#COVID19 Vita dhidi ya Corona: Rais Magufuli anaanza Marais wengine wanafuata

Abdalah Abdulrahman

JF-Expert Member
Aug 29, 2019
222
201
Sifa ya kiongozi ni kuweza kufikiri nje ya boxi, kwa maana ya kuwa na IQ kubwa katika kutatua changamoto za kila siku za wale unaowaongoza. Rais wa Tanzania amekua akilionesha hili wazi kupitia mapambano yake na rushwa, wafanyakazi hewa, matumizi mazuri ya pesa za umma, usimamizi mzuri wa watendaji na maamuzi mazuri katika kuendea mambo.

Janga la Corona limetoa taswira ya kipekee kwa uongozi wa Rais John Magufuli. Mfano wa kwanza ni ule wa vifaa feki vya kutoa majibu ya corona ambapo aliweka wazi kwa dunia kuwa kama vifaa hivi havitoi majibu sahihi ya vipimo kwa kupeleka sampuli ya papai, na vitu vingine ambavyo vilionekana vina corona.

Mafano wa pili ni wa hivi karibuni alipotoa angalizo kuwepo kwa barakoa feki na ambazo ndizo sababu za maambukizi ya corona. Angalizo hili sasa hivi linatolewa na nchi nyingi duniani.

Asante Dr Magufuli
 
Sometime ujue kuna wazee humu jukwaani, siyo kuandika mada na kuiweka hapa.

Eti 'Marais wengine' ni marais gani hao ambao hawana majina wala nchi zao?
 
Umenikumbusha mzazi wangu huwa anawaita watu kama wewe kichwa box.
 
Mafano wa pili ni wa hivi karibuni alipotoa angalizo kuwepo kwa barakoa feki na ambazo ndizo sababu za maambukizi ya corona. Angalizo hili sasa hivi linatolewa na nchi nyingi duniani.

Asante Dr Magufuli
Barakoa ndio zinasababisha maambukizi ya Corona ?

Kweli ni ajabu raia mwenyewe ambaye inabidi afya yake ilindwe na taasisi ambazo anazilipia kodi..., kufurahia hizi sarakasi...., Kumbuka unless otherwise na wewe una link ya mitungi ya gesi ya kutosha nyumbani yakikukuta ya kukukuta utaondoka kivyako...
 
Barakoa ndio zinasababisha maambukizi ya Corona?

Kweli ni ajabu raia mwenyewe ambaye inabidi afya yake ilindwe na taasisi ambazo anazilipia kodi, kufurahia hizi sarakasi, Kumbuka unless otherwise na wewe una link ya mitungi ya gesi ya kutosha nyumbani yakikukuta ya kukukuta utaondoka kivyako.
Ndio inaweza kusababisha kwasababu hiyo ni biashara. Medical industry inaweza kufanya huo mchezo. Hivi kwa mfano kikatokea kiwanda na kuchukua barakoa zinazotumika mahospitalini na kuzi recycle kisha kuwauzia watu wa mataifa ya nje vipi hapo.
 
ndio inaweza kusababisha kwasababu hiyo ni biashara. Medical industry inaweza kufanya huo mchezo. Hivi kwa mfano kikatokea kiwanda na kuchukua barakoa zinazotumika mahospitalini na kuzi recycle kisha kuwauzia watu wa mataifa ya nje vipi hapo.
Kwahio tumetoka kwenye inasababisha na kuingia kwenye inaweza kusababisha. Kwahio kutoka kwenye uhakika tunaingia kwenye assumptions, na kuleta mifano ya kinadharia?

Kampuni ipo liable, kosa kama hilo kwa kampuni yoyote ikigundulika ni kufilisiwa na malipo ni ya hali ya juu (is the risk worthwhile)?

Na kama kampuni fulani imegundulika imefanya hivyo ni kipi kimefanyika ili kuiwajibisha hio kampuni na ikibidi watu waliokufa walipwe fidia (am sure hio kampuni ina assests za kutosha)

Nadharia na inawezekana na shutuma sio za kutolewa bila kuwa na concrete proof.
 
Mwisho wa huu mchezo unaochezwa na mabeberu mtakuja kuugundua baada ya miaka 10 ijayo.Kwa sasa hivi mnaweza msielewe kutokana na ukomo wa kufikiria.
 
1614586634215.png
 
Mwisho wa huu mchezo unaochezwa na mabeberu mtakuja kuugundua baada ya miaka 10 ijayo.Kwa sasa hivi mnaweza msielewe kutokana na ukomo wa kufikiria.
Wewe una kichwa kama cha kuku. Wafanye hayo kwa faida ya nani wakati hili janga limepiga hodi dunia mzima?! Ulivyo na kichwa cha mtetea umeshasahau ni JPM huyo huyo na serikali yake walikuwa wanasema ni kagonjwa kadogo tu na katatoka kwa maombi wakati viongozi wanaotumia kichwa duniani wakaona huo ni ujinga! Sasa hao duniani waliofuata wendawazimu wenu ni akina nani?! Kuna taifa linalopiga nyungu kama taifa lenye majuha aina yako?! Mbona mnahamasisha barakoa kama wengine wakati mlisema ni kagonjwa kadogo?! Sasa ni nani hapo anayefuata kinachofanywa na mwenzake kama sio nyie wenyewe? Hivi hata yule kichaa aliye wizara ya afya hivi sasa anahubiri ule upuuzi mliokuwa mnaoshangilia?
 
Sifa ya kiongozi ni kuweza kufikiri nje ya boxi, kwa maana ya kuwa na IQ kubwa katika kutatua changamoto za kila siku za wale unaowaongoza. Rais wa Tanzania amekua akilionesha hili wazi kupitia mapambano yake na rushwa, wafanyakazi hewa, matumizi mazuri ya pesa za umma, usimamizi mzuri wa watendaji na maamuzi mazuri katika kuendea mambo.

Janga la Corona limetoa taswira ya kipekee kwa uongozi wa Rais John Magufuli. Mfano wa kwanza ni ule wa vifaa feki vya kutoa majibu ya corona ambapo aliweka wazi kwa dunia kuwa kama vifaa hivi havitoi majibu sahihi ya vipimo kwa kupeleka sampuli ya papai, na vitu vingine ambavyo vilionekana vina corona.

Mafano wa pili ni wa hivi karibuni alipotoa angalizo kuwepo kwa barakoa feki na ambazo ndizo sababu za maambukizi ya corona. Angalizo hili sasa hivi linatolewa na nchi nyingi duniani.

Asante Dr Magufuli
Sio wote katikati ya masikio yao hamna kitu ka huyo wako
 
Back
Top Bottom