Visa nilivyoshuhudia kwa ndugu yangu Mtaalam wa Tiba za Asili

Hizi familia za kuwa nazo makini mara mtoto wa baba mkubwa mara shangazi kumbe moyoni wana lao jambo umesema mlizika kitu kingine ni kwamba mshua alichukuliwa msukule? baada ya kuwatenda watesi wenu hamjapata kasumba tena?

Ndio maana mimi na mambo ya misaada sijui kutuma hela kwa wajomba huko vijijini nilishaacha maana hawana dogo wanaweza tumia pesa unayowatumia kukuadhibu wewe...

Pia naomba unisaidie namba ya huyo mtaalamu maana mwishoni mwa mwaka jana huku ninapokaa kuna asubuhi moja nimeamka kutoka nje nikakuta kuna damu, majimaji na majivu kwenye mlango wangu wa kuingilia sebuleni nikajua wazee wa kazi wananiwinda...

Hivyo na mimi ni muda wa kujihami sasa, mwisho kabisa huku maofisini tuwe makini sana huwezi jua ni nani hasa anatamani nafasi uliyopo muda wowote wazee wa kazi wanapindua meza...
Fafanua uliposema wanaweza kutumia hela uliyowatumia kukuadhibu
 
Kitakacho punguza uchawi ni maendeleo vijijini, wapelekewe umeme giza liondoke, wajenge nyumba za kujitegemea na mageti siyo Kila unachofanya wenzio hawana wanaweka husuda, misitu ipungue miti ya dawa itapotea, watabaki huko huko vijijini mwisho wanaishia huko huko vijijini bila kuja mjini Ila Kama niwachi wa kwenye familia Sasa hapo mtu atapambana na hali zao.

Chief ukisema misitu ipungue ili miti ya dawa ipotee naona kama umeenda mbali sana!

Hivi unafahamu ya kwamba chochote kile kina matumizi ya aina mbili, matumizi mazuri (ya kheri) na matumizi mabaya (ya Shari)?! Hata maandiko matakatifu, majina ya mitume na hata la Muumba mwenyewe, yakitumika vibaya ni hatari sana na yakitumika vizuri ni zaidi ya Poa sana?!

Tumejaaliwa kila aina ya mitishamba yenye kuagua almost 90 percent ya maradhi ya kidunia katika mfumo wa misitu na mapori across all over Tanzania! Hii mitishamba ikitumika vizuri inawezekana kabisa kuleta matokeo chanya ndani ya jamii hasa kulingana na asilimia kubwa ya wananchi hali kiuchumi sio safi sana na hizi mitishamba ni affordable!

Kwa sasa Taifa pia liko na wasomi wengi tu na advantage kubwa zaidi ni technological era tuliyomo, which means elimu sahihi ikipatikana na utafiti sahihi ukafanyika na namna bora ya matumizi ya mitishamba hii ikifahamika kwa angalau asilimia 60 ya wananchi, tutaokoa wengi sana na mengi sana, Taifa laweza kuponywa.

****
Sipendi kabisa kumuogopa mchawi kiasi cha kuhitaji kujicompromise ili tu niweze kumuaccomodate ndani ya jamii yangu, ukimuogopa anatumia hiyo fear as your core weakness na ndipo anakuumiza zaidi na kuiumiza jamii!

Tusiwaogope wachawi, waelekezwe namna bora ya kutumia hiyo taaluma yao kuleta manufaa kwa jamii na Taifa badala ya kuroga hovyo hovyo! Tuikutanishe taaluma hii na sayansi tuzalishe suluhisho la umaskini wa wengi wetu! Wachawi wakijikita katika kutemesha madini migodini kwa kutumia taaluma yao plus science & technology, all combined, we may be surprised! Ila Muumba awe dereva wa vyote!
 
Huu Uzi Umenifungua macho maana Ninayopitia ni magumu mno tangu mwaka jana Nilivunjiwa ofisi Yangu Nikaibiwa huku Mbagala Mwenye nyumba akanipeleka sehemu kwa Mtaalamu Sikufanikiwa chochote,Mzee mwingine akanipeleka sehemu nyingine aisee Nimerudi nyuma kinoma from hero to zero yaani Nimechakaa kupata kazi au hela ni mbinde nagongea mpaka elfu tano au buku mbili kwa Mara ya kwanza Nimeshindwa kulipa kodi wala kununulia watoto nguo za shule yaani acha tu Ndevu hizo yaani kibali sina kabisa Nimejifungia ndani mwaka mzima Nasali aisee sijui Nimemkosea nini Mungu yaani Niliowazidi maisha wamenipita mpaka simu zangu hawapokei kwa Mara ya kwanza naoga dawa za waganga Mtu ambaye Nilikuwa Nikiomba Mungu Anajibu hapohapo yaani ebwana eeeh kelele za Mwanamke sasa yaani imefika hatua Wanasema Nitafia ndani Wale Wazee kumamae zao sijui wamenifanya nini yaani basi tu kushinda na kulala njaa kawaida Mtu ambaye Nimesaidia Watu leo Nimefua yaani noma.
Pole sana mkuu. Usikate tamaa, utasimama tena kiuchumi ndg. Ila usiache kumuomba Mungu siku zote.
 
Huu Uzi Umenifungua macho maana Ninayopitia ni magumu mno tangu mwaka jana Nilivunjiwa ofisi Yangu Nikaibiwa huku Mbagala Mwenye nyumba akanipeleka sehemu kwa Mtaalamu Sikufanikiwa chochote,Mzee mwingine akanipeleka sehemu nyingine aisee Nimerudi nyuma kinoma from hero to zero yaani Nimechakaa kupata kazi au hela ni mbinde nagongea mpaka elfu tano au buku mbili kwa Mara ya kwanza Nimeshindwa kulipa kodi wala kununulia watoto nguo za shule yaani acha tu Ndevu hizo yaani kibali sina kabisa Nimejifungia ndani mwaka mzima Nasali aisee sijui Nimemkosea nini Mungu yaani Niliowazidi maisha wamenipita mpaka simu zangu hawapokei kwa Mara ya kwanza naoga dawa za waganga Mtu ambaye Nilikuwa Nikiomba Mungu Anajibu hapohapo yaani ebwana eeeh kelele za Mwanamke sasa yaani imefika hatua Wanasema Nitafia ndani Wale Wazee kumamae zao sijui wamenifanya nini yaani basi tu kushinda na kulala njaa kawaida Mtu ambaye Nimesaidia Watu leo Nimefua yaani noma.
Pole sana mkuu ila usiache kusali
 
uchawi kwa kiasi kikubwa upo sehemu zenue umaskini, maana umaskini huzaa wivu, chuki, roho mbaya, n.k huko kwa mitaa ya matajiri upo ila nakuhakikishia haufikii hata asilimia 20 ya ule wa uswazi ambao watu wengi mno wanashiriki.

ukishajijua una uwezo nenda penye nafuu tu kuliko kwenye majanga,

huwa natamanigi mno shetani angebadili hii kero ya wachawi iwe hata ya ujambazi, aisee wachawi wanakera jamani wasikieni tu.

Yani nilivyopigwa hizo chale nikaanza kusoma maneno tofauti, mfano sio naisoma ndio, kaja naisoma hakuja, 7 naisoma 2, alifanya naisoma hakufanya, yani bila kusoma mara 2 kuhakikisha nilikuwa napoteza mda. nakumbuka kuna kipindi kitu kinaweza kuwa mezani sikioni nakitafuta sana ila nakuja kukiona mezani, Duh nlikuwa sina amani, naogopa kusinzia maana nikiamka karibu kila wiki lazima nikute nimechanjwa.

Baada ya matambiko huko ndo hali ikaisha, kuanzia siku hio nawaonea sana huruma ambao hawaamini uchawi upo, hawa ndio huwa wakichezewa hawajitambui wala kufanya juhudi ya kutatua tatizo wao wanalikubali tu.

Mchawi ni mtu mshenzi sana,
Daah mimi nimekwaruzwa mgongoni na mabegani sana hadi damu nikiwa nafanya project moja huko mbeya, ilibidi nihame ule mtaa ndio ikatulia ila sijawahi kwenda kwa mtaalam maana sijui hata naanzia wapi
 
Kwangu ni mamdogo kabisa, mke wa bamdogo. Ukoo mzima akamaliza na mama yao ambaye ni bibi yangu mzaa baba. Bibi na bamdogo mumewe(eti kaanguka chooni). Wamekufa juzi hapo 2019 kwa kufatana, pale kijijini homeground pamejaa makaburi tu. Sasa alikuja kukosea akataka akavamie pale akae, weeeeh alienda mwenyewe church kukiri na kusema yote aliyofanya.

Ukimuona sasa, mpolee, mnyenyekevu na mtu wa church haswa. Ila ndo hivyo kapurura ukoo mzima.
Mi nimekoswa koswa nae mara kibao. Namfikiria tu nifanyeje baada ya kuskia ukoo kamaliza ni kazi yake. Sema si watu wa Dini sana toka kwa bibi kulipiza kichawi siwezi.
 
Kwangu ni mamdogo kabisa,mke wa bamdogo.
Ukoo mzima akamaliza na mama yao ambaye ni bibi yangu mzaa baba.
Bibi na bamdogo mumewe( eti kaanguka chooni)
wamekufa juzi hapo 2019 kwa kufatana
Pale kijijini homeground pamejaa makaburi tu.
Sasa alikuja kukosea akataka akavamie pale akae,
weeeeh alienda mwenyewe church kukiri na kusema yote aliyofanya.
Ukimuona sasa, mpolee,mnyenyekevu na mtu wa church haswa.
Ila ndo hivyo kapurura ukoo mzima.
Mi nimekoswa koswa nae mara kibao
Namfikiria tu nifanyeje baada ya kuskia ukoo kamaliza ni kazi yake.
Sema si watu wa Dini sana toka kwa bibi kulipiza kichawi siwezi.
Ebana na mm nimeshuhudia kisa cha Kichawi

Ikoo hivii mwishoni mwa mwaka nilienda Ukerewe kuna kisa cha kushangaza kidogo....

Mwaka 2017 wavuvi watatu kijiji cha Busagami walienda kuvua, wakapigwa na dhoruba wakazama..wakafa wote..kumbe walichukuliwa misukule na aliyewachukua akawa anawatumia kuvuta kokoro, basi si unajuaa hayaa mambo bhna kumbe pale pale kuna wale watu ambao nao sioo kidogo wana ndagu basi wakawa wanawaona wakija kwenye kokoro katika fatilia fatilia ikaonekana aliyewachukua kumbe alifariki so akakosa wa kutunza hiyo misukule basi, yule mwenye mtoto akapewaa taarifa kuwa tunamuona kijana wako tupe hela tumkamate jamaa akakataa baadae akakubali wale wakaenda kuvuta kokoro misukule ikaja kamata ile mingine miwili ikakimbia peleka polisi pale muriti wakamuita mwenye mtoto akadai mm wangu nshazika kama ni ivyo twende tufukue kaburi niwaoneshe nipenia askari wakampa Askari fika kaburi fukua (kumbuka walipozama maiti zilipatikana na zikazikwaa kwenye turubai) ilee fukua fukua kwenye kaburi, turubai walikutaa mifupa ya Samaki, Kifupi walizika Sangara na sio Binadamu... basi ikabidi kwenda kwa waganga ili kumfanya awe poa, manake alikuwa aongei, kakatwa ulimi, nywele ana afro, mikono ndani ndo nje....yaan uku nyuma ya Kiganja ndo anakoshikia, na unaambiwa walikuwa wakipata pesa wanagawana wanaenda hotelini kula chakula yaan bila kuonekana (invisible) pambana pambana ndo dogo kaanza kuongeaa hii Juzii tu last j5, japo ajasema nn kilimpataa...hapaa na walimleta kakakuru watu tukashuhudia...alikufa june 2017 amepatikana sept 2020....


Uchawii upooo.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebana na mm nimeshuhudia kisa cha Kichawi

Ikoo hivii mwishoni mwa mwaka nilienda Ukerewe kuna kisa cha kushangaza kidogo....

Mwaka 2017 wavuvi watatu kijiji cha Busagami walienda kuvua, wakapigwa na dhoruba wakazama..wakafa wote..kumbe walichukuliwa misukule na aliyewachukua akawa anawatumia kuvuta kokoro, basi si unajuaa hayaa mambo bhna kumbe pale pale kuna wale watu ambao nao sioo kidogo wana ndagu basi wakawa wanawaona wakija kwenye kokoro katika fatilia fatilia ikaonekana aliyewachukua kumbe alifariki so akakosa wa kutunza hiyo misukule basi, yule mwenye mtoto akapewaa taarifa kuwa tunamuona kijana wako tupe hela tumkamate jamaa akakataa baadae akakubali wale wakaenda kuvuta kokoro misukule ikaja kamata ile mingine miwili ikakimbia peleka polisi pale muriti wakamuita mwenye mtoto akadai mm wangu nshazika kama ni ivyo twende tufukue kaburi niwaoneshe nipenia askari wakampa Askari fika kaburi fukua (kumbuka walipozama maiti zilipatikana na zikazikwaa kwenye turubai) ilee fukua fukua kwenye kaburi, turubai walikutaa mifupa ya Samaki, Kifupi walizika Sangara na sio Binadamu... basi ikabidi kwenda kwa waganga ili kumfanya awe poa, manake alikuwa aongei, kakatwa ulimi, nywele ana afro, mikono ndani ndo nje....yaan uku nyuma ya Kiganja ndo anakoshikia, na unaambiwa walikuwa wakipata pesa wanagawana wanaenda hotelini kula chakula yaan bila kuonekana (invisible) pambana pambana ndo dogo kaanza kuongeaa hii Juzii tu last j5, japo ajasema nn kilimpataa...hapaa na walimleta kakakuru watu tukashuhudia...alikufa june 2017 amepatikana sept 2020....


Uchawii upooo.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Upo saana, kwetu juzi baada ya misiba hiyo miwili alipovagaa ardhi ndo alikiona cha moto.
Maana hamna aliyebakisha akaona rahisi tu kuhamia.
Yaliomkuta ndo kaongoza mwenyewe kwa mchungaji kusema kwamba yeye ndo mlozi na misiba yote pale kashiriki kutenda.
Ikabidi sister aende akamsikilize ndo pona yake.
 
Hizi familia za kuwa nazo makini mara mtoto wa baba mkubwa mara shangazi kumbe moyoni wana lao jambo umesema mlizika kitu kingine ni kwamba mshua alichukuliwa msukule? baada ya kuwatenda watesi wenu hamjapata kasumba tena?

Ndio maana mimi na mambo ya misaada sijui kutuma hela kwa wajomba huko vijijini nilishaacha maana hawana dogo wanaweza tumia pesa unayowatumia kukuadhibu wewe...

Pia naomba unisaidie namba ya huyo mtaalamu maana mwishoni mwa mwaka jana huku ninapokaa kuna asubuhi moja nimeamka kutoka nje nikakuta kuna damu, majimaji na majivu kwenye mlango wangu wa kuingilia sebuleni nikajua wazee wa kazi wananiwinda...

Hivyo na mimi ni muda wa kujihami sasa, mwisho kabisa huku maofisini tuwe makini sana huwezi jua ni nani hasa anatamani nafasi uliyopo muda wowote wazee wa kazi wanapindua meza...
Mtangulize Mungu Mbele achana na mambo ya mtaalamu binadamu, mtaalamu pekee ni Mungu.
 
Chief ukisema misitu ipungue ili miti ya dawa ipotee naona kama umeenda mbali sana!

Hivi unafahamu ya kwamba chochote kile kina matumizi ya aina mbili, matumizi mazuri (ya kheri) na matumizi mabaya (ya Shari)?! Hata maandiko matakatifu, majina ya mitume na hata la Muumba mwenyewe, yakitumika vibaya ni hatari sana na yakitumika vizuri ni zaidi ya Poa sana?!

Tumejaaliwa kila aina ya mitishamba yenye kuagua almost 90 percent ya maradhi ya kidunia katika mfumo wa misitu na mapori across all over Tanzania! Hii mitishamba ikitumika vizuri inawezekana kabisa kuleta matokeo chanya ndani ya jamii hasa kulingana na asilimia kubwa ya wananchi hali kiuchumi sio safi sana na hizi mitishamba ni affordable!

Kwa sasa Taifa pia liko na wasomi wengi tu na advantage kubwa zaidi ni technological era tuliyomo, which means elimu sahihi ikipatikana na utafiti sahihi ukafanyika na namna bora ya matumizi ya mitishamba hii ikifahamika kwa angalau asilimia 60 ya wananchi, tutaokoa wengi sana na mengi sana, Taifa laweza kuponywa.

****
Sipendi kabisa kumuogopa mchawi kiasi cha kuhitaji kujicompromise ili tu niweze kumuaccomodate ndani ya jamii yangu, ukimuogopa anatumia hiyo fear as your core weakness na ndipo anakuumiza zaidi na kuiumiza jamii!

Tusiwaogope wachawi, waelekezwe namna bora ya kutumia hiyo taaluma yao kuleta manufaa kwa jamii na Taifa badala ya kuroga hovyo hovyo! Tuikutanishe taaluma hii na sayansi tuzalishe suluhisho la umaskini wa wengi wetu! Wachawi wakijikita katika kutemesha madini migodini kwa kutumia taaluma yao plus science & technology, all combined, we may be surprised! Ila Muumba awe dereva wa vyote!
Nimekuelewa sana u wrote kile kilichokuw kicwhan mwangu!! 👊👊
 
Habari ndugu zangu,

Kwa kuwa leo nimetulia ngoja niwaeleze visa nilivyowahi kuviona katika safari yangu ya mwisho wa mwaka nilipomtembelea ndugu yangu ambae ni mganga.

Kwanza kabisa mimi tangu awali siamini mambo ya uchawi wala sina imani juu ya ulozi na uwepo wake hivyo ndugu yangu pamoja na kufanya shughuli hizo na kuendesha maisha yake lakini nilijua ni vitu ambavyo havipo.

Siku moja alfajiri alijiwa na ugeni wa bibi kizee na mjukuu wake msichana wa kama miaka 28 hivi kilingeni kwake, pamoja na kwamba siamini ushirikina lakini sikuonyesha wazi nilipokuwa pale ili niwe karibu nipate kujua undani wa haya mambo hivyo nikawa naingia kilingeni kwake kwa utiifu kuona utendaji na matokeo.

Na pia ni vigumu kumdharau kwa sababu amewekeza kuliko mimi msomi

Basi ndugu zangu, yule msichana alikuwa amedhoofu sana ishara kuwa ni mgonjwa wa muda mrefu, ramli ikaangaliwa na wakaambiwa mengi ambayo walikubaliana nayo mfano kama vile siku yalipoanza maradhi, namna anavyojisikia na chanzo cha maradhi.

Wakaandikiwa vifaa na kuondoka ili wakavitafute, cha ajabu ilipofika saa kumi jioni yule bibi akarudi peke yake na kumuuliza mganga kama anamkumbuka? Akajibiwa "Naaam si ulikuja asubuhi na mgonjwa, vipi maendeleo yake? Bibi akajibu sikuletwa na maendeleo yake ila nimekuja kukuomba akija usimuague na kwa kuwa ulimpa namba basi akikupigia mwambie umesafiri na kuhamisha kilinge kabisa!

Mganga akasema "kama hutaki aaguliwe ulimletea nini kwangu? Bibi akasema "kama nisingemleta ingewezekana vipi nije tuongee kama hivi mwanangu? Nimemleta nipajue na tujuane ili nije tuongee kama hivi, maana nisingemleta angekuja mwenyewe tu maana si unajua ameshasifiwa kwako".

Mganga akauliza nini lengo lako na ikiwa yule ni mjukuu wako kama ulivyosema asubuhi na kunisisitiza mbele yake nimuague apone kwani mmemaliza tiba zote na haponi?

Ajabu hapo yule bibi akavuta pumzi ndevu na kutabasamu huku akimsogelea kidogo karibu mganga na kusema "Enheee sasa hapo umeuliza swali la kiutu uzima, najua ki umri wewe ni mdogo sana kwangu ila kwa kuwa umeingia kwenye kazi hii basi wewe ni mtu mzima mwenzetu. Mimi nipo kwenye ngoma zetu hizi za utu uzima za usiku, unanielewa?
Mganga akajibu kifupi "endelea tu..

Bibi akaendelea..."yule ni mjukuu wangu kabisa na mama yake nilimtafuna mwaka tisini na mbili na nikapata daraja nzuri tu kwa kuanzia, ila sasa huyu binti ile ni kazi yangu mimi hivyo muda si mrefu nitaimaliza naomba usinirudishe nyuma! Kwani akifa leo yule basi mimi nitakuwa katika daraja nzuri sana na kilemba cha ngazi sita, nitakuwa na mimi nakaa kwenye kiti cha enzi na kutoa hukumu mbali mbali nimechoka kudharauliwa na watoto wadogo!

ITAENDELEA NGOJA NIPATE CHAKULA KWANZA...

NB: Hapa naeleza niliyoyaona kwa macho yangu na hakuna tangazo la uganga na sitahusika na hayo na pia sipo kuaminisha watu imani ya giza hivyo tujikite katika mikasa pekee.

=====

Baada ya yule bibi kusema hayo akanyamaza akisubiri majibu ya upande wa pili.

Moyoni mwangu nilidhani labda mganga atamfukuza yule mchawi au hata kugombana nae kutokana na hizo hila zake za kishenzi, ila kinyume chake mganga akatulia kidogo na kisha kumuuliza yule bibi, "unafanya hayo yote ili kuutumikia uchawi! Uchawi una faida gani?

Bibi akatabasamu na kujibu kwa hisia za furaha "baba uchawi una faida kubwa mno mwanangu kuzidi hata huo uganga wenu, mimi hapa nilipo nina pembe inakaa ziwani...inakusanya pesa za biashara za mji mzima kwa njia ya chumaulete, hebu fikiria ni wangapi ambao hawajazindika shughuli zao na wananichumia mimi? Bado sijagusia misukule ambao hunisaidia na kunizalishia mashambani kwangu.

Mganga akauliza tena kwa kama dharau fulani hivi, "sasa kama mna nyenzo hizo mbona mnakufa masikini na kuishi katika nyumba duni, kula yenu tu ni tabu achilia mbali mavazi yenu?

Ndugu msomaji, huyo bibi alikuwa amevaa khanga tofauti kuukuu na chini amekuja na ndala tofauti zilizoshonwa shonwa hivyo yale maongezi yake yalishangaza kidogo.

Safari hii bibi alicheka kwa kama kebehi na kumjibu mganga, "kumbe mwanangu bado wewe ni mtoto mdogo sana hujui kitu! Sisi fahari yetu siyo mchana ila ni usiku! Kwenye mwembe mkubwa kikaoni ndiyo utamjua tajiri ni nani kulingana tu na usafiri na zana za gharama atakazo ingia nazo...wapo wanaingia na ungo, wanaoingia na Fisi, wanaokuja kwa ufagio na ndege ya watu wengi nk na pia kuna watu wana pembe wamenunua zaidi ya milioni ishirini na hiyo ikiwekwa chini huioni na hata ukionyeshwa hutaweza kuinyanyua na uganga wako wote.

Najua nyinyi ufahari wenu ni makazi, mavazi na kula ila sisi raha yetu ipo sehemu tofauti kabisa na nikujuze tu usiku ni raha sana mwanangu na sasa nikipata hiki cheo nauelekea ukubwa sasa na kiti changu kitabebwa juu juu na katika mji nitaheshimika mno.

Maongezi yalifika mpaka muda wa magharibi na adhana ikalia...hapo yule bibi akasema naondoka nawahi kusali lakini ufanye hivyo nilivyokwambia au kama shida ni pesa nikupe mimi hilo fungu ulilopanga akupe bora tu usimuague.

Bibi wakati akisema hayo alifungua fundo kwenye nguo yake na kuonekana noti nyingi ambazo pengine zinaweza fika hata laki mbili au zaidi! Mganga akasema; sihitaji pesa ila nikuulize jambo? Sasa unakwenda kusali ili iweje ilihali wewe ni mchawi? Huoni unazidi kukufuru?

Bibi akasema huku kasimama anataka kuondoka "unapoingia katika uchawi masharti yake inatakiwa uvae kofia mbili, moja ya uchawi na nyingine ya Imani...hapa kwenye imani unaweza kushika dini sana uwe Mkristo, Muislam au dini yeyote na ukishindwa hilo basi kuwa na imani ya kupenda watu sana na kujitoa...hii inasaidia hata akitokea mtu mmoja akisema wewe ni mchawi, watatokea kumi watakao pingana nae na kuwa upande wako.

Mganga akasema kwa hasira; tafadhali ondoka usije ukadhurika, mimi ni mganga wa majini hivyo sirubuniwi na yeyote bali nawafuata wao walionipa uganga...ondoka haraka kabla sijachoma ubani ukapigwa na chini sasa hivi maana hawataki mambo machafu na ya kipumbavu namna hiyo!!!


NAENDELEA KUANDIKA HIVI NDUGU ZANGU...

======

Yule bibi alisema neno moja tu, UCHAGUZI NI WAKO SASA!! kisha akaondoka kwa hasira.

Tukabaki sisi wawili na kwa haraka nikamwambia kwa nini usingechukua mshiko ule na akanijibu kwamba yule hana nia njema hivyo anaweza kukupa pesa kumbe tayari zina husda ndani yake.

Nikamwambia sasa utafanyaje, akasema yule ni mtoto mdogo sana hivyo kwake hafui dafu na angetaka angemdhuru lakini kwa kuwa kaja ki binadamu ndiyo maana hakuona sababu ya kumdhuru na kuwa msimamo wake wa kumuagua yule binti uko pale pale rabda asije.

Tukaachana na hayo na ikapita wiki salama salmini huku akiendelea kutibu wageni wake tofauti tofauti bila wasiwasi wowote mpaka siku hiyo mida ya jioni akapigiwa simu na yule binti na kuulizwa kama amerudi au ndiyo amehama kabisa!

Kurudi wapi? Aliuliza ndugu mganga.

Binti akasema; "nilikamilisha vifaa ulivyoniagiza tangu siku ya tatu kutoka siku tuliyokuja, nikataka kukupigia simu unipangie siku ya kuja ila bibi akasema atakuja huko yeye...akaja na aliporudi akasema ameambiwa haupo umehama kabisa!!

Mganga akajibu tu mbele kwa mbele, "Naam nimerudi hivyo njoo keshokutwa kwa sababu kesho ni Jumanne siyo nzuri kwa tiba zako kwani kesho huwa inatawala Mirihi ambayo ni moto....lakini pia masharti ni kuwa usije na mtu wa nasaba yako akimaanisha mtu mwenye undugu nae.

Yule msichana akaanza kulalamika sana kuwa atamruka vipi bibi yake ilihali ndiye mtu pekee anae mhangaikia na kumjali, kumpenda na kumhudumia kila jambo.

Mganga siwezi kuacha kuja na bibi yangu maana ndiye kipenzi changu wa pekee na isitoshe amenilea!! Binti alilalama.
Mganga akajibu kifupi tu kama imeshindikana tafuta mganga mwengine! Binti akaomba msamaha na kuahidi atakuja hiyo keshokutwa na rafiki yake.

Usiku wa siku hiyo ya jumatatu ndugu yangu ambae ndiye huyo mganga alisema anajisikia vibaya mara akawa anaandika makombe anakunywa mara mara anajifukiza madawa ya mitimiti ila bado hali haikuwa hali na kufika usiku wa saa tisa akaamka mke na majini kichwani na kusema kuna matatizo ila mambo yote tumuulize kiti wake kwani ameshamuotesha tatizo na ufumbuzi.

Jini alipotoka na muda huo jamaa anagara gara tu chini akiugulia, shem akasema alioteshwa kikao kikubwa sana cha wachawi na mmoja wapo ni bibi ambae kama alishawahi kuja, kikao hicho kilikuwa na watu wengi mfano wa soko na kuna mtu mmoja amekaa kwenye kiti cha kifalme huku yule bibi akimshika miguu na kulalamika maneno haya "mkuu!!! Sio kama sitaki kulitimiza jambo letu ila kuna mganga ndiye kikwazo anataka kuturudisha nyuma mkuu!! Nimemkanya ila hakusikia hivyo naomba kiti kifanye kazi yake mkuu".

Hapo yule mkuu akachagua watu saba ambao nao wamekaa kwenye viti vidogo na kuwaambia mganga anatakiwa afe mara moja na nyama yake iletwe hapa tuile huku tukiisimanga.
Chukueni silaha tatu pamoja na maji ya aina saba kwa sababu yule mganga ana zindiko la moto.

Wachawi wale waliochaguliwa hawakuuliza chochote zaidi ya kuinamisha vichwa kwa utiifu na kuruka juu kuja kwetu! Akasema lakini ipo njia aliyooteshwa kumsaidia mume wake...

Huyu mke wa mganga nae ana majini nae ingawa hajishughulishi sana na mambo ya uganga zaidi ya kutumwa moto na vitu vidogo vidogo tena kwa kufanya kuitwa, ila siku hiyo majini yake yalikuja kwa uchungu baada ya kuona mganga amezidiwa.

Mke wa mganga akasema njia ya kumsaidia kaonyeshwa hivyo akaingia kilingeni na kuchukua dawa kadhaa za maduka ya dawa za asili na kuchanganya na dawa fulani ya kwenye tunguri na kuchanganya na unga wa sembe na kisha kumpaka mume wake baadhi ya sehemu na nyingine kumnywesha.

Baada ya muda akapata nafuu na kunyanyuka na hapo tukaanza kumcheka kuwa kawezwa, na yeye akacheka kidogo na kusema wale wamekuja kiume lakini moto ukokwe arudishe majibu muda huo huo.

Hapo tukafanya haraka kukoka moto na kuuweka katika chungu maalum anachokiita Bukhuri shari, akabadili nguo na kuvaa nyekundu tupu hadi kilemba na kuchukua tunguri yake ambayo ki umbo ni kubwa kuliko zote alizonazo na tunguri hiyo kipindi anaitengeneza nilikuwepo na ni mpya mwenyewe anaiamini sana.

Tunguri hii alipokuwa anaiunda alimchoma bundi aliyeuwawa na makunguru na majivu yake akachanganya unga wa mti uliopigwa na radi, mti wa nyumba ambayo ina maiti ndani, kisiki kinachokwaa watu njiani, mzizi uliokata njia, unga wa kichwa cha nyoka na vitu vingine pamoja na damu ya kuku wawili wa rangi maalum na ule ulimi wa tunguri pia ni miongoni mwa miti yenye siri kubwa kulingana na maelezo yake.

Naam kwa mara ya kwanza nikaona tunguri hiyo imeshikwa kwa jazba huku akiuelekea moto na kusema leo naua kuanzia walioshiriki na mpaka vilivyomo katika nyumba zao! Akaanza na kutia ubani na kusema na Waalim wake! "Enyi majini nimechokozwa kama mlivyoona, hamkunipa uganga nije niteseke...mmeniachisha shughuli zangu za maana mkanitia kichaa ili leo yanikute haya nife? Sasa leo naangamiza watu na kama mnaona huruma na kuona ni kufuru kaeni pembeni, niacheni na wakulungwa wa bara nitende malukazi....
Duh!!!
 
Back
Top Bottom