Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,157
Nami naomba nitie neno katika vita dhidi ya kutokomeza dawa za kulevya
Ki uhalisia hakuna mtu mwenye mapenzi mema na jamii inayomzunguka anayeweza kukubaliana na uuzaji wa dawa hizi hatari
DSM ndio kitovu cha nchi hii kiasi kwamba kwa asilimia kubwa kila kitu, kiwe kizuri au kibaya kinaanzia dsm ndio maana sishangai moto wa vita hii kukolezwa kuanzia dsm na leo tunaona mikoa mingine inafuata japo kwa namna tofauti.
Kinachonishangaza mimi kama uncle Jei Jei, ni kitendo cha kuwapa watu umaarufu katika vitu haramu hivyo vita nzima kugeuka kichekesho na kuonekana kuwa watu wazima wanafanya masikhara katika mambo ya hatari
Tangu wiki iliyopita vyombo vingi vya habari vinamtaja Makonda, tukisema lengo lake lilikuwa kujiongezea umaarufu tutakuwa tumekosea!?
Ni kweli kuwa hajui kama hana mamlaka ya kuwataja watu hadharani bila vidhibiti!?
Ni kweli kuwa hajui kama hana mamlaka ya kumuita mtu polisi!?
Sasa tukisema alikuwa anatafuta kuendelea kutajwa na vyombo vya habari kwa sababu siku chache nyuma hadi watu walimmisi!?
Leo hadi Gwajima naye aliyekuwa kimya kwa muda kaibuka, Manji ambaye huenda watu walikuwa hawamsemi semi naye kajaa midomoni mwa watu, huku sio kutafuta umaarufu kweli!?
Leo kina TID hawaishi kumtembelea na kumtaja brother Makonda, hatuoni kweli kwamba alihisi umaarufu unashuka!?
Wasaidizi wake wa karibu ni wakuu wa wilaya, cha ajabu katika vita hii hatuwaoni luningani!!
Vita ya muhimu kama hii hutakiwi kuingiza mzaha kama wa brother Makonda!?!... Eti Rose wa Tabata, Uledi wa Mwananyamala, Makomeo,... Kweli Tabata nzima Kuna Rose mmoja tu!?
Huu ni mzaha na katika mzaha huu wenyewe wenye madawa yao wanaicheka nchi kwa kukubali kuchezeshwa shele na huyu kijana!! Yangu ni hayo!!
Ki uhalisia hakuna mtu mwenye mapenzi mema na jamii inayomzunguka anayeweza kukubaliana na uuzaji wa dawa hizi hatari
DSM ndio kitovu cha nchi hii kiasi kwamba kwa asilimia kubwa kila kitu, kiwe kizuri au kibaya kinaanzia dsm ndio maana sishangai moto wa vita hii kukolezwa kuanzia dsm na leo tunaona mikoa mingine inafuata japo kwa namna tofauti.
Kinachonishangaza mimi kama uncle Jei Jei, ni kitendo cha kuwapa watu umaarufu katika vitu haramu hivyo vita nzima kugeuka kichekesho na kuonekana kuwa watu wazima wanafanya masikhara katika mambo ya hatari
Tangu wiki iliyopita vyombo vingi vya habari vinamtaja Makonda, tukisema lengo lake lilikuwa kujiongezea umaarufu tutakuwa tumekosea!?
Ni kweli kuwa hajui kama hana mamlaka ya kuwataja watu hadharani bila vidhibiti!?
Ni kweli kuwa hajui kama hana mamlaka ya kumuita mtu polisi!?
Sasa tukisema alikuwa anatafuta kuendelea kutajwa na vyombo vya habari kwa sababu siku chache nyuma hadi watu walimmisi!?
Leo hadi Gwajima naye aliyekuwa kimya kwa muda kaibuka, Manji ambaye huenda watu walikuwa hawamsemi semi naye kajaa midomoni mwa watu, huku sio kutafuta umaarufu kweli!?
Leo kina TID hawaishi kumtembelea na kumtaja brother Makonda, hatuoni kweli kwamba alihisi umaarufu unashuka!?
Wasaidizi wake wa karibu ni wakuu wa wilaya, cha ajabu katika vita hii hatuwaoni luningani!!
Vita ya muhimu kama hii hutakiwi kuingiza mzaha kama wa brother Makonda!?!... Eti Rose wa Tabata, Uledi wa Mwananyamala, Makomeo,... Kweli Tabata nzima Kuna Rose mmoja tu!?
Huu ni mzaha na katika mzaha huu wenyewe wenye madawa yao wanaicheka nchi kwa kukubali kuchezeshwa shele na huyu kijana!! Yangu ni hayo!!