VISA CARDS: Msaada please

cheusimangala

JF-Expert Member
Feb 27, 2010
2,585
497
hivi mtu akija hapa tanzania na VISA card ambayo amefungulia account katika nchi ya ulaya,anaweza kuingia ndani katika bank na kupewa pesa counter kama hataki kutoa pesa ktk ATM machines?kama inawezekana je ni katika bank gani?

..hope swali langu limeeleweka..
 
umeeleweka shost...mimi ninavyojua kwenye bureau de change ndio huwa inafanyika hiyo........kwa bank tusubiri mabankers waje watujuze
 
hivi mtu akija hapa tanzania na VISA card ambayo amefungulia account katika nchi ya ulaya,anaweza kuingia ndani katika bank na kupewa pesa counter kama hataki kutoa pesa ktk ATM machines?kama inawezekana je ni katika bank gani?

..hope swali langu limeeleweka..

Mbona kawaida tu...Hii ni interbank transaction ya kawaida, maana balance zote za mteja wa VISA CARD zinaonekana kwenye mtandao wa teller, kama ambavyo inakuwa katika ATM.
Na ijulikane kuwa kwenye ATM kuna limit ya withdrawal, hivyo kama mtu anataka kuchukua zaidi ni lazima aingie ndani!
 
Sio automatic kama ndugu yetu anavyotaka tuamini, huwezi tu kwenda over the counter ukafafanya hivyo sijui mwenzetu anazungumzia benki zipi labda azitaje. Ni sawa na wewe wa Tz huwezi kubeba CRDB visa card yako kwa mfano ukaenda marekani ama ulaya ukaingia benki yoyote ukapata, lazima uwe umefanya prior communication for example umeandika na ku sign TT huko ulikotoka ukielekeza kabisa ni benki ipi tena iwe na uhusiano na ile ya kule uliko na account, Swala la interbanking transaction linamaelezo yake. Nakushauri nenda kaulize kwenye tawi lako/benki yako huko uliko watakupa maelezo mazuri, kila case ni specific bado hatujafikia huko kwenye one touch, kama ambavyo hata huko ughaibuni bado hawafanyi hivyo na kila nchi.
 
Huwezi kwenda counter kuchukua fweza kwa sababu moja kubwa counter hawana chip n pin reader. Kitu unachoweza kufanya ni kuchukua katika ATM kiasi ambacho benki yako wamekubali unaweza kuchukua kwa siku. Benki ya Barclays ndio machine zake bomba hakuna tatizo. Other Banks mashine zake hazikubali ... ... ... jaribu bahati yako lakini Bongo kuna mashine ambazo zinaweza kukupatia US dollars currency.
 
Uzoefu niliopata binafsi, mimi nina account na Barclays UK, nilienda ndani tawi ya Barclays Dar na account details pamoja na Visa Card kwa sababu nilikuwa nahitaji kiasi cha Tshs. millioni moja, nilijua kwa vile ni Barclays haitokuwa shida, kumbe hapana! Adviser wao alinishauri hilo haliwezekani na ilibidi nitumie ATM kuchukua fraction ya pesa niliyohitaji.
 
hivi mtu akija hapa tanzania na VISA card ambayo amefungulia account katika nchi ya ulaya,anaweza kuingia ndani katika bank na kupewa pesa counter kama hataki kutoa pesa ktk ATM machines?kama inawezekana je ni katika bank gani?

..hope swali langu limeeleweka..

Haiwezekani kuchukulia Counter. Utaweza chukulia kwenye ATM machines zinazokubali aina ya kadi uliuonayo.

Ni sawa na sisi wenye Akaunti mfano Mimi nina acc Benki ya Posta, siwezi enda Kaunta ya CRDB au NMB kuchukua pesa, Ila Kama ATM machines zao zinakubali kadi yangu ya Uhuru, nitachukulia kwenye machine na watanicharge gharama flani hivi.
 
hivi mtu akija hapa tanzania na VISA card ambayo amefungulia account katika nchi ya ulaya,anaweza kuingia ndani katika bank na kupewa pesa counter kama hataki kutoa pesa ktk ATM machines?kama inawezekana je ni katika bank gani?
..hope swali langu limeeleweka..
Inawezekana kuchukua pesa kwenya ATM ila hiyo ATM lazima iwe imeandikwa VISA au MASTER CARD, kwa bongo zipo benki kama CRDB, KENYA COMMERCIAL BANK (KCB), BARCLAYS, STANDARD CHARTERD na nyingine kama MORGAN JP nk hizi zote unaweza kutoa pesa kwa visa credit card. Usiende NMB utaishia kutukanwa au THB, kwa NBC sijui mara ya mwisho nilipokuwa home walikuwa hawajaanza kupokea visa card ila walikuwa kwenye mpango. Nadhani inatosha kwa leo ila elewa kuwa kuna ghalama tofauti za kutoa kwa visa card, ni kama Tshs 5000/= kwa huduma ila nadhani siyo mbaya sana ukilinganisha na huduma yenyewe. Zingatia vile vile kiasi cha kutoa kwa siku nadhani kwa benki zetu huko hazizidi laki sita kwa siku kupitia ATM vinginevyo itakubidi umwone Bank Teller. Usiku mwema!
 
mimi nina MASTER CARD,niko nje ya nchi.Ninapokua bongo huwa natumia ATM ya Barclays pale OHIO STREET.Kila unapoweka card yako ndani ya ATM in one turn unaweza kuchukua 400,000shs.Lakini unaweza kuweka card yako as many times as you can on the same day,ikitegemea benki yako inakuruhusu uchukue pesa ngapi kwa siku.Mfano,benki yangu hapa Ugaibuni inaniruhusu kwa siku kutoa kwenye ATM nikitumia card yangu amount ambayo ni equivalent na kama milion tano za kitanzania.Kwa hiyo,siku moja nikiwa Tanzania,nililiweza kutumia MASTER CARD yangu pale Barclays,nkachukua milioni tatu na laki mbili kwa siku moja maana Bank yangu ya ughaibuni inaniruhusu hadi equivalent ya kama milion 5 per day kwa ATM.Nilichokua nafanya,nilikua naweka jadi ndani ya ATM nachukua laki 4,then nangoja kama dakika moja naingiza tena card nachuku a tena laki 4.Niliingiza kadi mara nane ,nkachukua a total of 3,200,000tshs.
Na hii nimefanya si mara moja kuna siku nilichukua kama milion2 per day.
Kuna siku nilichukua milion 1 per day.
sasa kwa kua kadi yako ni VISA CARD,na nina uhakikia ATM za Barclays zinakubali VISA CARD,basi hiki nilichofanya mimi,pia kwako nina hakika kinawezekana kwa asilimia mia.
Sasa pale Barclays OHIO STREET,OPPOSITE NA MOVENPICK HOTEL,wana ATM tatu.
ATM mbili ziko nje,ATM moja iko ndani.ATM za nje wameandika zinapokea VISA na MASTER CARD,lakini kwa sasa wameziblock,hazipokei VISA au MASTER CARD inayotolewa na BENKI isio bongo,ukiweka kadi yako,ATM itasema imeshindwa kuisoma.Kwa hiyo tumia ATM ya ndani ya BENK.Hiyo itakupa pesa bila wasiwasi kabisa.Utakachofanya,ni kuingia ndani ya BENK,kuwaambia wafanyakazi kuwa unataka kutumia ATM ya ndani mana ya nje imekataa,Watakuruhusu.
Kumbuka pia kwamba,inaweza benk yako ya ughaibuni ikawa inakuruhsu kuchukua kwa ATM mfano pesa ambayo ni sawa na milion tano za bongo kwa siku.Lakini unaweza kwenda Barclays,ukachukua mfano laki nane[yaani laki nne in two turns},then ukataka kuchukua tena laki nne mashine ikashindwa kukupa pesa,Hii hutokea ikiwa ATM inakuwa imeishiwa pesa.Hivyo,kama unataka pesa nyingi kwa siku moja,mimi huwa naenda asubuhi sana bado ATM ikiwa bado inapesa ya kutosha.
Pia ATM ya BARCLAYS inakundikia kuwa in one turn unaweza toka laki 4,Lakini usishangae siku moja unaweka kadi yako,unacommand ATM ikupe laki nne,then ATM ikasshindwa.Hii hutokea kama ndani ya ATM kwa siku hiyo wameweka pesa in terms of noti za elfu tano [badala ya noti za elfu kumi},hivyo laki nne kwa noti za elfu tano,unakuwa mzigo mkubwa kiasi kwamba hauwezi kupita kwenye eneo la ku release pesa la ATM,ukiona hivyo,basi komandi ATM ikupe laki mbili,na mambo yatakua ok.
Lakini ninakushauri,ikiwa ATM itakubali kukupa laki nne kila unapoweka kadi,basi tumia option hii ya laki nne .Kwa maana ukitumia option ya laki 2,utalazimika kuweka kadi mara nyingi kama unahitaji pesa nyingi{mfano kama unataka 3,200,000 utaweka kadi mara nane} na in every turn unapoweka kadi na kuchukua pesa,unalipia hiyo gharama [mfano kwa benki yangu,ikiwa nachukua pesa ATM nje ya nchi niliyopo kwa sasa,basi in every time ninapoweka kadi na kuchukua pesa wanani charge pesa ambayo ni sawa na kama shs 7,000 za TANZANIA]/
natumai umenipata vema sana.Haya maelezo nina hakika nayo kwa asilimia mia,,maana mimi nimekuwa nikifanya hivyo mara nyingi as lately as November 2009.
Kama kuna kitu hujanipata vema,usiwe na tatizo kuniuliza mkuu.
Mungu akubariki.
THE SON OF AFRICA a.k.a KIJANA WA KIJIJINI
 
hivi mtu akija hapa tanzania na VISA card ambayo amefungulia account katika nchi ya ulaya,anaweza kuingia ndani katika bank na kupewa pesa counter kama hataki kutoa pesa ktk ATM machines?kama inawezekana je ni katika bank gani?

..hope swali langu limeeleweka..

Barclays Do that for Master and Visa Card any branch
 
oh! mkuu huwezi kuchukua over the counter nduguyangu mtu asikudanganye, wewe inayokutambua ni atm yenye visa logo tu, kwani in practical teller anaweza ku debit kwenye akaunti ya benki husika tu na si vinginevyo, ndio maana huyo ndugu wa akaunti ya barclays uk alishindwa ku transact na barclays tz over the counter
 
ndani ya bank huwezi kupewa! kwanza shida itakuwa ni address proof hata kama unayo passport and all documents! kama una visa card unaweza kuchukua hela kaunta katika bank yako katika nchi uliyofungulia.

Note: unaweza kuchukua hela katika ATM zinazo support visa card popote pale duniani.
 
Preta,Pakajimmy,ndondo,wacha1.kweli,lizy,genekai,thesonofafrika,watu,furahaeliud and Pape.

nawashukuru sana kwa kunipa maelezo juu ya jambo nililoomba,special thanx kwa aliyenisaidia kubadili kichwa cha habari.

i love u guyz n thank u so much Mungu awabariki!
 
Barclays Do that for Master and Visa Card any branch
u mean,ukiingia counter teller anakupa pesa hata kama una Visa Card ya nchi nje ya tz?au!maana kwa jinsi wengi walivyoelezea inaonesha haiwezekani!.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom