Vita vya Syria: Wanajeshi wa Uturuki 33 wauawa katika mashambulio Idlib. Uturuki yatuma Maelfu ya Wanajeshi Syria

Sela Son

JF-Expert Member
Dec 31, 2018
2,620
6,079
Takriban askari 33 wa Uturuki wameuawa katika mashambulio ya anga ya "vikosi vya Syria" Kaskazini-Magharibi mwa Syria, amesema afisa wa ngazi ya juu wa Uturuki.

Wengi waliumizwa katika jimbo la Idlib, amesema Rahmi Dogan, Gavana wa jimbo la Uturuki la Hatay. Taarifa nyingine zinasema idadi ya vifo ni ya juu zaidi.

Uturuki kwa sasa inajibu kwa kuyalenga kushambulia dhidi ya maeneo ya vikosi vya Syria.

Vikosi vya Syria vinavyoungwa mkono na Urusi vinajaribu kurejesha jimbo la Idlib ambalo kwa sasa linadhibitiwa na waasi wanaosaidiwa na wanajeshi wa Uturuki

Maafisa nchini Syria bado hawajatoa kauli yao wazi kuhusu mapigano ya sasa ya Idlib, ambalo ni jimbo la mwisho lililosalia mikononi mwa upinzani.

Jeshi la Uturuki lilianza kupiga maeneo ya Syria baada ya Rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan kufanya mkutano na maafisa wa ngazi ya juu wa usalama mjini Ankara.

Kiongozi wa Uturuki anataka vikosi vya Syria virudi nyuma kutoka kwenye maeneo ambayo Uturuki imeweka vituo vya uchunguzi na awali ilitishia kuvishambulia kama haitaacha mashambulio yake.

Lakini serikali ya Syria na Urusi zimekataa madai yake ya kurudi nyuma kwenye mistari ya usitishaji mapigano iliyokubaliwa mwaka 2018. Urusi pia imeishutumu Uturuki kwa kukiuka makubaliano ya mwaka 2018 ya usitishaji mapigano kwa kuwaunga mkono waasi kwa kufyatua makombora.

Waangalizi wa haki za binadamu nchini Syria wenye makao yao makuu nchini Uingereza,The UK-based monitor, the Syrian Observatory for Human Rights, wamesema kuwa wanajeshi 34 wa Uturuki waliuawa Alhamisi katika mashambulio ya anga jana jioni.

Waliojeruhiwa wamerudishwa nchini Uturuki kwa ajili ya matibabu, amesema Bw. Dogan.

"Yote yanajulikana"maeneo ya serikali ya Syria yalishambuliwa na ndege za Uturuki na vikosi vya ardhini, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Uturuki Fahrettin alinukuliwa na Shirika la habari la taifa Anadolu akisema. Uturuki ilikua imeamua ku "jibu kwa ukarimu" mashambulio, alisema Bw, Altun.

Wakati huo huo ,Uturuki ambaye ni mjumbe wa Muungano wa kujihami wa nchi za Magharibi Nato imesema waziri wake wa mambo ya nje Mevlut Cavusoglu amezungumza na katibu mkuu wa muungano wa Nato -Generali Jens Stoltenberg.

Uwanja sasa umewekwa tayari kwa ajili ya makabiliano kamili baina ya Uturuki na Syria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aknowledge source ya taarifa yako mkuu,,utashtakiwa kucopy na kupaste ni criminal offence,inaitwa pragirism
Ah sawa sawa. Unaweza kufuatilia hili kupitia shirika la habari la serikali la Uturuki Anadolu na pia Sputnik ( Russia) Al masdar ( Lebanon)
Hii huwezi Iona BBC Wala CNN coz ni habari isiyopendeza miongoni mwa wamagharibi japo hawaipendi Turkey

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uturuki imejiweka pabaya mno hapo Idlib ila serikali ya Erdogan pia inatakiwa ijilaumu yenyewe kwa kushindwa kutekeleza makubaliano ya Astana kati yake,Urusi na Iran kwa kushindwa kuyavunja makundi ya kigaidi (HTS) kama walivyoahidi.
 
Erdogan is Arrogant..
Hivi anafikiri Turkey ni US au Russia kwamba watu watamuogopa ...analetea matatizo yasiyo ya lazima wanajeshi wake na familia zao...
Alitoa mpaka mwisho wa mwezi huu...baada ya hapo ataanza kuwashambulia Syria kuwasukuma nje ya observation points zao..cha ajabu siku moja kabla ya deadline kuisha....watu wanamtandika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si amekataa kuondoka sirya kwa hiyari sasa ataondoka kwa razima atake asitake kilicho mpeleka ninini?
Kuanzia Leo ndio mtambue Iran ni wanaume maana hizo ligi ndio zake na hajawahi kushidwa kwenye ligi yeyote.
Kujiingiza kwenye ligi ya mashariki ya kati ina hitaji akili kubwa sana na sio eti ukiwa na pesa au uchumi Mkubwa.
Hivi Edorgan anadham Israel ni wapumbavu sana kutoingiza majeshi yake nchini sirya japo wanaomba usiku na mchana asadi aanguke.
 
Si amekataa kuondoka sirya kwa hiyari sasa ataondoka kwa razima atake asitake kilicho mpeleka ninini?
Kuanzia Leo ndio mtambue Iran ni wanaume maana hizo ligi ndio zake na hajawahi kushidwa kwenye ligi yeyote.
Kujiingiza kwenye ligi ya mashariki ya kati ina hitaji akili kubwa sana na sio eti ukiwa na pesa au uchumi Mkubwa.
Hivi Edorgan anadham Israel ni wapumbavu sana kutoingiza majeshi yake nchini sirya japo wanaomba usiku na mchana asadi aanguke.
Good.. nimepata somo hapa kumbe middle east kujiingiza haitaki tu uchumi mkubwa Bali akili kubwa! Safi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Erdogan is Arrogant..
Hivi anafikiri Turkey ni US au Russia kwamba watu watamuogopa ...analetea matatizo yasiyo ya lazima wanajeshi wake na familia zao...
Alitoa mpaka mwisho wa mwezi huu...baada ya hapo ataanza kuwashambulia Syria kuwasukuma nje ya observation points zao..cha ajabu siku moja kabla ya deadline kuisha....watu wanamtandika

Sent using Jamii Forums mobile app
Tofauti na Israel., Turkey militarily hayuko vyema .. kitendo tu Cha kulundikana kwenye maghorofa wakati mko vitani nao ni upumbavu wa kiwango Cha juu.. Sasa wanagongwa mbaya.. inavyoonekana Syria huwaogopa Sana Israel kuliko yeyote middle east.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamii forums mnazingua Sana.. alowaambia muedit huu Uzi Nani? Yaani mmeedit kote halafu bado jina ni langu.. upumbavu huo..
Kwanini msiandike wenyewe toka usiku was Jana Kama siyo u. Fa, la.
Futeni jina langu fa ,, la..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom