Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Kuna baadhi ya kauli za viongozi wetu huwa zinatia wasiwasi kama kweli wana nia ya dhati ya kupambana na uovu ukiwemo ufisadi! Kauli ya Ole Sendeka kwamba atamharibia Rais Kikwete kwa kuanika maovu ya Serikali endapo hataacha kuwafuatilia wabunge kwa tuhuma za kulipwa posho mara mbili kwa kazi moja! Kauli nyingine ni ya Dkt Mwakyembe alipoitoa mara baada ya kutoa Ripoti ya Richmond kwa wale ambao walikuwa wanachokonoa kiaina mambo ya Richmond kwamba Kamati yake ingetoa hata yale ambayo hawayakusema kwa kuwa waliogopa kuiumbua Serikali! Sakata linaloendelea sasa hivi la posho mbili kwa kazi moja nako limekuwa na timing kali sana mpaka limeleta mkanganyiko mkubwa! Kauli nyingine ni ya Mh Zitto Kabwe aliyoitoa humu kwamba anawajua waheshimiwa wabunge wanaofoji tiketi za mabasi! Sina hakika kama Mh Zitto na yeye kama ameweka silaha kibindoni ili na yeye akilipuliwa amlipue mtu au amefikisha taarifa hiyo kwenye vyombo vinavyohusika! Observation yangu nyingine ni kuhusu Kesi ya Zombe ambaye alidai kwamba ETI amegundua kwamba Jeshi la Polisi linabambikizia watu kesi! Iweje huyu bwana Zombe "agundue" ubambikiziaji huo baada ya yeye kuwa na kesi huku akijua kwamba malalamiko ya ubambikiziaji kesi ni ya siku nyingi? Baada ya kutoa hayo machache nionavyo mimi upambanaji dhidi ya maovu kwa TZ utachukua muda mrefu kwa sababu "wapambanaji" wanapambana ili kujijenga wao binafsi zaidi kuliko kupambana na uovu kama ulivyo! The theory behind: "mwaga mboga nimwage ugali!" Huu ndio ukweli, kwa hali ilivyo sasa! Rais mwenyewe ana orodha ya wabwia/wauzaji wa madawa ya kulevya, anasubiri wakimchokonoa pabaya ana-single out (anam-shortlist, if you like) jina la mbaya wake na kumzima kiulaini! Hii ni TZ bwana, acha mchezo!