Vita ya Ethiopia: Waafrika ni lini tutaacha unafiki?

Peter Agostino

Senior Member
Sep 23, 2016
105
226
Mpaka sasa hivi sijasikia Taifa lolote la Kiafrika likitaja waziwazi kusimama na Taifa la Ethiopia katika vita yake na Waasi wa Tigray zadi ya kila mtu kufuata mkumbo wa Mataifa ya Magharibi kudai , OO... haki za binadamu zinavunjwa Tigray, Aby Ahmed akae meza moja na Waasisi kusuluhisha na hata kufikia hatua ya kuondoa raia zao Adis Ababa kwa propaganda za waasi kuwazidi nguvu Serikali halali. Hivi wakati Abraham Lincoln alipokuwa akipigana na Waasi Marekani karne ya 19 kuna mahali ulisikia alikaa nao meza moja kujadiliana? Mbona Wamarekani walipigana hadi Taifa lao leo ni moja na wanatetea umoja huo kwa udi na uvumba?

Waafrika hebu tuamke tuwe kitu kimoja. Tulimwacha Muamar Gadafi akauwawa hivihivi na hatuoni Libya mpaka leo ikiwa salama, hali ni hiyohiyo katika Mataifa mengine mengi Mataifa ya Magharibi walikojidai wanapeleka demokrasia yao. Hata Mataifa ya jirani kabisa kama Tanzania, Kenya, Uganda nK. ambayo kimsingi yalipaswa angalao hata kuonyesha mshikamano wao kwa kuwakemea waasi wanaotaka kuisambaratisha Ethiopia wamenyamaza kimya wakiogopa Marekani na wenzake. Kwanini Mataifa ya Afrika tusisimame na China kukataa Nchi zetu kuingiliwa na Mataifa ya nje?

Hakuna Taifa Duniani lingekubali hata siku moja uasi wa eneo lake moja kujitenga, hata Umoja wa Ulaya wenyewe japo siyo nchi lakini Uingereza ilipoamua tu kujimega EU iliweka vipingamizi kibao. Marekani hata sijawahi kusikia mtu aliyejaribu kuzungumzia jimbo fulani kujitenga sembuse kutumia vikosi vyake kushambulia serikali kuu ya Washington. Sasa iweje uasi ukitokea tu Afrika Rais Halali akiukandamiza ananyang'anywa hadi nishani ya Nobeli waliyompa wenyewe? Kumbe ilikuwa ni janja yao kumnyamazisha aendelee kutetea maslahi yao. Aby awarudishie linishani lao, Waafrika tuungane naye kuitetea Ethiopia moja na wala siyo vipandevipande vya Ethiopia.
 
Africa vibaraka wengi sana kiasi umelimega bara vipandevipande.

ndo maana ni ngumu sana kwa maraisi wa Africa kukaa meza moja wakajadili wakaelewana kwa maslahi ya bara letu,

wengi wanawaza misaada na mikopo ili kujiimarisha kisiasa nchini mwao na vyama vyao, linapokuja suala la kupigania mslahi ya Africa kwa waafrika akipigwa mkwara na western country wanaufyata, utumwa tumejipa wenyewe

hivyo ni ngumu sana Africa kusolve matatizo ya vita Africa au udictator.

Akili zinawaza starehe kuliko kujikomboa
 
Nasikitika kuona wewe siyo mfuatiliaje wa huu Mgogoro wa Ethiopia . Aby Ahmed kakataa suluu ,kuna viongozi wengi wametumwa kwenda kutatua mgogoro imeshindikani.

Aby Ahmed kuna mazuri kafanya pia kuna mabaya kafanya

Kama aliweza kutatua mgogoro kati ya Ethiopia na Eritrea wa muda mrefu ameshindwaje kutatua mgogoro wa ndani wa Nchi yake.
 
Nasikitika kuona wewe siyo mfuatiliaje wa huu Mgogoro wa Ethiopia . Aby Ahmed kakataa suluu ,kuna viongozi wengi wametumwa kwenda kutatua mgogoro imeshindikani.
Aby Ahmed kuna mazuri kafanya pia kuna mabaya kafanya
Kama aliweza kutatua mgogoro kati ya Ethiopia na Eritrea wa muda mrefu ameshindwaje kutatua mgogoro wa ndani wa Nchi yake.
Lakini ukumbuke Watigray walikuwa na matakwa yao tokea mwanzo wa mgogoro huu na ndio walioanza kukataa usuluhishi Serikali iliporudi nyuma baada ya waasi kuonyesha kutaka kushinda. Hivi hata ungekuwa ni wewe kiongozi wa nchi ungekubali kutii masharti ya kikundi cha waasi kisa tu ni watu wenye nguvu waliokamata madaraka ya nchi kwa miongo 3?

Suluhu pekee ambayo wangekubali Watigray ni kurejeshewa mamlaka waliyokuwa nayo awali kabla ya Aby kushika madaraka kitu ambacho hakuna Rais duniani angekubali. Wakati nchi ya Ethiopia ina makabila mengine mengi tu makubwa. Ni kitu kigumu sana kumnyang'anya paka au mnyama yeyote yule mkali kitoweo alichozowea siku zote, ni lazima akuparure makucha na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Watigray, wasingekubali usulihishi wa kina Obasanjo zaidi ya suluhisho la kijeshi. Ungezungumza vipi na watu walioamua kupora silaha za jeshi la Taifa kisa hawataki kufuata katiba ya nchi kwa kisingizio cha haki za kabila?
 
Nasikitika kuona wewe siyo mfuatiliaje wa huu Mgogoro wa Ethiopia . Aby Ahmed kakataa suluu ,kuna viongozi wengi wametumwa kwenda kutatua mgogoro imeshindikani.
Aby Ahmed kuna mazuri kafanya pia kuna mabaya kafanya
Kama aliweza kutatua mgogoro kati ya Ethiopia na Eritrea wa muda mrefu ameshindwaje kutatua mgogoro wa ndani wa Nchi yake.
Na ukumbuke pia siyo TPLF ya Watigray tu, kuna makundi mengine kibao kama Waoromia na Wasomali ambao walikuwa wakisubiri tu kuona jinsi ambavyo Aby angefyata mkia kisha na wao wachomoze pembe zao. Na hata hivyo tayari wameshaanza kuwaunga mkono TPLF. Kwa hiyo unataka kuniambia Aby atafanya mazungumzo ya usuluhishi na makundi mangapi? Mbona Mawaziri wakuu waliopita kama kina Zenawi na wenzie hawakuvumilia makundi hayo na Serikali za Mangaribi zilikuwa zikiwakumbatia? au ni kwa vile walikuwa tabaka tawala la Watigray?
 
Nasikitika kuona wewe siyo mfuatiliaje wa huu Mgogoro wa Ethiopia . Aby Ahmed kakataa suluu ,kuna viongozi wengi wametumwa kwenda kutatua mgogoro imeshindikani.
Aby Ahmed kuna mazuri kafanya pia kuna mabaya kafanya
Kama aliweza kutatua mgogoro kati ya Ethiopia na Eritrea wa muda mrefu ameshindwaje kutatua mgogoro wa ndani wa Nchi yake.
Kitendo cha kuvamia kambi ya jeshi ni uasi tosha kabisa.kama walikuwa wanapigana kwa ajili ya kujilinda,iweze wavamie majimbo mengine kama Amhara na Afar.kwanza unatakiwa ujue kuwa awa ndo watu wa kwanza kupinga wazi wazi mapatano ya amani kati Ethiopia na Eritrea.wao walikuwa wanataka Eritrea aendelee kuwa adui yao wakati si jambo zuri kugombana na jirani yako.sasa watu kama awa Amani gani ya kupatanishwa wanaitaka?.

Abby anataka kufuta mambo ya ukabila na kutengeneza taifa moja lenye nguvu moja na sauti ya watu wote.ndo maana alianza kubana watu wa kabila lake ili iwe mfano tosha kwa watu wengine.Wa-Ethiopia wengi wanajua kabisa Abby ni kiongozi ambaye yupo kwa ajili ya watu wote na wala sio kabila fulani.
 
Kitendo cha kuvamia kambi ya jeshi ni uasi tosha kabisa.kama walikuwa wanapigana kwa ajili ya kujilinda,iweze wavamie majimbo mengine kama Amhara na Afar.kwanza unatakiwa ujue kuwa awa ndo watu wa kwanza kupinga wazi wazi mapatano ya amani kati Ethiopia na Eritrea.wao walikuwa wanataka Eritrea aendelee kuwa adui yao wakati si jambo zuri kugombana na jirani yako.sasa watu kama awa Amani gani ya kupatanishwa wanaitaka?.

Abby anataka kufuta mambo ya ukabila na kutengeneza taifa moja lenye nguvu moja na sauti ya watu wote.ndo maana alianza kubana watu wa kabila lake ili iwe mfano tosha kwa watu wengine.Wa-Ethiopia wengi wanajua kabisa Abby ni kiongozi ambaye yupo kwa ajili ya watu wote na wala sio kabila fulani.
Asante, na mifano tunaiona wenyewe hapahapa kwetu, Iddi Amini alipodaiwa kutaka kuimega ardhi ya Kagera, uliona Mwalimu alivyoungwa mkono na wananchi wa kawaida? Vipi kuhusiana na Zanzibar? nadhani tumewahi kusikia kilichowahi kuwapata baadhi ya watu/viongozi waliojaribu kuamsha chockochoko za kisiwa hicho kutaka kuwa nchi inayojitegemea. Hapo Kenya halikadhalika Mombasa Republic uliona Kenyata akiwachekea meno? Sasa iweje eti Aby awachekee meno TPLF huku Mataifa ya Magharibi yakishadidia Aby kusalimu amri? Aby asingelikuwa sahihi Wananchi wa Ethiopia wasingeliandamana kila kona kutaka kwenda mstari wa mbele kuitetea nchi yao.
 
Kitendo cha kuvamia kambi ya jeshi ni uasi tosha kabisa.kama walikuwa wanapigana kwa ajili ya kujilinda,iweze wavamie majimbo mengine kama Amhara na Afar.kwanza unatakiwa ujue kuwa awa ndo watu wa kwanza kupinga wazi wazi mapatano ya amani kati Ethiopia na Eritrea.wao walikuwa wanataka Eritrea aendelee kuwa adui yao wakati si jambo zuri kugombana na jirani yako.sasa watu kama awa Amani gani ya kupatanishwa wanaitaka?.

Abby anataka kufuta mambo ya ukabila na kutengeneza taifa moja lenye nguvu moja na sauti ya watu wote.ndo maana alianza kubana watu wa kabila lake ili iwe mfano tosha kwa watu wengine.Wa-Ethiopia wengi wanajua kabisa Abby ni kiongozi ambaye yupo kwa ajili ya watu wote na wala sio kabila fulani.
Ukweli huu watu wengi hatutaki kuusikia kabisa !
 
Asante, na mifano tunaiona wenyewe hapahapa kwetu, Iddi Amini alipodaiwa kutaka kuimega ardhi ya Kagera, uliona Mwalimu alivyoungwa mkono na wananchi wa kawaida? Vipi kuhusiana na Zanzibar? nadhani tumewahi kusikia kilichowahi kuwapata baadhi ya watu/viongozi waliojaribu kuamsha chockochoko za kisiwa hicho kutaka kuwa nchi inayojitegemea. Hapo Kenya halikadhalika Mombasa Republic uliona Kenyata akiwachekea meno? Sasa iweje eti Aby awachekee meno TPLF huku Mataifa ya Magharibi yakishadidia Aby kusalimu amri? Aby asingelikuwa sahihi Wananchi wa Ethiopia wasingeliandamana kila kona kutaka kwenda mstari wa mbele kuitetea nchi yao.
Unajuwa Kitu alichokifanya Aby kutatua mgogoro na Eritrea
Kuna eneo lilikuwa linamilikiwa na Watigray walilipigania ilo eneo Damu nyingi za ndugu zao zilimwaga kupata ilo eneo. Vilipigwa vita na Eritrea Na kushindwa.
Inakuwaje kiongozi kama Aby Ahmed aliyehapa kulindi katiba na mipaka ya Nchi anatoe eneo kwa Eritrea wakati kuna wa Tigray wamemwaga Damu zao kwa ajili ya ilo eneo.

Aby Ahmed anastaili kuwa kiongozi wa Nchi. Itokee hapa kwetu Rais aje na kutoa mkoa wa Kagera kuwa sehem ya Uganda au ziwa nyasa kuwa sehemu ya Malawi. Rais kashindwa kulinda mipk ya Nchi
 
Kitendo cha kuvamia kambi ya jeshi ni uasi tosha kabisa.kama walikuwa wanapigana kwa ajili ya kujilinda,iweze wavamie majimbo mengine kama Amhara na Afar.kwanza unatakiwa ujue kuwa awa ndo watu wa kwanza kupinga wazi wazi mapatano ya amani kati Ethiopia na Eritrea.wao walikuwa wanataka Eritrea aendelee kuwa adui yao wakati si jambo zuri kugombana na jirani yako.sasa watu kama awa Amani gani ya kupatanishwa wanaitaka?.

Abby anataka kufuta mambo ya ukabila na kutengeneza taifa moja lenye nguvu moja na sauti ya watu wote.ndo maana alianza kubana watu wa kabila lake ili iwe mfano tosha kwa watu wengine.Wa-Ethiopia wengi wanajua kabisa Abby ni kiongozi ambaye yupo kwa ajili ya watu wote na wala sio kabila fulani.
Maelezo yamejitosheleza.
 
Nasikitika kuona wewe siyo mfuatiliaje wa huu Mgogoro wa Ethiopia . Aby Ahmed kakataa suluu ,kuna viongozi wengi wametumwa kwenda kutatua mgogoro imeshindikani.
Aby Ahmed kuna mazuri kafanya pia kuna mabaya kafanya
Kama aliweza kutatua mgogoro kati ya Ethiopia na Eritrea wa muda mrefu ameshindwaje kutatua mgogoro wa ndani wa Nchi yake.

Ethiopia na Eritrea ni nchi mbili tofauti so vita haikuwa na faida hata angepigana akashinda hakuna ambacho angepata ila kuruhusu kuongea na waasi wa ndani ya nchi ni kuruhusu watu wengine kuasi pia wakitegemea watakaa wazungumze na madhara ya mazungumzo huwa yanalenga kila mtu anufaike, je unayajua madai ya tplf , so ili tplf anufaike lazima madai yake yapewe sikio na madai yenyewe ni ya kipuuzi ( kama unaujua mgogoro ulipoanzia) Serikali ilihailisha uchaguzi kwa sababu ya mlipuko wa corona na kusogeza mbele tarehe ya uchaguzi ila watigray walifanya uchaguz bila baraka za serikali kuu, yaan Kwenu chitohori wajifanyie vitu watakavyo tu bila ridhaa ya serikali kuu, je nini umuhimu wa serikali kuu kama mnajifanyia mtakavyo?

Turudi kwenye hoja so ili tplf anufaike lzma uchaguzi ilifanywa awali bila ridhaa ya serikali kuu , ubarikiwe na serikali kuu kwenye meza ya mazungumzo, je hiyo inaleta picha gani kama taifa kwa siku za usoni , huoni wakati mwingine serikali utapoteza heshima kwa serikali za majimbo? So unachopaswa kujua serikali haipigani kuteka Jimbo ya tigray maana walifanya hivyo awali na wakaliachia , ila serikali ya ethiopia inapigania dignity ( heshima) ambayo ni moja ya elements of state ( dutu zinazounda taifa kamili ) .
 
Kitendo cha kuvamia kambi ya jeshi ni uasi tosha kabisa.kama walikuwa wanapigana kwa ajili ya kujilinda,iweze wavamie majimbo mengine kama Amhara na Afar.kwanza unatakiwa ujue kuwa awa ndo watu wa kwanza kupinga wazi wazi mapatano ya amani kati Ethiopia na Eritrea.wao walikuwa wanataka Eritrea aendelee kuwa adui yao wakati si jambo zuri kugombana na jirani yako.sasa watu kama awa Amani gani ya kupatanishwa wanaitaka?.

Abby anataka kufuta mambo ya ukabila na kutengeneza taifa moja lenye nguvu moja na sauti ya watu wote.ndo maana alianza kubana watu wa kabila lake ili iwe mfano tosha kwa watu wengine.Wa-Ethiopia wengi wanajua kabisa Abby ni kiongozi ambaye yupo kwa ajili ya watu wote na wala sio kabila fulani.
Genius 100%
 
Unajuwa Kitu alichokifanya Aby kutatua mgogoro na Eritrea
Kuna eneo lilikuwa linamilikiwa na Watigray walilipigania ilo eneo Damu nyingi za ndugu zao zilimwaga kupata ilo eneo. Vilipigwa vita na Eritrea Na kushindwa.
Inakuwaje kiongozi kama Aby Ahmed aliyehapa kulindi katiba na mipaka ya Nchi anatoe eneo kwa Eritrea wakati kuna wa Tigray wamemwaga Damu zao kwa ajili ya ilo eneo.

Aby Ahmed anastaili kuwa kiongozi wa Nchi. Itokee hapa kwetu Rais aje na kutoa mkoa wa Kagera kuwa sehem ya Uganda au ziwa nyasa kuwa sehemu ya Malawi. Rais kashindwa kulinda mipk ya Nchi
usidanganye umma boss , Aby hawez fanya ujinga kama huo , lile eneo ni la Eritrea na historia inaeleweka tu
 
Mpaka sasa hivi sijasikia Taifa lolote la Kiafrika likitaja waziwazi kusimama na Taifa la Ethiopia katika vita yake na Waasi wa Tigray zadi ya kila mtu kufuata mkumbo wa Mataifa ya Magharibi kudai , OO... haki za binadamu zinavunjwa Tigray, Aby Ahmed akae meza moja na Waasisi kusuluhisha na hata kufikia hatua ya kuondoa raia zao Adis Ababa kwa propaganda za waasi kuwazidi nguvu Serikali halali. Hivi wakati Abraham Lincoln alipokuwa akipigana na Waasi Marekani karne ya 19 kuna mahali ulisikia alikaa nao meza moja kujadiliana? Mbona Wamarekani walipigana hadi Taifa lao leo ni moja na wanatetea umoja huo kwa udi na uvumba?

Waafrika hebu tuamke tuwe kitu kimoja. Tulimwacha Muamar Gadafi akauwawa hivihivi na hatuoni Libya mpaka leo ikiwa salama, hali ni hiyohiyo katika Mataifa mengine mengi Mataifa ya Magharibi walikojidai wanapeleka demokrasia yao. Hata Mataifa ya jirani kabisa kama Tanzania, Kenya, Uganda nK. ambayo kimsingi yalipaswa angalao hata kuonyesha mshikamano wao kwa kuwakemea waasi wanaotaka kuisambaratisha Ethiopia wamenyamaza kimya wakiogopa Marekani na wenzake. Kwanini Mataifa ya Afrika tusisimame na China kukataa Nchi zetu kuingiliwa na Mataifa ya nje?

Hakuna Taifa Duniani lingekubali hata siku moja uasi wa eneo lake moja kujitenga, hata Umoja wa Ulaya wenyewe japo siyo nchi lakini Uingereza ilipoamua tu kujimega EU iliweka vipingamizi kibao. Marekani hata sijawahi kusikia mtu aliyejaribu kuzungumzia jimbo fulani kujitenga sembuse kutumia vikosi vyake kushambulia serikali kuu ya Washington. Sasa iweje uasi ukitokea tu Afrika Rais Halali akiukandamiza ananyang'anywa hadi nishani ya Nobeli waliyompa wenyewe? Kumbe ilikuwa ni janja yao kumnyamazisha aendelee kutetea maslahi yao. Aby awarudishie linishani lao, Waafrika tuungane naye kuitetea Ethiopia moja na wala siyo vipandevipande vya Ethiopia.
Binadamu yeyote ambae ni mwafrika huwa ana laana ya unafiki Kwa asilimia 99
 
Ethiopia na Eritrea ni nchi mbili tofauti so vita haikuwa na faida hata angepigana akashinda hakuna ambacho angepata ila kuruhusu kuongea na waasi wa ndani ya nchi ni kuruhusu watu wengine kuasi pia wakitegemea watakaa wazungumze na madhara ya mazungumzo huwa yanalenga kila mtu anufaike , je unayajua madai ya tplf , so ili tplf anufaike lazima madai yake yapewe sikio na madai yenyewe ni ya kipuuz ( kama unaujua mgogoro ulipoanzia ) Serikali ilifuta uchaguzi kwa sababu ya mlipuko wa corona na kusogeza mbele tarehe ya uchaguzi ila watigray walifanya uchaguz bila baraka za serikali kuu , yaan Kwenu chitohori wajifanyie vitu watakavyo tu bila ridhaa ya serikali kuu , je nini umuhimu wa serikali kuu kama mnajifanyia mtakavyo ? , turudi kwenye hoja so ili tplf anufaike lzma uchaguzi ilifanywa awali bila ridhaa ya serikali kuu , ubarikiwe na serikali kuu kwenye meza ya mazungumzo , je hiyo inaleta picha gani kama taifa kwa siku za usoni , huoni wakati mwingine serikali utapoteza heshima kwa serikali za majimbo ? So unachopaswa kujua serikali haipigani kuteka Jimbo ya tigray maana walifanya hivyo awali na wakaliachia , ila serikali ya ethiopia inapigania dignity ( heshima) ambayo ni moja ya elements of state ( dutu zinazounda taifa kamili ) .
Sasa hivi vita vinapigwa Ethiopia kwani Corona hakuna
Kwa nini Aby asisitishe vita kwa sababu Corona ipo
Aby Ahmed atabaki kuwa kiongozi wa hovyo ameharibu Taifa la Ethiopia.

Atazuia vipi uchaguzi kisa Corona alikuwa anafuata matakwa ya Nchi za magharibi, sasa hivi anaona jinsi walivyomgeuka.

Ethiopia wiki zilizopita kulikuwa na maandamono ya kumuunga Aby Ahmed Corona ilikuwepo kwa nini asizuie haya maandamano ya kuunga mkono Serikali yake.

Aby Ahmed alikuwa ni Mtu kama mwenye kisasi kwa Tigray
Watigray hawawezi kusalimu amri chini ya uongozi wa Aby Ahmed, mgogoro ule utaendelea faida itakuwa ya Nani.
Unazuia uchaguzi kwa sababu ya Corona kama siyo chuki zake binafsi Watigray wapo 06%
 
Sasa hivi vita vinapigwa Ethiopia kwani Corona hakuna
Kwa nini Aby asisitishe vita kwa sababu Corona ipo
Aby Ahmed atabaki kuwa kiongozi wa hovyo ameharibu Taifa la Ethiopia.

Atazuia vipi uchaguzi kisa Corona alikuwa anafuata matakwa ya Nchi za magharibi, sasa hivi anaona jinsi walivyomgeuka.

Ethiopia wiki zilizopita kulikuwa na maandamono ya kumuunga Aby Ahmed Corona ilikuwepo kwa nini asizuie haya maandamano ya kuunga mkono Serikali yake.

Aby Ahmed alikuwa ni Mtu kama mwenye kisasi kwa Tigray
Watigray hawawezi kusalimu amri chini ya uongozi wa Aby Ahmed, mgogoro ule utaendelea faida itakuwa ya Nani.
Unazuia uchaguzi kwa sababu ya Corona kama siyo chuki zake binafsi Watigray wapo 06%
Hv unahisi angenufaikaje kwa kupeleka uchaguzi mbele , ethiopia sio bongo
 
SASA TUTETEE UPANDE GANI? WA ABIY AU WA TIGRAY? :oops:
Tetea upande wa Tigray
Kazuia uchaguzi wa Tigray kwa sababu ya Corona, Corona ipo mpaka Leo inamaana uchaguzi usingefanyika?
Kapeleka wanajeshi kupigana na Watigray hatari ya Corona hajaiona
Aby Ahmed alikuwa na chuki binafsi na Watigray
 
Back
Top Bottom