Pole sana ndugu. Usiache muomba Mungu... japo binadam tumeumbiwa kusahau na uvivu poa.Jamani nina miaka mingi sijalog in huwa nasomaga tu ila huu uzi umenifanya nimelia sana acheni tu hii dunia.itoshe tu kusema nateseka lakini maombi yamenifunilia yalio sirini naonyeshwa kabisa anayenitesa. Ukiniona huwezi jua mateso nayopitishwa hapa nalia nitahadithia nikitulia
Ndio inavyokuaga hivyo yaani mi sitaki kukumbuka yaliyo huko kwetuInauma sana, yani unakuta unapitia mateso mengi katika maisha halafu mwisho wa siku unagundua kuwa mtu wako wa karibu sana ndo mhusika wa hayo yote.
Humu JF kuna mihemko ya kitoto sana. Mtu ndo kwanza umeanza story ye keshawaza njaa kwa sababu ana njaa.Mimi si mtu wa kaliba hiyo na sina njaa mkuu, tazama mara ya mwisho niliwahi kupost miaka mingapi nyuma...ndio maana wakongwe tumetulia hatupost chochote kutokana na ujinga ujinga na utoto wa siku hizi humu.
Wanasemaga katika majini yote duniani ni jini mmoja tu mkristo anaitwa Jimmy.Ngoja jamaa ashushe nondo hapa utawaelewa tu.....na usikute hata nawe uko kwenye kundi lao bila kujijua🤣🤣🤣...natania lkn,usimaindi ukanipiga kipapai🤣🤣🤣
Hadithia basiJamani nina miaka mingi sijalog in huwa nasomaga tu ila huu uzi umenifanya nimelia sana acheni tu hii dunia.itoshe tu kusema nateseka lakini maombi yamenifunilia yalio sirini naonyeshwa kabisa anayenitesa. Ukiniona huwezi jua mateso nayopitishwa hapa nalia nitahadithia nikitulia
Aisee kama yote haya umekariri we kiboko kabisaInaendelea....SEHEMU YA NNE
Huyu mke wa mganga nae ana majini nae ingawa hajishughulishi sana na mambo ya uganga zaidi ya kutumwa moto na vitu vidogo vidogo tena kwa kufanya kuitwa, ila siku hiyo majini yake yalikuja kwa uchungu baada ya kuona mganga amezidiwa.
Mke wa mganga akasema njia ya kumsaidia kaonyeshwa hivyo akaingia kilingeni na kuchukua dawa kadhaa za maduka ya dawa za asili na kuchanganya na dawa fulani ya kwenye tunguri na kuchanganya na unga wa sembe na kisha kumpaka mume wake baadhi ya sehemu na nyingine kumnywesha.
Baada ya muda akapata nafuu na kunyanyuka na hapo tukaanza kumcheka kuwa kawezwa, na yeye akacheka kidogo na kusema wale wamekuja kiume lakini moto ukokwe arudishe majibu muda huo huo.
Hapo tukafanya haraka kukoka moto na kuuweka katika chungu maalum anachokiita Bukhuri shari, akabadili nguo na kuvaa nyekundu tupu hadi kilemba na kuchukua tunguri yake ambayo ki umbo ni kubwa kuliko zote alizonazo na tunguri hiyo kipindi anaitengeneza nilikuwepo na ni mpya mwenyewe anaiamini sana.
Tunguri hii alipokuwa anaiunda alimchoma bundi aliyeuwawa na makunguru na majivu yake akachanganya unga wa mti uliopigwa na radi, mti wa nyumba ambayo ina maiti ndani, kisiki kinachokwaa watu njiani, mzizi uliokata njia, unga wa kichwa cha nyoka na vitu vingine pamoja na damu ya kuku wawili wa rangi maalum na ule ulimi wa tunguri pia ni miongoni mwa miti yenye siri kubwa kulingana na maelezo yake.
Naam kwa mara ya kwanza nikaona tunguri hiyo imeshikwa kwa jazba huku akiuelekea moto na kusema leo naua kuanzia walioshiriki na mpaka vilivyomo katika nyumba zao! Akaanza na kutia ubani na kusema na Waalim wake! "Enyi majini nimechokozwa kama mlivyoona, hamkunipa uganga nije niteseke...mmeniachisha shughuli zangu za maana mkanitia kichaa ili leo yanikute haya nife? Sasa leo naangamiza watu na kama mnaona huruma na kuona ni kufuru kaeni pembeni, niacheni na wakulungwa wa bara nitende malukazi....
Inaendelea....