Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Nimekuwa nikistajabishwa na hili tangazo la kwenye luninga ambalo lina waonyesha katuni wakizungumzia jinsi ya kujikinga na Malaria kwa kutumia chandarua chenye dawa.Kinachonishangaza ni kuwa tangazo hili liko kwa lugha ya kingereza wakati tunatambua kabisa kwamba zaidi ya asilimia 60 ya watanzania hawafahamu lugha hii.Na kimsingi wasiofahamu lugha hii ndio wale wasiofahamu jinsi ya kujikinga na Malaria,nikiassume kwamba hawajaenda shule hivyo hawafahamu kabisa jinsi ya kujikinga na Malaria.Hivi hili tangazo limemlenga nani hasa?Kwa mwendo huu hii vita ya Malaria itaisha kweli?na je rasilimali katika vita hii zinatumika ipasavyo?