Katika pita pita yangu nikitafakari kwa kina kuna nini hasa kiasi yaliyo dhahiri yanafanywa uchuro na yaliyo uchuro kuhusu ugonjwa huu yanafanywa amali, nimegundua yafuatayo:
1. Makundi mengi ya wafanya biashara (yana gundu) yamebambikiwa viwango vikubwa zaidi vya kodi visivyoendana na biashara zao kwa mwaka huu wa 2020. Kwamba katika maeneo yote ya biashara, kwa mwaka huu kodi za mapato ya biashara zote zimepandishwa sana.
2. Kama alivyomweleza jiwe, king msukuma kwenye ule mkutano wa wafanya biashara kuhusiana na makadirio tata ya biashara, bambikizi hizi za kodi zimekamilika leo 31 March 2020.
Katika kipindi chote cha makadirio ya kodi, TRA kama kawaida yao wamefanya mavuno kweli kweli kupitia rushwa katika kipindi chote kilicho kamilika leo. Na wameneemeka kweli kweli.
3. Kodi zimepandishwa bila kujali mdororo wowote wa biashara ulioletwa na Corona, wala bila kujali mdororo huo utaendelea hadi lini. Hii ni kwa Tanzania tu ambako walipa kodi wake hufikiriwa kuwa "immune" kwa mazahama yoyote hata yawezekana mazito mazito ya kidunia kama corona.
Kwingine kote serikali zimekuja na stimulus packages za aina mbalimbali kusaidia biashara zao zisife ili pia ziendelee kutoa ajira.
Tanzania ng'ombe hukamuliwa hadi atoe damu au afe kabisa.
Kwa mwonekano wa hali ilivyo na hii pandisha pandisha ya kodi, kwa hakika serikali ya Tanzania haijaathirika kwa vyovyote kimapato na Corona bali imechukua wasaa huo kikamilifu kujinufaisha kweli kweli.
Ni aibu kubwa kuwa kuna institution yoyote kuwa ati kwa namna yoyote iko kwenye kunufaika kwa namna yoyote katika kipindi hiki cha ugonjwa huu.
Kwa hakika, kwa hali ilivyo mtaani, ni wazi kuwa pana ukakasi wa kutosha baina ya wafanya biashara na serikali. Kinyume na sehemu zingine ambako wafanya biashara na serikali wameshikana mikono kuona jamii zao zinavuka athari zinazoletwa na ugonjwa huu kwa salama kadri inavyowezekana.
Yale yale ya matetemeko ya Kagera.
Ama kweli jasiri haachi asili.
1. Makundi mengi ya wafanya biashara (yana gundu) yamebambikiwa viwango vikubwa zaidi vya kodi visivyoendana na biashara zao kwa mwaka huu wa 2020. Kwamba katika maeneo yote ya biashara, kwa mwaka huu kodi za mapato ya biashara zote zimepandishwa sana.
2. Kama alivyomweleza jiwe, king msukuma kwenye ule mkutano wa wafanya biashara kuhusiana na makadirio tata ya biashara, bambikizi hizi za kodi zimekamilika leo 31 March 2020.
Katika kipindi chote cha makadirio ya kodi, TRA kama kawaida yao wamefanya mavuno kweli kweli kupitia rushwa katika kipindi chote kilicho kamilika leo. Na wameneemeka kweli kweli.
3. Kodi zimepandishwa bila kujali mdororo wowote wa biashara ulioletwa na Corona, wala bila kujali mdororo huo utaendelea hadi lini. Hii ni kwa Tanzania tu ambako walipa kodi wake hufikiriwa kuwa "immune" kwa mazahama yoyote hata yawezekana mazito mazito ya kidunia kama corona.
Kwingine kote serikali zimekuja na stimulus packages za aina mbalimbali kusaidia biashara zao zisife ili pia ziendelee kutoa ajira.
Tanzania ng'ombe hukamuliwa hadi atoe damu au afe kabisa.
Kwa mwonekano wa hali ilivyo na hii pandisha pandisha ya kodi, kwa hakika serikali ya Tanzania haijaathirika kwa vyovyote kimapato na Corona bali imechukua wasaa huo kikamilifu kujinufaisha kweli kweli.
Ni aibu kubwa kuwa kuna institution yoyote kuwa ati kwa namna yoyote iko kwenye kunufaika kwa namna yoyote katika kipindi hiki cha ugonjwa huu.
Kwa hakika, kwa hali ilivyo mtaani, ni wazi kuwa pana ukakasi wa kutosha baina ya wafanya biashara na serikali. Kinyume na sehemu zingine ambako wafanya biashara na serikali wameshikana mikono kuona jamii zao zinavuka athari zinazoletwa na ugonjwa huu kwa salama kadri inavyowezekana.
Yale yale ya matetemeko ya Kagera.
Ama kweli jasiri haachi asili.