kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,301
- 12,600
Wamarekani na wazungu wengi huwa hawajui kile serikali zao zinachokifanya kwenye mataifa mengine, lakini safari hii ni tofauti sana, wameanza kuufahamu upuuzi wanaofanya wanasiasa wao kwa wengine. Na hii ni baada ya maisha Yao kuguswa na kupanda kwa gharama za maisha kunakotokana na uhaba wa ngano, mafuta ya kupikia, gesi ya kupikia, petrol, umeme na wakimbizi wengi ambao ni wazungu wenzao kwenye mitaa Yao. Imewalqzimu kuutafuta ukweli kuhusu wanasiasa wao na sera zao za mambo ya nje.
Wazungu wengi ndio kwanza wanagundua kuwa kumbe nchi zao zinakopa ili kusaidia kutoa misaada kwa nchi nyingine. Wanagundua kuwa kumbe Kodi zao hazitumiki vizuri bali zinatumika kugharamia vita visivyowahusu.
Vita hii inaweza kuusambaratisha umoja wa Ulaya EU kama hawatakuwa makini, vita hii inaweza kumuondoa madarakani Joe Biden, Boris Johnson na wengine kama yule chancellor wa ujerumami na yule wa Italy.
Vikwazo vyote dhidi ya Urusi vinarudi kwenye nchi zao na watu wao, hii haijawahi kutokea kwao huko nyuma wakati wanaziwekea vikwazo nchi nyingine kama Iran, somalia, Ethiopia, north Korea, au Venezuela.
Wazungu lazima watalazimika kuachana na vita hii maana baadhi ya washirika wa NATO wamegundua kuwa vita hii inanufaisha makampuni ya silaha ya kimarekani .
Wazungu wengi ndio kwanza wanagundua kuwa kumbe nchi zao zinakopa ili kusaidia kutoa misaada kwa nchi nyingine. Wanagundua kuwa kumbe Kodi zao hazitumiki vizuri bali zinatumika kugharamia vita visivyowahusu.
Vita hii inaweza kuusambaratisha umoja wa Ulaya EU kama hawatakuwa makini, vita hii inaweza kumuondoa madarakani Joe Biden, Boris Johnson na wengine kama yule chancellor wa ujerumami na yule wa Italy.
Vikwazo vyote dhidi ya Urusi vinarudi kwenye nchi zao na watu wao, hii haijawahi kutokea kwao huko nyuma wakati wanaziwekea vikwazo nchi nyingine kama Iran, somalia, Ethiopia, north Korea, au Venezuela.
Wazungu lazima watalazimika kuachana na vita hii maana baadhi ya washirika wa NATO wamegundua kuwa vita hii inanufaisha makampuni ya silaha ya kimarekani .