unapaswa kufanya maamuzi magumu wewe mwenyewe.

Horowitz, kupitia uzoefu wake kwenye kuanzisha na kukuza biashara mbalimbali, anatuonesha jinsi maamuzi yalivyo magumu na jinsi ya kufanya maamuzi sahihi. Kama upo au unapanga kuingia kwenye biashara, hiki ni kitabu ambacho unapaswa kusoma, kitakuandaa vizuri sana kukabiliana na ugumu wa safari.

18. The plague by Albert Camus

Kitabu namba 15 hapo juu kimeonesha maisha wakati wa mlipuko, hasa kwa wananchi wa kawaida, namna walivyokuwa wanapambana na hali ya mlipuko. Kitabu hicho kina matukio mengi ambayo yalikuwa ya kweli kabisa.

Albert Camus yeye aliandika riwaya iliyoelezea maisha wakati wa mlipuko, hasa kwa upande wa wapambanaji. Ni riwaya inayotuonesha wakati mgumu wanaokuwa nao wale walio mstari wa mbele katika kupambana na mlipuko. Kuanzia viongozi wa kisiasa, vingozi wa dini na wahudumu wa afya.

Wapo ambao wanaamua kusimamia ukweli na wapo wanaoukataa ukweli. Riwaya hii inatuonesha madhara ya yote hayo, inatuonesha jinsi mlipuko wa majanga unavyogusa kila eneo la maisha, hasa eneo la kiroho.

Kama unapata wakati mgumu wa kufanya maamuzi mbalimbali kipindi hiki cha mlipuko wa Covid 19, soma kitabu hiki, kitakupa msingi wa kufanya maamuzi sahihi.

19. How to Win Friends and Influence People by Dale Carnegie

Chochote unachotafuta kwenye maisha, kipo kwenye mikono ya wengine. Ukiwanyang’anya kwa nguvu hutakifurahia, lakini ipo njia ya kuwashawishi wao wenyewe wakupe unachotaka tena wakiwa wanafurahia.

Carnegie ametupa ufungu wa kuingia kwenye mioyo ya watu na kukubalika. Ametupa siri nyingi, moja wapo ni kutumia jina la mtu kwa usahihi.

Kitabu hiki ni cha kusomwa na kila mtu, kwa sababu kila mmoja wetu kuna kitu anataka kwa mwingine, ukiwa na ushawishi mzuri, utapata kila unachotaka.

20. Thinking, Fast and Slow-Farrar - Daniel Kahneman

Ubongo wetu una mifumo miwili ya kufikiri, wa kwanza ni wa haraka na unaotumia hisia, wa pili ni wa taratibu na unaotumia mantiki.

Makosa mengi tunayofanya kwenye maisha ni kwa sababu tunatumia zaidi mfumo wa kwanza kuliko wa pili.

Kahneman ameichambua vizuri mifumo hiyo miwili na kutuonesha jinsi ya kuitumia kufanya maamuzi ambayo ni bora. Kama umekuwa unafanya maamuzi kwa mhemko na yanakugharimu, soma kitabu hiki.

21. Bird by Bird - Some Instructions on Writing and Life - Anne Lamott

Kwa waandishi, unapokuwa na kazi kubwa ya kuandika ni rahisi kuahirisha kuliko kukaa chini na kuandika.

Mfano makala hii yenye vitabu 31 vya kusoma, kila mara nimekuwa najiambia nitaiandika, lakini naona mpaka nimalize vitabu vyote 31 itachukua muda.

Lakini nikakumbuka ushauri wa Lamott, kwamba kama una kazi kubwa ya kuandika, nenda kipande kwa kipande.

Kitabu hiki ni kozi fupi ya uandishi, tangu kupata wazo, kuandika, kuhariri mpaka kuchapa. Kama ni mwandishi au unataka kuandika, kitabu hiki ni muhimu kukisoma.

22. Fahrenheit 451 by Bradbury Ray

Riwaya nyingine inayoendana na zama tunazoishi, unaweza kuona orodha hii ya vitabu ina riwaya (novel) saba, na zote zinaendana mno na zama tunazoishi sasa.

Msingi wa riwaya ya Fahrenheit 451 ni jamii inayoangamia kwa sababu imeacha kusoma vitabu. Watawala wanafurahia hilo, kwa sababu watu hawafikiri tena, muda wote wanaangalia tv huku wakijazwa propaganda. Kikosi cha zimamoto kimepewa kazi ya kusaka na kuchoma vitabu vyote vilivyosalia.

Umeshaona jinsi inaendana na zama hizi? Iko wazi, watu kwa sasa hawasomi tena vitabu, ila muda wote wapo kwenye mitandao ya kijamii, wanajazwa propaganda nyingi na hawawezi tena kufikiri kwa usahihi.

Tushukuru bado vitabu havijapigwa marufuku, lakini hatujui siku zijazo, huenda sisi wasomaji tukaonekana ndiyo kikwazo na vitabu vikaanza kupigwa marufuku. Hivyo tusome vitabu, tufikiri kwa akili zetu na kuyaishi maisha yenye maana kwetu na siyo kufuata tu mkumbo.

Soma kitabu hiki kama unataka kuwa na maisha huru, kufikiri kwa akili yako na kufanya maamuzi yako mwenyewe.

23. Surely Youre Joking, Mr. Feynman (Adventures of a Curious Character) by Richard P. Feynman, Ralph Leighton

Kuna watu huwa wanachagua kuyaishi maisha yao na kwa namna wanavyoyaishi, wengine wanahamasika kuchagua kuishi maisha yao pia.

Mmoja wa watu hao ni aliyekuwa mwanafizikia Richard Feynman, huyu alifanya kazi ana kwa ana na akina Albert Einstein, Niel Bohr na wanasayansi wengine wakubwa ambao tumesoma nadharia zao kwenye vitabu.

Feynman alikuwa ni mtu mwenye udadisi mkubwa, ambaye hakuwa anakubaliana na kitu kwa sababu wengi wanakubaliana nacho, badala yake alikuwa anajaribu kila kitu yeye mwenyewe.

Kuna mifano mingi mno ya jinsi alivyojaribu mambo na kugundua watu walikuwa hawapo sahihi, soma kitabu hiki, kitakuhamasisha kuchagua kuyaishi maisha yako na kuwa na msimamo sahihi.

24. High Growth Handbook - Elad Gil

Kuna aina mbili za ukuaji wa biashara, ukuaji wa awali, pale kampuni inapotoka wafanyakazi chini ya kumi mpaka kufika wafanyakazi makumi. Halafu kuna ukuaji wa kasi wa baadaye, kutoka wafanyakazi makumi kwenda maelfu.

Mikakati ya ukuaji haifanani katika vipindi hivyo. Vitabu vingi vya biashara vinaelezea ukuaji wa awali, lakini ukuaji wa kasi wa baadaye huwa hauelezewi kwa kina na hapo ndipo wengi hufanya makosa yanayoangusha kabisa biashara.

Kama upo kwenye biashara, hiki ni kitabu muhimu kusoma, pia kama upo kwenye taasisi yenye malengo ya kukua zaidi, soma kitabu hiki, utapata madini ya kuisaidia taasisi kitu kitakachofanya uthaminiwe zaidi.

25. Give and Take; A Revolutionary Approach to Success - Adam M. Grant Ph.D.

Watu wamegawanyika katika makundi matatu, watoaji, wachukuaji na wabadilishanaji.

Watoaji ni wale wanaotoa kwa wengine bila kuangalia wanapata nini. Wachukuaji hawa huangalia wanapata nini bila kujali wengine wanapata nini. Wabadilishanaji ni wale wa nipe nikupe, nikune nikukune.

Katika makundi hayo matatu, wanaopata mafanikio makubwa sana ni watoaji. Unaweza usielewe, lakini mwandishi ameeleza vizuri nguvu ya utoaji kwenye mafanikio. Soma kitabu hiki, kitakusaidia mno katika kujenga msingi utakaokufikisha kwenye mafanikio makubwa hata kama unaanzia chini kabisa.

26. Siddhartha - Hermann Hesse

Riwaya ya kiroho, inayoelezea maisha ya kijana aliyechoshwa na imani ya mazoea kwenye jamii yake na kwenda kutafuta imani mpya na yenye maana. Katika safari hiyo anapotea, anaanguka kwenye maisha ya anasa za dunia, lakini baadaye anapata uamsho na kurudi kwenye njia sahihi.

Maisha yana njia mbalimbali za kututega na kutuangusha, kibaya siyo kuanguka, bali kuanguka na kutokuinuka tena. Maisha ya Siddhartha yanatufundisha mengi, kuanzia kukataa kuishi kwa mazoea, kuwa na kitu chenye thamani ndani yako na kutokusahau kile kilicho ndani yako.

Soma riwaya hii, itakupa nguvu ya kukabiliana na magumu ya maisha.

27. Mindset - Changing The Way You think To Fulfil Your Potential by Carol S. Dweck

Kuna mitazamo miwili ya kiakili, mgando (fixed) na ukuaji (growth).

Wale wanaofanikiwa kwenye maisha ni wenye mtazamo wa ukuaji na siyo mtazamo wa mgando.

Kupitia tafiti mbalimbali, Dweck anatuonesha kwa nini inakuwa hivyo.

Kikubwa sana ambacho utajifunza kwenye kitabu hiki, ni kulea watoto wenye mtazamo wa ukuaji na siyo mgando.

Kuna kauli ambazo ukizitumia kama mzazi zinamjengea mtoto mtazamo mgando na kuwa kikwazo kwake. Mfano mtoto akifaulu ukamwambia ana akili au akifeli na kumwambia hana akili, hapo unamfanya awe na mtazamo mgando, aamini ana akili au hana. Lakini ukimwambia mtoto amepata matokeo aliyopata kutokana na juhudi alizoweka, anakuwa na mtazamo wa ukuaji, ambao utamsukuma aweke juhudi zaidi na afaulu zaidi.

Kama ni mzazi, mwalimu, kocha au kiongozi wa aina yoyote ile, kitabu hiki ni muhimu mno kusoma.

28. Influence - the psychology of persuasion by Cialdini, Robert B

Kitabu namba 19 hapo juu ni cha kukusaidia uwe na ushawishi mkubwa kwa wengine kwenye mahusiano binafsi. Kitabu hiki cha namba 28 kinakusaidia kuwa na ushawishi mkubwa kwa wengine kwenye biashara au uongozi.

Mwandishi ametumia tafiti mbalimbali kuelezea silaha kuu sita za ushawishi, silaha ambazo zina nguvu ya kumshawishi mtu kuchukua hatua fulani.

Matangazo yoyote ya biashara unayokutana nayo kila siku, yanatumia sana misingi ya kitabu hiki.

Kama unataka kuwa na ushawishi kwa watu, hata ambao hawakujui, basi soma kitabu hiki. Kama upo kwenye biashara au kazi yako inahusisha masoko na mauzo, hii inapaswa kuwa biblia yako, zijue silaha sita za ushawishi na jinsi ya kuzitumia kupata matokeo mazuri.

29. Can't Even - How Millennials Became the Burnout Generation by Anne Helen Petersen

Kuna kitu kimoja nimekuwa nakiona kwenye kazi yangu ya utabibu, sehemu kubwa ya watu wenye miaka kati ya 25 mpaka 45 wanaokuja hospitali hawaumwi chochote, ni uchovu tu.

Mtu atakuja akionekana yuko hoi, kila kiungo cha mwili kinamuuma, vinafanyika vipimo mbalimbali na vyote vinaonesha hakuna tatizo. Watu wengi walio kwenye hilo kundi (ukiondoa wajawazito na wenye magonjwa sugu) huwa wako kwenye afya njema kabisa, ila uchovu ndiyo unawasumbua.

Kwa kuwa siku hizi kazi nyingi tunazofanya ni za kutumia akili kuliko mwili, mtu anakikuta anafanya kazi muda mrefu na hapati muda wa kutosha wa kupumzisha akili, kinachotokea ni akili kuulazimisha mwili upumzike, hilo ndiyo linafanya mtu aone anaumwa wakati hana ugonjwa wowote.

Petersen kupitia kitabu hiki anaonesha kwa nini kizazi cha milenia (watu waliozaliwa kati ya mwaka 1981 mpaka 1996) kimekuwa kizazi cha watu wenye uchovu sana.

Anaonesha jinsi uchovu umeanzia shuleni ambapo tulikazaniwa kusoma sana ili tufaulu, ukaenda kwenye kazi ambapo kwanza hazipatikani na zikipatikana siyo zenye kipato kizuri. Na mbaya zaidi ni hii mitandao ya kijamii ambayo inafanya mtu kuwa bize muda wote.

Sina haja ya kukueleza zaidi kuhusu uchovu unaopitia, unaujua, soma kitabu hiki ili ujue hatua sahihi za kuondokana na uchovu ulionao sasa na kuwa na maisha tulivu.

30. The Four Agreements by Don Miguel Ruiz

Kuna maagano mengi ambayo unayaishi sasa, maagano ambayo yamekuweka kwenye kifungo na kujikuta ukiishi kama uko jehanamu. Maagano hayo yana nguvu kubwa ila huijui, kwa sababu jamii haitaki ujue, inataka uendelee kukaa kwenye maagano hayo ili ikutumie utakavyo.

Miguel kupitia kitabu chake anatushirikisha maagano mapya manne ya kuyaishi kwenye maisha yako, ambayo yatakufanya uwe huru na uishi mbingu ukiwa hapa duniani. Kwa kuyajua na kuyaishi maagano haya, hutakuwa tena kwenye utumwa wa kijamii, badala yake utakuwa huru kuyaishi maisha yako.

Huwezi kujua gereza ulilopo kama hujasoma kitabu hiki, hivyo kisome, maagano ni rahisi kabisa na hayakutaki ubadili chochote kwenye maisha yako isipokuwa fikra zako na namna unavyoyachukulia maisha.

31. The Psychology of Money - Timeless Lessons on Wealth, Greed, and Happiness by Morgan Housel

Inapokuja kwenye pesa, kila mtu anafanya maamuzi ambayo kwake anaona ni sahihi, japo kwa wengine yanaweza kuonekana ni ya ajabu. Haijalishi utawashauri nini watu kuhusu pesa, bado mwisho wa siku watafanya maamuzi ambayo huwezi kuyaelewa.

Hiyo ni kwa sababu maamuzi yetu ya kifedha huwa tunayafanya kwa hisia na siyo mantiki. Hivyo kilicho muhimu sana kwenye fedha ni saikolojia yetu. Tunashindwa kubadilika inapokuja kwenye fedha, kwa sababu hatujui jinsi ya kubadili saikolojia yetu kifedha.

Kwenye kitabu hiki, Morgan Housel anatupa masomo 20 kuhusu saikolojia ya fedha, jinsi tunavyosukumwa kufanya maamuzi ya kifedha na namna ya kufanya maamuzi bora.

Fedha ni eneo muhimu kwenye maisha ya kila mtu, hivyo hiki ni kitabu ambacho kila mtu anapaswa kukisoma ili aweze kufanya maamuzi sahihi kifedha.

Rafiki, hivyo ndiyo vitabu 31 vya kusoma ili mwaka 2021 uwe bora kabisa kwako.

Asante sana mkuu
 
Binafsi nimepia tu Maelekzo ya hivi vitabu vikanipa mtazamo Mpya ,, kikubwa Cha kuzingatia ni kusoma na kuchukua hatua! learn as much as possible but is not necessary to follow each thing you learn,,,,,,,,,,. Akili za kuambiwa changanya na zako
 

UCHAMBUZI WA KITABU; Why Don't We Learn From History? (Kwa Nini Hatujifunzi Kutoka Kwenye Historia?)


Karibu kwenye uchambuzi wa kitabu kinachoitwa Why don't we learn from history? Kilichoandikwa na B. H. Liddell Hart.

Kitabu hiki ni mkusanyiko wa mafunzo ambayo B. H. Liddell Hart aliyekuwa mwanajeshi na mwanahistoria alikuwa ameyaandaa na baadaye kuchapwa na mtoto wake anayeitwa Adrian J. Liddell Hart

Sir Basil Henry Liddell Hart (31 October 1895 – 29 January 1970), alikuwa kapteni wa jeshi la Uingereza na mwanahistoria wa kijeshi. Aliandika vitabu mbalimbali vya mbinu za kivita na kuonesha makosa ambayo yamekuwa yakifanywa kwenye vita na kuleta madhara makubwa.

Mafunzo yake ya kivita yalikuwa yakitumiwa na majeshi ya nchi mbalimbali kipindi cha vita ya kwanza na ya pili ya dunia.

Kitabu kina sehemu tatu, historia na ukweli, serikali na uhuru na vita na amani. Uchambuzi utakuwa na sehemu mbili, sehemu ya kwanza itakuwa na uchambuzi wa sehemu mbili za kwanza za kitabu na sehemu ya pili itakuwa na uchambuzi wa sehemu ya tatu na hitimisho.

Karibu kwenye uchambuzi wa kitabu hiki, tujifunze jinsi ambavyo serikali, majeshi na hata watu binafsi tumekuwa tunarudia makosa kutokana na kutokujifunza kutoka kwenye historia.


Utangulizi kutoka kwa mwandishi.

Kuandika kuhusu historia ni kazi ngumu na inayochosha sana. Hiyo ni kwa sababu kuujua ukweli inahitaji mtu kuweka kazi ya ziada.

Historia imetawaliwa na uongo ambapo waandishi na wanahistoria wengi hulazimika kuandika kisichokuwa kweli hasa maisha yao yanapotegemea kuwaridhisha wengine.

Inahitaji mtu kuwa na uhuru wa kipato kwenye maisha ili uweze kuutafuta ukweli na kuandika kilicho kweli bila ya kushinikizwa na yeyote.

Uandishi wa historia unahitaji muda na uvumilivu kwani unapogusa kitu kimoja, unagundua kimeungana na vitu vingine vingi, ambavyo vyote unapaswa kuvichunguza kwa undani ili kujua ukweli wake.

Pamoja na ugumu wa kuandika kuhusu historia, kuna manufaa yake ambayo ni kama ifuatavyo;

1. Ni kitu kinachompa mtu hamasa kadiri anavyoendelea kuchunguza na kujifunza.

2. Ni kazi inayoipa akili mazoezi na hivyo kuizuia isizeeke haraka.

3. Ni kazi ambayo manufaa yake yanadumu kwa muda mrefu.

Historia siyo tu muhimu kwa mataifa, bali pia ni muhimu kwa mtu mmoja mmoja kwani inatusaidia kujijengea falsafa binafsi na kutuzuia kurudia makosa ya wengine huku ikitusaidia kuwa na hekima.

Mwanahistoria wa kale, Polybius, amewahi kusema kwamba njia bora ya kujifunza ni kupitia makosa na majanga yanayowakumba wengine.

Historia inatupa nafasi ya kujifunza hayo na kutupa matumaini kwamba hata mambo yawe magumu kiasi gani, huwa yana mwisho, baada ya giza nene ni mwangaza.

Historia ina manufaa makubwa kwa mtu mmoja mmoja, kwa taifa na dunia kwa ujumla. Kama tunataka kuwa na maisha bora, kuepuka kurudia makosa waliyofanya wengine na kuwa na matumaini wakati tunapitia magumu, tunapaswa kujifunza kutoka kwenye historia.


Thamani ya historia.

Lengo kuu la historia ni ukweli, kujua nini kilitokea na kwa nini kilitokea. Kwa maneno mengine, lengo la historia ni kujua uhusiano na visababishi vya matukio mbalimbali.

Ili historia iwe sahihi na yenye manufaa, lazima isimame kwenye ukweli, kitu ambacho kinahitaji kazi na maadili kukisimamia. Watu wengi hawapendi ukweli, kwa sababu huwa haubembelezi au kutekeleza matakwa yao binafsi.

Historia ina ukomo wake, japo inaweza kutuonesha uelekeo, haiwezi kutupa maelezo kuhusu hali ya njia itakavyokuwa. Lakini ukomo huu haufanyi historia isiwe muhimu, bali unakuwa ni tahadhari ambayo mtu anapaswa kuwa nayo anapojifunza kupitia historia.

Historia inatuonesha nini tunachopaswa kuepuka, hata kama haiwezi kutufundisha kipi cha kufanya, itatuonesha makosa yaliyofanywa na wengine ili tusiyarudie.

Bismarck amewahi kunukuliwa akisema; “wapumbavu husema wanajifunza kwa uzoefu, napendelea kujifunza kupitia uzoefu wa wengine.” Ni kupitia historia ndiyo tunaweza kujifunza kupitia uzoefu wa wengine, kuangalia makosa waliyofanya ili tusiyarudie na kukosea kama wao.

Jamii nyingi zimekuwa zinachukulia umri wa mtu kama kipimo cha hekima, kwamba mwenye umri mkubwa ana uzoefu mkubwa na hivyo kuwa na hekima zaidi. Lakini ukiangalia kupitia historia, hilo haliwezi kuwa kweli, mwenye umri mkubwa ambaye anatumia uzoefu wake binafsi, hawezi kuwa na hekima ukilinganisha na mwenye umri mdogo anayejifunza kwenye historia.

Kama mtu ana miaka 80 na anatumia uzoefu wake binafsi, atazidiwa na mwenye miaka 40 ambaye amejifunza historia ya miaka elfu 3 iliyopita. Uzoefu binafsi pekee hautoshi, historia ina mengi ya kujifunza ambayo mtu mmoja hawezi kuyapitia yote kwa uzoefu wake mwenyewe.

Mwandishi anasema kama mtu anajua kusoma na kuandika, ni uzembe kama akili yake haina miaka zaidi ya elfu tatu.

Ni Polybius aliyesema kuna njia mbili za kuijenga jamii, ya kwanza kupitia makosa yake yenyewe na ya pili kupitia makosa ya wengine. Njia ya kwanza ni ngumu na yenye maumivu, njia ya pili ni rahisi na isiyoumiza. Maarifa ambayo mtu anayapata kwa kujifunza kupitia historia ni maarifa bora kwenye maisha.

Historia ni kumbukumbu za hatua na makosa ya mwanadamu. Inatuonesha kwamba hatua huwa zinapigwa taratibu lakini makosa yanatokea haraka. Inatupa fursa ya kujifunza na kunufaika kwa makosa ya waliotutangulia.

Wengi hufanya makosa na kuchukulia historia kama somo linalowahusu wanahistoria pekee, lakini historia ni kitu kinachogusa kila sehemu ya maisha yetu na hivyo inamhusu kila mtu. Kwa taaluma na tasnia yoyote ile, kuna watu waliotangulia ambao walifanya makosa mbalimbali, kujifunza kupitia wao inatuzuia tusirudie makosa yao.


Mbinu za kisayansi.

Kuweza kukabiliana na changamoto na matatizo ya dunia, kuweza kuyaona jinsi yalivyo, kuyachambua na kufikia ukweli, mbinu za kisayansi zinahitajika.

Hapo mtu anapaswa kuachana na upendeleo alionao na kuwa tayari kudadisi na kuhoji kila kitu badala ya kukipokea kilivyo.

Lazima mtu awe tayari kujikosoa yeye mwenyewe na kujisukuma kuutafuta ukweli badala ya kuchukulia mazoea.

Lengo la kwanza kwenye historia linapaswa kuwa ukweli na njia ya kufikia ukweli huo ni kutumia mbinu za kisayansi.

Pale mtu anaposikia chochote kinachopingana naye au kukosoa anachosimamia, hapaswi kukikataa kwanza, bali anapaswa kujiuliza swali hili; je ni kweli? Swali hilo linamsukuma kuchimba ili kujua ukweli, kwa kuweka upendeleo wake pembeni na kulikabili jambo kama ni jipya kwake.

Mtu hapaswi kupinga au kukataa wazo kwa sababu ya sifa za mtu aliyetoa wazo hilo au kukubaliana na kitu kwa sababu kimetolewa na wenye mamlaka. Bali mtu anapaswa kufanya uchunguzi kujua kama kitu ni kweli, maana ukweli huwa upo wazi pale njia sahihi zinapofuatwa.

Kama mtu anakubaliana na kitu kwa sababu tu hakipaswi kuhojiwa, mtu huyo anakuwa amekubali kwamba kitu hicho siyo kweli. Ukweli huwa hauhitaji kulindwa wala kutetewa, ukweli huwa upo wazi na ukichunguzwa unabaki kuwa ukweli. Lakini uongo unajua ukichunguzwa utajulikana, hivyo nguvu kubwa hutumika kuulinda ili usihojiwe au kuchunguzwa.

Hatua ya kwanza ya kuufikia ukweli ni kuwa na mashaka kwa kila jambo ambalo hujathibitisha ukweli wake. Mafunzo ya Chang-Tsai yanaeleza: “Kama unaweza kuwa na mashaka pale wengine wanapokuwa na uhakika, unakuwa kwenye nafasi ya kupiga hatua.


Kuhofia ukweli.

Tunajifunza kwenye historia kwamba kwenye kila zama, watu wengi huwa wanakuwa upande usio wa ukweli. Wengi hupokea kile wanachoambiwa na mamlaka bila ya kukihoji, kwa sababu mamlaka huwa zinapenda utii wa watu na kama watu wakijua ukweli, hawatakuwa na utii ambao mamlaka hizo zinataka.

Tunajifunza zaidi kwenye historia kwamba pale ukweli unapofichwa, matokeo yanayopatikana huwa siyo mazuri. Madhara yote makubwa ambayo yametokea duniani, yalianza na kufichwa kwa ukweli.

Pale baadhi ya vitu vinapochukuliwa kama ni vitakatifu na mwiko kuhojiwa, ndipo uongo hupata nafasi ya kukua na kuleta madhara makubwa. Ukweli huwa hauogopi kuhojiwa au kuchunguzwa.

Watu wengi huwa wanahofia ukweli kwa sababu wanajua unavuruga uhakika ambao tayari wamejijengea, hivyo huendelea kujilisha na kuamini uongo ili kutotikisa kile ambacho wamekiamini maisha yao yote.

Njia ya uhakika ya kuyafanya maisha kuwa bora ni mtu kuyakabili maisha kwa kufungua macho yake na kuutafuta ukweli, badala ya kuyaendea maisha kama kipofu au mlevi.

Ni mara chache sana utakutana na mtu ambaye swali lake la kwanza kwa kila anachokabiliana nacho ni; je ni kweli? Kama swali hilo halijawa sehemu ya mtu, ni dhahiri ukweli siyo kipaumbele kwa mtu huyo na kupiga hatua itakuwa vigumu kwake.

Hatari kubwa kwenye maisha ni pale historia inapopindishwa na ukweli kufichwa ili kuwapa watu matumaini fulani. Ni kosa linaloleta madhara makubwa lakini limekuwa linarudiwa kila mara.

Serikali au taasisi kwa nia njema zinaweza kuchagua kuficha ukweli fulani ili kuzuia wananchi wasitaharuki na kukata tamaa, lakini hilo huwa linaleta madhara makubwa kutokana na ukweli unaofichwa.

Ukweli haupaswi kufichwa kwa namna yoyote ile, ukweli unapaswa kuwa wazi kwa sababu ndiyo njia pekee ya watu kuwa huru.


Mwenendo wa udikteta.

Tunajifunza kutoka kwenye historia kwamba madikteta huwa wanafuata mwenendo unaofanana.

Katika kuingia kwenye madaraka;

1. Huonesha utawala uliopo au uliokuwepo kabla yao haukuwa mzuri au kutengeneza uhasama baina ya makundi ya watu.

2. Huahidi mambo makubwa na yasiyo na ukomo, ambayo huwa hawawezi kuja kuyatimiza.

3. Hudai kwamba wanataka madaraka kamili na yasiyohojiwa (absolute power) kwa kipindi kifupi, ili kuinyoosha nchi, lakini wakishayapata madaraka hayo huwa hawayaachii.

4. Huwa wanatengeneza hali ya wananchi kuwaonea huruma kwa kutengeneza njama feki dhidi yake na hivyo kutaka apate madaraka zaidi. Hutaka watu wawaonee huruma kwa kuwa wanajitoa kwa ajili yao na kujitoa kwao kunawaweka kwenye hatari.

Katika kubaki kwenye madaraka.

1. Huanza kuwaondoa wale waliowasaidia kuingia madarakani na kuonesha kwamba ni wasaliti.

2. Hukandamiza ukosoaji na kuwaadhibu wale wote wanaozipinga au kuzikosoa sera zao, hata kama wanachosema ni kweli.

3. Huweka dini upande wao na kuhakikisha viongozi wa dini wanakuwa watiifu kwao na inaposhindikana kwa dini zilizopo huwa tayari kuchochea kuanzishwa kwa dini mpya zinazotimiza matakwa yao.

4. Huwa wanatumia fedha za umma kwenye miradi mikubwa na inayoonekana na kujisifia wameleta maendeleo kama fidia ya uhuru ambao wanakuwa wameupora kwa umma.

5. Huwa wanaichezea sarafu na kufanya uchumi wa nchi uonekane unakua vizuri tofauti na uhalisia.

6. Huwa wanaanzisha vita au uadui na mataifa mengine au kukuza migogoro fulani kama njia ya kuwafanya watu wasione uhalisia wa mambo yanayoendelea ndani. Hutumia njia hiyo kuhamisha hasira za wananchi kutoka kwenye uongozi wake na kwenda kwenye adui aliyetengenezwa.

7. Husisitiza sana kuhusu uzalendo na kuutumia huo kama njia ya kuwafanya watu kuwa watiifu kwake, wale wanaompinga wanaonekana siyo wazalendo.

8. Hujijengea umaarufu binafsi na kufanya yale yanayowafurahisha watu ili tu kuendelea kubaki kwenye madaraka, kitu kinachopelekea kwenye anguko lao.

Mwenendo huu umekuwa unarudiwa tangu enzi na enzi na bado watu wamekuwa hawajifunzi mapema na kuchukua hatua sahihi.


Mienendo isiyo sahihi.

Pamoja na maendeleo makubwa ambayo dunia imepiga, hasa kwenye mfumo wa demokrasia, kumekuwa na mienendo isiyo sahihi ambayo mwandishi alikuwa anaiona katika kipindi chake. Mienendo hiyo mpaka sasa ipo na imekuwa siyo kiashiria kizuri.

1. Urasimu umekuwa mkubwa kitu kinachochelewesha kufikiwa kwa maamuzi mbalimbali.

2. Baadhi ya viongozi wamekuwa wanajijengea sifa binafsi na kuzitumia kuminya demokrasia.

3. Chaguzi nyingi zimekuwa siyo huru na za haki kama demokrasia inavyotaka.

4. Propaganda zimekuwa ni nyingi katika kuwashawishi wananchi kukubaliana na vitu fulani, wao wanaona ni maamuzi yao kumbe wameathiriwa na propaganda.

5. Udhibiti wa usambaaji wa maarifa na taarifa umekuwa mkubwa kitu kinachohatarisha upatikanaji wa ukweli.

Mfumo wa demokrasia unapaswa kulindwa na kila mtu kwa sababu ni rahisi watu kuutumia vibaya na kutekeleza maslahi yao na hata kubadili mfumo na kuwa wa kidikteta.

Viashiria vya hayo ni vingi kwa zama tunazoishi sasa.

Rafiki, karibu usome uchambuzi kamili wa kitabu hiki ambao unatuonesha jinsi ambavyo hatujifunzi kutoka kwenye historia na hivyo kurudia makosa yale yale.
Duuuuuuuh mbona jiwe kwa sifa hizi alikuwa dictotar haswaa
 
Back
Top Bottom