Vita vya uchumi: Tanzania inapigana na Mabeberu au inapigana na nchi jirani za Kiafrika?

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Hii dhana ya vita vya kiuchumi inachanganya sana. Maana ikiangaliwa kwa upande mmoja watu wengi hudhania kuwa vita hivi huwa vinapiganwa baina ya taifa maskini lenye rasilimali zake dhidi ya mataifa matajiri yenye nia ya kunyonya rasilimali zake.

Tafsiri sahihi vita vya kiuchumi ni mikakati au mbinu zinazoweza kutumiwa na taifa lolote kuweza kudidimiza uchumi wa taifa fulani. Mfano ni kuweka kikwazo au kususa kununua bidhaa za taifa fulani.

Sasa kama ndio hivyo sisi kama Taifa ambalo tunataka tupige hatua kiuchumi tuko kwenye vita kiuchumi na akina nani? Mabeberu? Au jirani zetu waafrika?

Ni wazi kuwa tunaweza kuwa kwenye uwezekano wa either mabeberu wanataka waje hapa kuchota rasilimali zetu tusiambulie chochote na uchumi wetu usikuwe. Pia huenda kuna jirani zetu, waafrika wenzetu hawataki tukuwe kiuchumi nao wanafanya kila mbinu tusifanikiwe.
 
Naona unanichanganya. Zilishikiliwa lini na mabeberu maana tumepata uhuru tangu 1961. Azimio la Arusha likafukuza ubepari hapa nchini mwaka 1967.
Hapo kati tulitishwa na mtaifa ya nje pamoja na mashirika ya fedha ya kimataifa, wakatupa masharti magumu ya kuuza rasilimali zetu zote kutoka mikononi mwa serikali na kwenda kwenye sekta binafsi.

Watanzania wengi wakati ule walikuwa hawana uwezo wakujimilikisha vitu kama migodi, mashamba, mawasiliano nk. Hapo ndio mabeberu wakazamia na kukomba kila kitu. Leo hii, tuko kwenye vita ya kukomboa rasilimali zetu na kujenga uchumi wetu kwa manufaa ya Watanzania wote.
 
Kuna mashiko kwenye fikra hii hasa ikizingatiwa kuwa Afrika haikuwahi kuwa huru katika nyanza zote zaidi ya siasa ambazo nazo zimezalisha wakoloni weusi katika nchi nyingi. Acheni ubishi kama hamjui someni. Afrika bado ni koloni kiuchumi hata kijamii kama mtaangalia madhara yaliyosababishwa na dini nyemelezi za kigeni.
 
Ngoja nami niweke mawili hapa.

1. Hii vita iliyotangazwa si vita ya kweli.
Ni kampeni ya hadaa tu kwa wananchi.

Ni njia ya kutafuta kukandamiza wenye maoni tofauti na yale ya watawala.

Hii ni zana ya kujiongezea umaarufu na kutafuta kupendwa. Haina tofauti yoyote na hadaa ya "wanyonge" tunaoambiwa ndio wanaopewa kipaumbele/upendeleo kuletewa maendeleo. Kwa ujumla ni kupumbaza wananchi kwa lengo la kuwakandamiza.

2. "Mabeberu" wanazo njia chungu nzima za kuharibu uchumi wa nchi yoyote wanayotaka kupambana nayo.

Siyo lazima waje hapa kubeba mavitu yetu ndio waweze kutumaliza.

Huu wimbo wa "mabeberu" ni kama yaleyale ya "vita vya kiuchumi". Tukilia MABEBERU - ni rahisi kwa watu kutuunga mkono, kwa sababu huko nyuma tulisha watemesha mabeberu nyongo. Sasa hivi ni wimbo tu, hakuna lolote linalofanyika.

3. Nchi za jirani, zinaweza sana kuwa sehemu ya kudidimiza uchumi wa nchi.

Chukulia mfano wa ushirikiano wa EAC. Mabeberu wanaweza kutumia baadhi ya washirika kudhoofisha mshirika wasiyemtaka.

Kuna baadhi ya nchi inawawekezaji wengi na wa siku nyingi ambao wana uraia wa nchi mbili. Nyumbani kwao ni ubeberuni, na nyumbani kwa kufanyia biashara ni kwenye ushirika wetu, sasa unaweza kujazia unayotaka kuyajazia kwenye hali ya namna hiyo.
Halafu wewe utabaki unaimba: "tunapigana vita vya kiuchumi", kumbe hata adui unayepigana naye humjui!

Mwisho ngoja niulize maksudi: Hivi "mabeberu" ni akina nani? Naona tunabatiza watu kwa rangi ya ngozi zao, au siyo?
 
Sie hatuna vita ya uchumi,sie tuna upuuzi mtupu wa vita Kati ya taasisi za serikali na wafanyabiashara,TRA na wafanyabiashara na makadirio ya Kodi,LATRA na wamiriki wa mabasi,TARURA na watu wa malori.

Huku kwetu ni mwendo wa kukomoana katika kusaka kodi zaidi,maana nchi ni hoehae,

Vita za uchumi zipo Kati ya Southafrika na Nigeria,maana hizi nchi zina makampuni makubwa yanayofsnya kazi ndani ya hizi nchi,MTN ya SA ipo Nigeria,Uganda,na nchi nyingine, SA na Nigeria Wana tengeneza bland kibao za magari lazima washindsnie soko.

Vita ya kiuchumi ipo Kati ya China na USA,china kuna Telecom giant Huawei,ambayo inatengeneza vitu vya tekinolojia kubwa,kama 5G,USA,hapa lazima ashikwe na hola, vita itakuwepo,

Sie tuna bidhaa gani ya pekee ambayo ni kutoka Tanzania pekee yake mpaka majirani waanzishe vita ya uchumi?
 
Mambo ya kiuchumi kwa nchi majilani ni sawa na wewe unavyoishi na jilani zako hapo mtaani kwako.

Wewe kama unaishi vibaya na jilan zako na jilani zako watakutenga kwa kukuogopa au kukukomoa.

Ukisema wanakuogopa hapa kuna mambo mengi kwamba mtu huyu akija kwako kukuomba chochote cha ushirikiano majilani wanasema mtu huyo hata ukishirikiana nae lakini mwisho wake sio mzuri.

Mwisho watafikia kiwango wataambizana,msiende kuomba au.kuazima hata kununua chochote kwa huyo jilani.
Maana ni mkolofi,hana kauli nzuri na majilan /wateja lakin hata biashars yake hainaviwango.

HIVYO ILI UFANIKIWE KIBIASHARA NA KIUCHUMI KWA DUNIA YA SASA NI LAZIMA UWE NA KAULI NZURI NA WADAU WAKO KUANZIA KWA MAJILANI NA MAJILANI HATA AKIJA MGENI KUTOKA MBALI WATAMWAMBIA KUYOKANA NA HITAJI LAKO NENDA KWA JILANI ANGU ATAKUSAIDIA.

LAKINI UKIWA NA KAULI MBAYA INAMFANYA JILANI HATA AKIJA MGENI ATAMWAMBIA USIENDE KWA HUYO MTU MAANA HANA KAULI NZURI HATA NA SISI.JILANI ZAKE.
 
Elimu pia inahitajika sana kwa watanzania.

We chukua mfano.

Wakati EAC inaanzishwa Kenya, Uganda na Tanzania.

Kipindi kile kenya na uganda zilikua vizur kiuchumi ukilinganisha na Tanzania yetu.

Wakaa wakaweka mkkakati kua Tanzania ikipeleka bidhaa zake kenya au.uganda inatozwa kodi kidogo kuliko kenya ikileta bidhaa zake Tanzania.

Lakini mpaka sasa naona bado hata watanzania wenyewe hawaijui.EAC. matokeo yake hata baadhi ya viongozi hawajui au wanasahau vile vipengele vya kwenye EAC wanakulupuka na wanajikuta ndio wanajihalibia kabisa.

Mkenya leo anakuja kuomba kazi tanzania watanzania wanamlaumu lakini wanasahau kuna kipengele cha Rasilimali watu.

Mkenya leo analeta vifaranya au biashara inahalibiwa bila ya sababu za msingi wanasahau kua kuna uhuru wa EAC wa masoko kati ya nchi wanachama.

WATANZANIA KIUKWELI TUNATAKIWA KUELIMISHWA SANA KUHUSU HAYA MAMBO YA MUUNGANO KAMA VILE EAC,SADIC,CENTRAL COLIDO NK.

Lasivyo miaka nenda rudi tunakua wajinga na tutapigwa bao sana.

Leo hii heti.kuna karot,viazi, hadi mchicha unatoka kenya badala ya tanzania kuwapa elimu watu wake kuhusu EAC kua kuna uhuru wa masoko kwenye nchi hizo matokeo yake wanaenda kuvuruga biashara za majilani.

WATANZANIA TUPO NYUMA SANA KWASABABU HATUNA ELIMU .

KAMA MTANZANIA ANASOMA KUANZIA CHEKECHEA HADI FORM6 HAJUI ALICHOKISOMA NA HANA FANI YOYOTE.
MTU WA FORM 6 WA TANZANIA HAFAI KUPEWA KAZIYOYOTE ,ANASHINDWA NA DARASA.LA 7.ALIEENDA VETA.
UNAONA KABISA NI UJINGA.

TUSIPOREKEBISHA MIFUMO YETU YA ELIMU WATANZANIA TUSAHAU HATA KUSHINDANA NA RWANDA TU.
 
Elimu pia inahitajika sana kwa watanzania.

We chukua mfano.
Wakati EAC inaanzishwa kenya,uganda na tanzania.
Kipindi kile kenya na uganda zilikua vizur kiuchumi ukilinganisha na Tanzania yetu...
Kaa chini utulie na upitie stages za economic integration. Naona unakurupuka.
 
Hii dhana ya vita vya kiuchumi inachanganya sana. Maana ikiangaliwa kwa upande mmoja watu wengi hudhania kuwa vita hivi huwa vinapiganwa baina ya taifa maskini lenye rasilimali zake dhidi ya mataifa matajiri yenye nia ya kunyonya rasilimali zake...
Hapa hakuna cha mabeberu,wala nchi jirani,tunashindwa wenyewe kuinua uchumi wetu Mimi naandika kitabu cha ujasiriamali ,tunafundishwa kwamba asilimia 80% ya mafanikio kwenye biashara yoyote ile yanategemea 'personal quality' yaani jinsi unavyo enenda kwenye biashara lakini kihalisia asilimia 20% ina nguvu zaidi kukwamisha biashara, husababishwa na 'political,physical and environmental factors',yaani siasa,afya na yanayo mzunguka mfanya biashara. Yanayomzunguka mfanyabiasha huanzia ngazi ya familia hadi kimataifa (The entrepreneur and his environments) , somo ni refu kidogo cha ziada nikwamba serikali nyingi hupoteza pesa nyingi na muda mwingi kutengeneza sheria na kanuni za namna ya kuendesha biashara lakini cha ajabu biashara hizo huwa hazifanikiwi sababu kuu ni mbili 1.wanao tunga hizo sheria na kanuni hawana elimu ya ujasiriamali 2.wafanyanyabiashara huwa hawashirikishwi
 
Hapa hakuna cha mabeberu tunashindwa wenyewe kuinua uchumi wetu Mimi naandika kitabu cha ujasiriamali ,tunafundishwa kwamba asilimia 80% ya mafanikio yanategemea 'personal quality' yaani jinsi unavyo enenda kwenye biashara lakini kihalisia asilimia 20% INA nguvu zaidi ambayo husababishwa na 'political,physical and environmental factors',yaani siasa,afya na yanayo mzunguka mfanya biashara kuanzia ngazi ya familia hadi kimataifa ni somo refu kidogo
Umeilewa mada husika?
 
Back
Top Bottom