Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,526
- 46,053
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.
Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.
Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.
Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k
Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.