Zuckerman
JF-Expert Member
- Jun 14, 2016
- 1,375
- 2,417
sasa huoni kama hayo maandishi yalikuwepo baada ya Musa na miaka mingi kupita, ingekuwa ina maana kama yangeandikwa kabla ya Musa kujaUmesema kuhusu Tissue za Mafarao. Sasa yule Farao wa Misri aliomsumbua Sana Mussa na wana wa Israel. QURAN imesema mwili wake utahifadhiwa. Wala hautooza ili iwe fundisho kwa vizazi vijavyo. Na ndio maana mpaka leo ukienda Misri utaukuta mwili wake na ndani ya mwili wake kuna organs zote kama moyo, mapafu , utumbo nk. Heby jiulize toka Enzi za Mussa mpaka leo ni miaka Mingapi?
Quran inasema hivi:-
10:90-92
90.
Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!
91.
Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!
92.
Leo, basi, TUTAKUOKOA KWA MWILI WAKO, ili uwe ISHARA kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu.