Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
.
Baraza la wafamasia (Pharmacy Council) liliaanzishwa kwa sheria ya Bunge namba 7 ya mwaka 2002.TFDA ilianzishwa kwa sheria ya Bunge namba 1 ya mwaka 2003. Vikiwa ni vyombo viwili vyenye majukumu tofauti.
Kutokana na kungangania kinachoitwa ulaji na visa yapo majukumu ya TFDA yamechukuliwa na kupelekwa Pharmacy Council ambako sasa afya ya mtanzania haina mwenyewe.
Kitu kilicho cha ajabu ni kuwa TFDA toka ilipoanzishwa ilitengeneza mfumo ambao usajiri wa awali na usimamizi wa awali ulifanywa na wafamasia wa wilaya mpaka mkoa kasha TFDA makao makuu ukishirikina na timu ya afanyakazi wa TFDA katika ngazi mbalimbali. TFDA pia ilianza kujengewa nguvu ya rasilimali watu ambapo ilikuwa na hadi sasa inao wafanyakazi wengi wenye utaalamu katika fani mbalimbali kuanzia zile za chakula, dawa, vifaa tiba na vipodozi.
Hivi karibuni Pharmacy Council wamechukua jukumu la kusimamia maduka yote ya Dawa (Pharmacy), maduka ya dawa muhimu (Accredited Drugs Dispensing Outlet-ADDO) na Maduka ya dawa baridi ambayo awali lilikuwa chini ya TFDA; kituko cha ajabu Pharmacy Council hakina wafanyakazi wanaozidi hata 30 kama siyo 20. Tetesi zinasema kisa cha hayo ni kuwa Pharmacy Council walikuwa hawana hela/ulaji waliamua kuchukua ili na wapate ulaji na si kuwaachia TFDA kila kitu. Na la pili kulikuwa na watu wana-madeal ya kuanzisha maduka makubwa ya dawa na kupitisha dawa zao, hivyo kama zingekuwa chini ya TFDA ilikuwa ni kikwazo kwao. Kwani Mkurugenzi aliyekuwepo alikuwa kigingi kwao.
Kitu cha ajabu ni hiki maduka ya dawa yanafunguliwa hakuna udhibiti, ukaguzi wala usimamizi. Mfano tu Dare s salaam yenye karibu asilimia 80 ya Pharmacy zote nchini ambazo zinakadoriwa kufika kama si kuzidi 500, na maduka kadhaa ya Dawa Muhimu pamoja na utitiri wa maduka ya Dawa Baridi; kwa idadi ya staff waliyonayo pharmacy Council hawawezi kumaliza hata tukiwapa miaka miwili tu kukagua maduka yote ya Dar pekee.
Swali la ziada nini kuhusu ya mikoani? Ni nani anayeweza kuwakamata wafanyabiashara wa dawa bandia na zilizoharibika? Je ni watanzania wangapi wanaaathirika kama si kufa kutokana na kungangania majukumu ambayo hawayawezi?
Huku mtaani kuna madawa mengi sana feki na yaliyokwisha muda lakini bado yanauzwa.
Waliochangia kufika hapa tulipo ni Zarina Madabida (Mbunge viti maalumu-CCM), Ms Kinyawa (Mrajisi wa Baraza la wafamasia), Ms Blandina Nyoni (Katibu wa Wizara ya Afya aliyefukuzwa). Ambapo inatajwa kama tetesi kwamba kulikuwa na bifu la chini kwa chini kati ya Ms Nyoni na Ms Madabida dhidi ya Ms Ndomondo (aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TFDA {she has resigned})
Rejea comment alizotoa Z Madabida juu ya muswada wa marekebisho ya sheria ya Pharmacy Council wakati ukijadiliwa bungeni.
Baraza la wafamasia (Pharmacy Council) liliaanzishwa kwa sheria ya Bunge namba 7 ya mwaka 2002.TFDA ilianzishwa kwa sheria ya Bunge namba 1 ya mwaka 2003. Vikiwa ni vyombo viwili vyenye majukumu tofauti.
Kutokana na kungangania kinachoitwa ulaji na visa yapo majukumu ya TFDA yamechukuliwa na kupelekwa Pharmacy Council ambako sasa afya ya mtanzania haina mwenyewe.
Kitu kilicho cha ajabu ni kuwa TFDA toka ilipoanzishwa ilitengeneza mfumo ambao usajiri wa awali na usimamizi wa awali ulifanywa na wafamasia wa wilaya mpaka mkoa kasha TFDA makao makuu ukishirikina na timu ya afanyakazi wa TFDA katika ngazi mbalimbali. TFDA pia ilianza kujengewa nguvu ya rasilimali watu ambapo ilikuwa na hadi sasa inao wafanyakazi wengi wenye utaalamu katika fani mbalimbali kuanzia zile za chakula, dawa, vifaa tiba na vipodozi.
Hivi karibuni Pharmacy Council wamechukua jukumu la kusimamia maduka yote ya Dawa (Pharmacy), maduka ya dawa muhimu (Accredited Drugs Dispensing Outlet-ADDO) na Maduka ya dawa baridi ambayo awali lilikuwa chini ya TFDA; kituko cha ajabu Pharmacy Council hakina wafanyakazi wanaozidi hata 30 kama siyo 20. Tetesi zinasema kisa cha hayo ni kuwa Pharmacy Council walikuwa hawana hela/ulaji waliamua kuchukua ili na wapate ulaji na si kuwaachia TFDA kila kitu. Na la pili kulikuwa na watu wana-madeal ya kuanzisha maduka makubwa ya dawa na kupitisha dawa zao, hivyo kama zingekuwa chini ya TFDA ilikuwa ni kikwazo kwao. Kwani Mkurugenzi aliyekuwepo alikuwa kigingi kwao.
Kitu cha ajabu ni hiki maduka ya dawa yanafunguliwa hakuna udhibiti, ukaguzi wala usimamizi. Mfano tu Dare s salaam yenye karibu asilimia 80 ya Pharmacy zote nchini ambazo zinakadoriwa kufika kama si kuzidi 500, na maduka kadhaa ya Dawa Muhimu pamoja na utitiri wa maduka ya Dawa Baridi; kwa idadi ya staff waliyonayo pharmacy Council hawawezi kumaliza hata tukiwapa miaka miwili tu kukagua maduka yote ya Dar pekee.
Swali la ziada nini kuhusu ya mikoani? Ni nani anayeweza kuwakamata wafanyabiashara wa dawa bandia na zilizoharibika? Je ni watanzania wangapi wanaaathirika kama si kufa kutokana na kungangania majukumu ambayo hawayawezi?
Huku mtaani kuna madawa mengi sana feki na yaliyokwisha muda lakini bado yanauzwa.
Waliochangia kufika hapa tulipo ni Zarina Madabida (Mbunge viti maalumu-CCM), Ms Kinyawa (Mrajisi wa Baraza la wafamasia), Ms Blandina Nyoni (Katibu wa Wizara ya Afya aliyefukuzwa). Ambapo inatajwa kama tetesi kwamba kulikuwa na bifu la chini kwa chini kati ya Ms Nyoni na Ms Madabida dhidi ya Ms Ndomondo (aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TFDA {she has resigned})
Rejea comment alizotoa Z Madabida juu ya muswada wa marekebisho ya sheria ya Pharmacy Council wakati ukijadiliwa bungeni.