Vita na uganda (idi amini dada)

Kiherehere

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
1,806
621
Wana Jamii

Kwa uelewa wangu, na ufuatiliaji, NACHELEA KUSEMA KUWA vita na Uganda, Tanzania ilikuwa haina UWEZO wa kuishinda Uganda kama tunavyosema.

Kama Watanzania tunavyodai kuwa Jeshi letu linaouwezo mimi sina hakika kwa hayo.
Kilichofanya Tanzania Ishinde ni mambo yafuatayo na si vinginevyo:-

1.Uganda iliyosambaratika kutokana na Mapibduzi aliyoyafanya Amini kwa mtangulizi wake ilipelekea kuwa na mgawanyiko.

2.Rebel groups za waganda wenyewe, ambazo ziliisaidia Tanzania kumuondoa Amini (Yowel Museven) ambao walikuwa wanaijua uganda vizuri.

3.Mgawanyiko ulioletwa na baadhi ya wahamiaji waliotimuliwa na Amini.
Haya yote na mengineyo ndio yaliyopelekea Ushindi wa Tanzania, Uganda na sio vinginevyo, kama watanzania wanavyodai kuwa JESHI LETU LIKO FIT.

Tulipigana na adiu ambaye alikuwa amejeruhiwa na mambo kama hayo, so ilikuwa ni rahisi kushinda kuliko tungeikuta Uganda iliyo na mshikamano kama ilivyokuwa Tanzania.

Ni mtazamo na mawazo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom