Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,179
Wanabodi,

Salaam.

Hapa jf tuko wanachama wengi wenye shughuli mbalimbali. Kikubwa tunachokifanya ni kujadili tuu issues na kuishia kutoa maoni ambayo japo mengi huishia kutekelezwa mengi ya maoni mazuri ya humu huishia humu humu bila kufanyiwa chochote kwa vile mwisho wa uwezo wetu ni kujadili.

Mimi mwanachama mwenzenu wa jf, mbali ya shughuli zangu za kawaida kuniendeshea maisha yangu full time, mimi pia ni part time freelance producer wa vipindi vya Redio na Televisheni.

Nimejikuta ninaguswa sana na baadhi ya hoja zinazojadiliwa humu hivyo nimeona niutumie muda wangu wa ziada kuwatumikia Watanzania kwa kujitolea kuandaa vipindi vya Redio na TV vya Elimu kwa Umma kuhusu mada mbalimbali.

Kufuatia maoni mengi ya maana yanayotolewa na wanabodi kuhusu hoja mbalimbali nimeamua kujitolea to walk an extra mile kwa kuyatumia baadhi ya maoni/hoja katika vipindi maalum, series za talk shows kuhusu haya tunayojadili humu.

Kwa ruhusa ya invisible, na ruhusa yenu, nitaomba kutumia quote za baadhi ya members wa jf na nitatumia majina yenu haya haya ya jf, mara moja moja nitatoa number ya kupokea sauti kuhusu very specific issues na mara moja moja nitawaalika baadhi ya wana jf ambao hawatamaind expose ili kuchambua baadhi ya issues kwa maslahi ya taifa.

Ownership ya program itakuwa ni PPR kwa sababu ndio atafoot production costs na mwendeshaji wa kipindi nitakuwa ni mimi. Kwa kuanzia nitaanza na kipindi kimoja kwa mwezi, kikigain momentum kina kuwa by weekly, then weekly.

Main benefisharies wa program hizi ni Watanzania kwa ujumla ambao watakuwa more informed hivyo utakapo fikia muda wa kufanya maamuzi fulani, watafanya more informed decisions. Jf nayo itabenefit kwa ku feature more predominantly na baadhi ya mawazo ya hawa ma great thinkers wetu humu jf kama kina Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3 , Mchambuzi etc na ma gt wetu humu, yatawafikia watu wengi zaidi.

Kwa kuanzia nitawaomba wanabodi, kunikubalia kuiepuka siasa na kufuatia kukijua ni nini kilikikuta kile kipindi cha "Kiti Moto". Hivyo nitachagua mada kwa uangalifu sana, nitapenda kujikita kwenye mada za kijamii na za kimaendeleo na sio za kisiasa.

Kwa kuanzia
Prog1. Itahusu mgomo wa madaktari uliomalizika hivi karibuni.

Nimeatach draft script naomba wenye nafasi muipitie na kunipa mawazo yenu.

Nimepanga kuanza recording next week hivyo program itakwenda hewani in the next few weeks.

Natanguliza shukrani kwa ushirikiano wako.

Asante.

Pascal Mayalla.
 

Attachments

  • Scipt ya TV Prog ya Yatokanayo na Mgomo wa Madaktari-1st Draft..pdf
    64.3 KB · Views: 347
Mkuu ahsante kwa habari njema hiyo ila hicho kipindi kitakuwa kinarushwa kupitia tv zipi?
Nimeandaa barua kwenda kwenye TV stations zote kuomba free airtime. Kwenye TV nitajitambulisha mimi kama mimi na sio jf ili nisije nikafungiwa milango kabla!. Nilisha zungumza na baadhi ya wamiliki walionyesha kuwa positive as long as sio politics.
 
@Pascal sio wazo baya lakini implications zake may prove fatal kwa ustawi wa JF. Kinachoifanya JF iwe chachu ya mijadala mizito ni ule UHURU na anonymity anayopata mchangaiji. Watu wanaeleza mambo mazito humu kwa uhuru kabisa.

Sasa, idea yako ya kutumia majina ya JF kwenye talk shows zako mimi inanipa mashaka. Utaua hii platform inayotoa fursa hadimu kwa watanzania kueleza kero za msingi kwa taifa hili kwa uhuru zaidi kuliko ambavyo wangefanya kama wangetumia mainstream media i.e TV.

Pia ningependa niamini kuwa viongozi wengi, tena wazito wanapata points nyingi sana humu. Kama ulimsikiliza vema Waziri wakati wa zogo la madaktari pale Muhimbili alitamka wazi kuwa watu wamekuwa wanatoa tuhuma kwenye mitandao.

Binafsi ningeshauri tufikirie zaidi namna ya kuifanya JF iwafikie watanzania wengi (pengine watumie simu) kwani uhuru (msisitizo) wa kutoa mawazo ndani ya JF ni wa kulinda!
 
Tunashukuru mkuu, ila kumbuka tuko makini na wewe uwe makini mkuu. Wacha tupitie script kwanza.......
Bukanga, kwa vile jf ina michango makini na michango ya ovyo, tutachagua ile makini tuu na ile ya ovyo tutaachana nayo. Kwa vile program hizi sio za kisiasa hivyo pia niko aware na maoni extreme yatakajifungamanisha na sera za vyama vya kisiasa.
 
Utupe kituo cha TV kitakacho rusha haya mawazo yetu,mimi nashauri iwe ni TV ambayo coverage yake ni kubwa...isije ikawa ni Mlimani TV..otherwise for me it is a good idea and I appreciate.
 
NI wazo zuri sana Pasco ila ni vyema pia kujua dhamira yako hasa ni ipi!! nauliza hili swali kwasababu kama ulikua biased wakati wa mgomo, then your views will never be balanced and you as a moderator, you may choose what to present

I LIKE THE IDEA, I LIKE IT A LOT,, BUT I DONT LIKE THE FIRST TOPIC
 
@Pascal sio wazo baya lakini implications zake may prove fatal kwa ustawi wa JF. Kinachoifanya JF iwe chachu ya mijadala mizito ni ule UHURU na anonymity anayopata mchangaiji. Watu wanaeleza mambo mazito humu kwa uhuru kabisa. Sasa, idea yako ya kutumia majina ya JF kwenye talk shows zako mimi inanipa mashaka. Utaua hii platform inayotoa fursa hadimu kwa watanzania kueleza kero za msingi kwa taifa hili kwa uhuru zaidi kuliko ambavyo wangefanya kama wangetumia mainstream media i.e TV.

Pia ningependa niamini kuwa viongozi wengi, tena wazito wanapata points nyingi sana humu. Kama ulimsikiliza vema Waziri wakati wa zogo la madaktari pale Muhimbili alitamka wazi kuwa watu wamekuwa wanatoa tuhuma kwenye mitandao.

Binafsi ningeshauri tufikirie zaidi namna ya kuifanya JF iwafikie watanzania wengi (pengine watumie simu) kwani uhuru (msisitizo) wa kutoa mawazo ndani ya JF ni wa kulinda!
FJM, hoja yako hii ni ya msingi sana, hata mimi nikiifikiria sana, kwa vile wengi wa members humu wanatumia pen names ili wasitambulike mathalan kwenye program yangu nikisema tusikilize maoni ya FJM, naweka maandishi ya quote yako ulichosema kuhusu mada fulani, then who will give a dam who FJM is?.

Ila pia ninaconcern uhuru wa watu kujinwaga ukawa jeopardized na knowledge kuwa wanaweza kuwa quoted.

Ndio maana nimeomba maoni yenu, kwa mfano mtu kama Mzee Mwanakijiji yeye tayari anatoa maoni yake kwenye magazeti mbalimbali hivyo sidhani kama atatatizwa na kuwa quoted as long as hautabadili kile alichokusudia.

Naomba maoni zaidi kwenye hili.
 
Wanabodi,
Salaam.
Hapa jf tuko wanachama wengi wenye shughuli mbalimbali. Kikubwa tunachokifanya ni kujadili tuu issues na kuishia kutoa maoni ambayo japo mengi huishia kutekelezwa mengi ya maoni mazuri ya humu huishia humu humu bila kufanyiwa chochote kwa vile mwisho wa uwezo wetu ni kujadili.

Mimi mwanachama mwenzenu wa jf, mbali ya shughuli zangu za kawaida kuniendeshea maisha yangu full time, mimi pia ni part time freelance producer wa vipindi vya Redio na Televisheni.

Nimejikuta ninaguswa sana na baadhi ya hoja zinazojadiliwa humu hivyo nimeona niutumie muda wangu wa ziada kuwatumikia Watanzania kwa kujitolea kuandaa vipindi vya Redio na TV vya Elimu kwa Umma kuhusu mada mbalimbali.

Kufuatia maoni mengi ya maana yanayotolewa na wanabodi kuhusu hoja mbalimbali nimeamua kujitolea to walk an extra mile kwa kuyatumia baadhi ya maoni/hoja katika vipindi maalum, series za talk shows kuhusu haya tunayojadili humu.

Kwa ruhusa ya invisible, na ruhusa yenu, nitaomba kutumia quote za baadhi ya members wa jf na nitatumia majina yenu haya haya ya jf, mara moja moja nitatoa number ya kupokea sauti kuhusu very specific issues na mara moja moja nitawaalika baadhi ya wana jf ambao hawatamaind expose ili kuchambua baadhi ya issues kwa maslahi ya taifa.

Ownership ya program itakuwa ni PPR kwa sababu ndio atafoot production costs na mwendeshaji wa kipindi nitakuwa ni mimi. Kwa kuanzia nitaanza na kipindi kimoja kwa mwezi, kikigain momentum kina kuwa by weekly, then weekly.

Main benefisharies wa program hizi ni Watanzania kwa ujumla ambao watakuwa more informed hivyo utakapo fikia muda wa kufanya maamuzi fulani, watafanya more informed decisions. Jf nayo itabenefit kwa ku feature more predominantly na baadhi ya mawazo ya hawa ma great thinkees wetu humu jf kama kina Mzee Mwanakijiji, Waberoya, Nguruvi 3 etc yatawafikia watu wengi zaidi.

Kwa kuanzia nitawaomba wanabodi, kunikubalia kuiepuka siasa na kufuatia kukijua ni nini kilikikuta kile kipindi cha "Kiti Moto". Hivyo nitachagua mada kwa uangalifu sana, nitapenda kujikita kwenye mada za kijamii na za kimaendeleo na sio za kisiasa.

Kwa kuanzia
Prog1. Itahusu mgomo wa madaktari uliomalizika hivi karibuni.

Nimeatach draft script naomba wenye nafasi muipitie na kunipa mawazo yenu.

Nimepanga kuanza recording next week hivyo program itakwenda hewani in the next few weeks.

Natanguliza shukrani kwa ushirikiano wako.

Asante.

Pascal Mayalla.
pascal mayalla

sikubaliani na hoja yako kamwe kwa sababu inawezekana umeshachukua kibahasha.yaani umeshaandaa andiko la kipindi ndo unakuja kuomba?huu ni unafiki tu.mimi naamini huu mfumo unaoendelea jf ni mzuri,ingawa wewe Pascal huoni kwamba jf inaleta impact kwa jamii.leo hii hakuna mkoa au ofisi ambayo utamkosa mwanajf,isitoshe magazeti na vyombo vingine vya habari wanachukua news kutoka jf.huu urembo unaotaka kuuleta unaweza kutuondolea ladha ya jf.kwenye hiyo script yako unasema mgomo wa madaktari umeisha rasmi!!are u sure!acha porojo zako Pascal!!
 
Nimeandaa barua kwenda kwenye TV stations zote kuomba free airtime. Kwenye TV nitajitambulisha mimi kama mimi na sio jf ili nisije nikafungiwa milango kabla!. Nilisha zungumza na baadhi ya wamiliki walionyesha kuwa positive as long as sio politics.

Ahsante kwa ufafanuzi wako, ila kama unavyojua JF maoni yake ya member wake ni mazito, je utaweza kuyasoma yote bila woga wowote au ndio utakuwa unatoa yale mepesi? Na je kwenye hicho kipindi chako utakuwa unaalika watu wa aina gani? achilia wale wa JF.
 
NI wazo zuri sana Pasco ila ni vyema pia kujua dhamira yako hasa ni ipi!! nauliza hili swali kwasababu kama ulikua biased wakati wa mgomo, then your views will never be balanced and you as a moderator, you may choose what to present

I LIKE THE IDEA, I LIKE IT A LOT,, BUT I DONT LIKE THE FIRST TOPIC
MTM, huyu sasa ni Pascal Mayalla, the real one. Pasco ni Pasco ana mawazo yake na bias zake na mimi Pascal Mayalla ni mtumishi wa watu, kipindi ni cha kuwatumikia watu, ukipitia script utaona nimejaribu ku strike the balance kati ya wadau mbalimbali.
 
Wanabodi,
Salaam.
Hapa jf tuko wanachama wengi wenye shughuli mbalimbali. Kikubwa tunachokifanya ni kujadili tuu issues na kuishia kutoa maoni ambayo japo mengi huishia kutekelezwa mengi ya maoni mazuri ya humu huishia humu humu bila kufanyiwa chochote kwa vile mwisho wa uwezo wetu ni kujadili.
Natanguliza shukrani kwa ushirikiano wako.

Asante.

Pascal Mayalla.


Mimi binafsi nakuunga mkono kwa asilimia zote. Ni kweli kuna mawazo mazuri sana humu ambayo yanaishia humu kwani si watu wote wanaojua huu mtandao. Ni kweli viongozi hasa wabunge kuna baadhi ni wanachama na wengine wanapita njia tu humu kupata kinachochangiwa.

Hivyo kwa uamuzi wako wa kutumia baadhi ya mada zenye mtazamo wa kijamii, mimi nakuunga mkono. na kama ulivyotoa tahadhari kuhusiana na siasa, hapo ni wewe wa kuchuja kipi kizuri kweli humu tunakosoa sana serikali ingawa wanaona kama sisi ni wapinga Serikali kumbe sisi tunatoa mawazo yetu. Hili ni kama Bunge kwani kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo na kukosoa, mbona hata Bungeni wanakosoana!!!!!!!!

Isipokuwa sisi huwa tunaingia kwa undani zaidi kuliko hata Bungeni, na mara nyingi hoja zetu huwa zinakuwana evidency hivyo siyo za kugushi kinachosemwa hapa ni kweli kipo nakama viongozi wa Serikali wangelikuwa wafuatiliaji wa kinachosemwa hapa ina maana nchi yetu ingellikuwa na maendeleo sana. Hapa tunapeana habari mpya za matukio ambazo hata vyombo vya habari wnyewe bado kuzipata sisi tumeshapata.

Mfano mimi hata kuangalia TV na magazeti huwa nimepoteza upenzi kwani hapa napata habari ambayo jioni nitasikia katika TV / Redio au kesho itaandikwa katika magazeti, sasa sioni umuhimu wa magazeti na TV/radio. Mimi kwangu JF ni chanzo cha habari tosha kabisa.

Pia naunga mkono wazo lako kwani nakumbuka kulikuwa na mtandao ambao kipindi cha nyuma "bcstimes.com" lakini naona siku hizi hakunahuenda viongozi wetu wa siasa wameshaupiga pini. Huu mtandao kutokana na mawazo mazuri tuliyokuwa tunayatoa uongozi waliamua kuchukua baadhi ya maoni yetu nakuyachapisha kama yalivyo katika GAZETI LA MAJIRA. yaani tulikuwa na ukurasa mzima kwa ajili yetu kwa wiki.

Inasaidia sana kufikisha ujumbe huu kwajamii ya Kitanzania na kuleta maendeleo.


Nakupongeza sana P. Mayalla kwa uamuzi wako huo na ninaomba wanachama wote JF tumuunge mkono.

naomba kutoa hoja:


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
NI wazo zuri sana Pascal ila ni vyema pia kujua dhamira yako hasa ni ipi!! nauliza hili swali kwasababu kama ulikua biased wakati wa mgomo, then your views will never be balanced and you as a moderator, you may choose what to present

I LIKE THE IDEA, I LIKE IT A LOT,, BUT I DONT LIKE THE FIRST TOPIC
ningekupa like lakini kitufe kimepotea
 
pascal mayalla=pasco

sikubaliani na hoja yako kamwe kwa sababu inawezekana umeshachukua kibahasha.yaani umeshaandaa andiko la kipindi ndo unakuja kuomba?huu ni unafiki tu.mimi naamini huu mfumo unaoendelea jf ni mzuri,ingawa wewe pasco huoni kwamba jf inaleta impact kwa jamii.leo hii hakuna mkoa au ofisi ambayo utamkosa mwanajf,isitoshe magazeti na vyombo vingine vya habari wanachukua news kutoka jf.huu urembo unaotaka kuuleta unaweza kutuondolea ladha ya jf.kwenye hiyo script yako unasema mgomo wa madaktari umeisha rasmi!!are u sure!acha porojo zako pasco!!
Jackbauer, mimi ni Pascal Mayalla mwenyewe. Pasco ni Pasco na mimi Pascal Mayalla ni Pascal Mayalla. Kumfananisha member yoyote wa jf na member mwingine ni kosa la name calling!.
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom