Troublemaker
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 19,881
- 38,506
Amuokoe halafu yeye aangamizwe.Dah, watu makatili, ila jamaa yako ana makosa pia, kwa nn asimuokoe binti kama anaweza
Amuokoe halafu yeye aangamizwe.Dah, watu makatili, ila jamaa yako ana makosa pia, kwa nn asimuokoe binti kama anaweza
Yeye mganga ana majini yake, ataangamizwaje na anajiamini na majini anayo.Amuokoe halafu yeye aangamizwe.
Ngoja jamaa ashushe nondo hapa utawaelewa tu.....na usikute hata nawe uko kwenye kundi lao bila kujijua🤣🤣🤣...natania lkn,usimaindi ukanipiga kipapai🤣🤣🤣Wachawi huwa siwaelewagi saa zingine.
Noma sana.Nilimuuliza swali hili hili, akanijibu angemtibia angekuwa kaanzisha vita kubwa wangeitana jeshi kupambana naye, naye hakuwa na sababu ya kupambana vita isiyomhusu. Akanipa kisa kilichomtokea miaka miwili kabla, aliletewa mgonjwa yani mke alimleta mume akiwa mgonjwa sana jamaa anadai akakaa pale anamtibia. Anasema kuna siku akaamka kama anaumwa yani kama kachanganyikiwa anagawa gawa nguo anatoa wosia kwa watoto wake, ilikuwa ijumaa. Anasema baadaye akaja kijana akamwambia anaitwa na mzee yuko kwenye gari kule chini. Alipoenda akaambiwa aingie kwenye gari, mzee kuingia akamkuta mzee flani.
Eti akamuuliza kwanini unataka kuniharibia kazi yangu, huyo ni mwanangu na mimi ndiye nataka kumtoa kwa ajili ya biashara zangu. Jamaa akamwambia ashakula pesa lazima amalize kazi, mzee akatoa chupa na glass nyuma ya kiti cha gari akamwekea maji akamwambia kunywa nijue kama unataka pambana nami au utaachana naye.
Jamaa akanywa nusu glass kumaanisha kuwa hataki shari, wakaachana, alivyofika kwake akamwambia yule mama na mme wake kuwa ugonjwa umemshinda hawezi kuutibu. baadaye akakusikia yule jamaa alifariki.
Dalili za hapa zinaonyesha hii hekaya bado ndefu.
Twende kaziMkasa ni mzito sana na umenifanya nione hii dunia ipo tofauti kabisa...naendelea muda si mrefu mkuu.
Tayari mkuu.Twende kazi