Vita dhidi ya Corona:Serikali ipeleke msuwaada Bungeni kwa hati ya dharura utakaotaka kila sehemu watu wanakoingia kupata huduma kuwe na sanitizer

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Katika kupambana na corona,naishauri serikali kupeleka muswaada Bungeni katika Bunge linaloendelea kwa hati ya dharura,muswaada ambao ukiwa sheria, utataka kila sehemu(jengo la kibiashara,duka,n,k) ambapo watu huingia kupata huduma ni lazima kuwe na sanitizer au ndoo ya maji na sababuni na pia sheria itamke ni kosa kwa mtu kutonawa mikono na kuwe na adhabu ya faini kwa atakebainika kupuuza sheria hiyo.

Nashauri hivi kwasababu kuna sehemu hakuna huduma za watu kunawa miklono licha ya sehemu hizo kupokea watu wengi kwa wakati mmoja, na pia kuna madai(taarifa) kuwa baadhi ya watu wanakaidi kunawa mikono wanapotakiwa kufanya hivyo.

Kwenye masoko.japo ni vigumu sana,nashauri Halmashauri husika zichukue jukumu la kusambaza ndoo za maji na sabani katika njia zote za kuingilia na kutokea sokoni na mgambo wa Halmashauri wapewe jukumu la kusimamia watu kunawa mikono.

Kama tutaona gharama ya fedha ni muhimu kuliko afya zetu,ipo siku tutajua bila afya, hata hizo fedha hazina maana unless Mungu mwenyewe atatunusuru na hili janga.

Kama kila hatua itatushinda au tutaiona ni ngumu,basi tujiandae kushindwa na corona na kutengwa na mataifa mengine siku za baadae unless gonjwa hili hapa Bongo litatoweka kwa maombi kama tulivyoambiwa.
 
Katika kupambana na corona,naishauri serikali kupeleka muswaada Bungeni katika Bunge linaloendelea kwa hati ya dharura,muswaada ambao ukiwa sheria, utataka kila sehemu(jengo la kibiashara,duka,n,k) ambapo watu huingia kupata huduma ni lazima kuwe na sanitizer au ndoo ya maji na sababuni na pia sheria itamke ni kosa kwa mtu kutonawa mikono na kuwe na adhabu ya faini kwa atakebainika kupuuza sheria hiyo.

Nashauri hivi kwasababu kuna sehemu hakuna huduma za watu kunawa miklono licha ya sehemu hizo kupokea watu wengi kwa wakati mmoja, na pia kuna madai(taarifa) kuwa baadhi ya watu wanakaidi kunawa mikono wanapotakiwa kufanya hivyo.

Kwenye masoko.japo ni vigumu sana,nashauri Halmashauri husika zichukue jukumu la kusambaza ndoo za maji na sabani katika njia zote za kuingilia na kutokea sokoni na mgambo wa Halmashauri wapewe jukumu la kusimamia watu kunawa mikono.

Kama tutaona gharama ya fedha ni muhimu kuliko afya zetu,ipo siku tutajua bila afya, hata hizo fedha hazina maana unless Mungu mwenyewe atatunusuru na hili janga.

Kama kila hatua itatushinda au tutaiona ni ngumu,basi tujiandae kushindwa na corona na kutengwa na mataifa mengine siku za baadae unless gonjwa hili hapa Bongo litatoweka kwa maombi kama tulivyoambiwa.
Huu ugonjwa kwa kiasi kikubwa unaenezwa kwa njia ya kuvuta hewa yenye virus kutoka kwa mtu mwenye maambukizo anapokohoa au kupiga chafya au kuongea na matone ya mate yakamtoka. Hata unawe mikono na mafuta ya moto bila kupunguza misongamano ni bure. Kwanza wakiweka vitu kama hivyo vitaleta kujiamini kusikotakiwa. Mtu akishanawa mikono atafikiri ndiyo amemaliza kila kitu. Inatakiwa waanze na kupunguza mikusanyiko na misongano ya watu kadiri iwezekenavyo.
 
Huu ugonjwa kwa kiasi kikubwa unaenezwa kwa njia ya kuvuta hewa yenye virus kutoka kwa mtu mwenye maambukizo anapokohoa au kupiga chafya au kuongea na matone ya mate yakamtoka. Hata unawe mikono na mafuta ya moto bila kupunguza misongamano ni bure. Kwanza wakiweka vitu kama hivyo vitaleta kujiamini kusikotakiwa. Mtu akishanawa mikono atafikiri ndiyo amemaliza kila kitu. Inatakiwa waanze na kupunguza mikusanyiko na misongano ya watu kadiri iwezekenavyo.
Tatizo uvaaji wa mask umekuwa discouraged hapa Bongo na hata udhibiti wa mikusanyiko nao umetushinda labda mpaka hali iwe tete ndio tutalazimika kuchukua maamuzi magumu.
 
Hapana, kwa nini iwe sheria...

Kinachotakiwa ni usimamizi madhubuti basi...

Ikiwezekana tucharazane viboko tunapokaidi au kuhatarisha afya zetu na za watu wengine...



Cc: mahondaw
Ni sahihi usemacho,ila watu wakisikia kuna sheria kwanza wataona hili ni jambo muhimu na pia wataogopa.
 
Ni sahihi usemacho,ila watu wakisikia kuna sheria kwanza wataona hili ni jambo muhimu na pia wataogopa.

Sheria its a long term plan...

Covid19 its not here to stay... It will eventually pass...

Ikitungiwa sheria kama ilivyoanishwa hapo, tutakuja kusumbuana huko mbeleni wakakti ikiwa haipo tena...



Cc: mahondaw
 
Hivi kwanini mnakuza mambo aya..Rais amesema tutishane ila tufanya kazi..sasa disko,baa,usafiri,makanisani,miskitini,kwenye masoko na magulio .TUACHE KUTISHANA ..TUCHAPE KAZI
 
Sheria its a long term plan...

Covid19 its not here to stay... It will eventually pass...

Ikitungiwa sheria kama ilivyoanishwa hapo, tutakuja kusumbuana huko mbeleni wakakti ikiwa haipo tena...



Cc: mahondaw
Kuna mazingira hulazimisha uwepo wa sheria fulani hivyo sio ajabu na sheria hio inaweza kuja kutumika hata huko mbeleni iwapo janga kama hili litajirudia au likatokea lingine la kufanana na hili.

Kumbuka ziko sheria nyingi tu ambazo hazitumikia ila ziliwahi tungwa miaka mingi tu.
 
Kukiwekwa hao migambo utakuja kufungua uzi mwingine hapa kuwa migambo imetumwa na ikulu iwanyanyase!
 
Back
Top Bottom