MyTanzania
Senior Member
- Sep 9, 2008
- 106
- 8
Ndugu zangu ndani ya JF habari zenu.
Mimi nina matatizo ya vipele mwisho wa nywele za kichwani upande wa kisogoni ambavyo vinatokana na kunyoa.
Nimepata ushauri kwa madaktari mbalimbali juu ya dawa za kutumia bila mafanikio.Kama kuna mtu anajua ni namna gani naweza kutibu na pia kuzuia visitokee tena naomba tuwasiliane humu JF.
Nimeona watu wengi hivi karibuni wamekuwa na hali hiyo ambapo baadhi inapelekea kuota nyama kubwa baadaye. Naomba anayejua asaidie,maana najua watu wengi wanahangaika sana kuutibu ugonjwa huo sasa.
Nitashukuru kwa mtu yeyote aliye tayari kutoa msaada wa ushauri na hata kama kuna dawa aiandike humu niitafute.
Asante.WENGINE WENYE KUHITAJI UFUMBUZI WA TATIZO HILI
Naombeni msaada wenu hivi vidude naona vimekuja kwa kasi sana na Mara nyingi vinakua vingi zaidi nikienda kunyoa saloon na saloon nazoenda ni zile zenye kila aina ya usafi unaohitajika.
Lakini naona hivi karibuni vimeongezeka zaidi Kama vinavyoonekana hapo pichani.
Naombeni msaada wenu hivi vipele vinasababishwa na nn na tiba yake ni nn.
Hello JF Doctor,
Pengine kuna thread kama hii lakini ningependa kuomba msaada kwa mwenye uzoefu wa dawa inayoweza kutibu permanently vipele hivi. Wengine wanasema ni barber rashes, lakini mimi kwa zaidi ya miaka 3 sasa natumia mashine yangu binafsi nikienda kwa kinyozi. Nimejaribu kutumia mafuta mbalimbali na antibiotics nyingine kali lakini vinarudi. Naomba msaada kwa mwenye uzoefu.
View attachment 325127
FAHAMU TATIZO LA ACNE KELOIDALIS NUCHAE
Acne Keloidalis Nuchae ni nini?
Licha ya jina, acne keloidalis nuchae sio aina ya chunusi. Ni aina ya folliculitis, na dalili ambazo zinafanana na chunusi. Kwa kawaida huwa kama upele karibu na sehemu ya nywele upande wa nyuma wa shingo. Mwishowe haya huwa makovu na nywele zinzozunguka eneo hilo zinaweza kuondoka.
Tatizo hili linaweza kuwa lisizofurahisha, kukera na lenye kuleta maumivu na msongo wa mawazo. Wagonjwa wengi wa tatizo hili hupoteza kujiamini.
Folliculitis kwa upana inahusu kuvimba au kuambukizwa kwa follicle, yaani vishimo vya nywele. Folliculitis ni ugonjwa wa kawaida wa ngozi ambao unaweza kutokea mahali popote kwenye mwili ambapo nywele hukua.
Visababishi vya Acne Keloidalis Nuchae
Sababu haswa haijulikani. Walakini, kuna nadharia kadhaa za kuelezea hali hiyo, pamoja na:
- Kunyoa au kukatia nywele chini sana
- Kofia na mavazi
- Homoni
- Reaction ya kinga mwili
- Masuala yahusuyo vinasaba
Kofia na mavazi. Helmet au collars zilizovaliwa karibu na shingo zinaweza kuvuta kwenye nywele na kusababisha msuguano. Mvutano huu unaweza kuzidishwa na joto au jasho.
Homoni. AKN hutokea karibu kwa wanaume wazima, na kupendekeza kwamba androjeni zinaweza kuchukua jukumu moja kwa moja au kwa njia isiyo sawa.
Reaction ya kinga mwili. Antijeni ndani ya follicles ya nywele huvutia seli za uchochezi, na kusababisha uharibifu wa ukuta wa follicular na, mwishowe, upotezaji wa nywele (shida ya alopecia).
Masuala yahusuyo vinasaba
Nani yuko hatarini?
AKN huathiri kati ya 0.45% na 9% ya idadi ya watu. Inasemekana huathiri zaidi wanaume wenye ngozi nyeusi, haswa wale wa asili ya Kiafrika, ingawa inaweza pia kuwaathiri wenye ngozi nyeupe. Hali hii huanza baada ya ujana na ni nadra sana baada ya miaka 55.
Wanaume walio na nywele ngumu (kinky) wanahusika hasa na hili. Wakati hakuna uhusiano wa moja kwa moja, inadhaniwa kuwa hii inaweza kuwa ni kwa sababu ya kukata nywele na ni trauma inayosababishwa na wembe wa umeme. Kupindika kwa follicle ya nywele kwenye ngozi inaweza pia kuwa sababu.
Tatizo hili lipoje kwa wanawake?
AKN haipatikani sana kwa wanawake, na wanaume wakiwa na uwezekano wa zaidi ya mara 20 kupata hali hiyo. Hii inaipa nguvu nadharia kuhusu mazoea ya kukata nywele, kwa kuwa wanawake wana uwezo mdogo wa kunyoa nyuma ya shingo. Pia inaimarisha nadharia ya kuwa homoni zinaweza kuchangia katika hali hiyo.
Matibabu kwa dawa za Over the Counter
Makundi haya ya dawa zinaweza kutumika kutibu tatizo hili.
- Antimicrobial cleansers
- Triamcinolone cream
- Topical steroids
- Oral antibiotics
- Oral isotretinoin
Endapo dawa za Over The Counter zikishindwa kufanya kazi, wagonjwa wanaweza kuzingatia matibabu yafuatayo:
- Matibabu ya laser
- Matibabu ya upasuaji
- Radiotherapy
Wakati matibabu ya AKN yanaweza kuwa magumu, kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua ili kupunguza hatari ya dalili zinazoendelea. Ikiwa tayari unasumbuliwa na hali hiyo, mazoea haya ya maisha yanaweza pia kuzuia dalili kuwa mbaya.
- Epuka kunyoa au kukata nywele fupi sana ambavyo inaweza kuharibu nerve follicle.
- Epuka kuvaa mavazi, kofia au helmeti ambazo hutambaa nyuma ya shingo.
- Epuka kutumia bidhaa za nywele kama hairsprays, gels au pomades, ambazo zinaweza kuingilia ukuaji wa nywele.
- Hakikisha shingo yako ni safi na kavu wakati wote
- Kuwa makini wakati wa kusafisha ngozi nyuma ya shingo, kwani kusugua kwa bidii kunaweza kusababisha kuwasha.
MICHANGO YA WADAU
KUWA NA VIPELE BAADA YA KUNYOA NYWELE: CHANZO NA USHAURI
KWANINI TUNATOKEWA NA VIPELE BAADA YA KUNYOA?
Tutajiuliza kwanza swali hili ivi ni kwanin watu kama wazungu waarabu na watu wa asia mara nying hawapati tatizo hili la mapele au vidonda baada ya kunyoa.
Ukichunguza utagundua ya kua sisi nywele zetu ni zenye kuji sokota au kujinyongorota, hivyo unapo nyoa na kukata mzizi wa nywele kabisa una jiweka katika hatar ya kupata mapeli.
SABABU
Bahati mbaya hakuna aliewahi kutufundisha namna ya kunyoa ndo maana utakuta mtu haoshi uso wala kichwa kwa maji ya moto KABLA YA KUNYOA kwa ajili ya kuua bacteria waliopo kwenye uso na kwenye kichwa ambapo mtu huyo akisha nyolewa bacteria hao huingia kwenye matundu hayo ndo maana ukiwachunguza wazee wanao nyoa na viwembe hawana mapele maana wana jisafisha kabla ya kunyoa.
Sasa Matundu hayo yanapo ingia bacteria huziba na pia ukinyoa nywele zote kwenye ngozi kumbuka nywele zetu ni za kujisokota hivyo nywele hujisokotea ndan kwa ndan ( ingrowing ) na huleta muwasho na uvimbe
sasa kwanin wale walio chonga nyuma hupata mapele mwisho wa siku
sababu ni kwamba ukisha nyoa ukapata vidonda ngozi hutoa (collagen) hii ni kwa ajili ya kurepair ngozi iliyo aribika hivyo unapo LINYOA tena lile jeraha unatengeneza hali ya ngozi kuvimbiana na kutengeneza kama uvimbe ( keloid scarring ) wa mfano wa alie katwa na wembe na ngozi yake ikipona hua ni yenye uvimbe maana ngozi hujirepair kama nilivyosema hapo awali
USHAURI
Unapo taka kunyoa ziwe ni nywele za chumban, kikwapan au popote hakikisha una jisafisha kwa maji ya moto kuondoa bacteria na kulainisha ngozi
asubuh unapo nawa uso hakikisha maji hayabaki kwenye kidevu maana nadhan kila mtu anajua mikono yake USIKU hujisika wapi hivyo unapo osha uso hakikisha maji yanatiririka yote chini kuondoa bacteria
Nyoa nywele kwa muelekeo wa nywele zako ili usizikate nywele zote kwan utafanya nywele kuto kutoka kwenye ngozi
Kuna aina ya mafuta husaidia sana kulainisha na kusimamisha nywele unapakaa kabla hujanyoa na baada ya kunyoa ukipakaa huondosha msuguano unao pelekea mzizi wa nywele kunyolewa na pia huondoa mauvimbe tuliyo yaongelea uKihitaji hiyo Dawa Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano MziziMkavu Email barua ya pepe. fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169
USHAURIKuna aina ya mashine hususani hizi za saluni zetu ni butu hivyo zinang'oa nywele badala ya kukata, kwa hiyo ukikata nywele kwa kifaa butu ikang'ooka lile tundu ilipong'oka nywele linakuwa affected na bacteria hatimae ngozi ina react kama hivyo manundu yanakutoka! SASA NINI UFANYE:
1. Tumia kifaa kikali kukata nywele zako, hata kama ni za sehemu za siri, kata kwa kifaa chenye ncha kali sana. Chagua wembe mkali
2. Inaaminika mashine za umeme huleta matokeo mazuri zaidi ya unyoaji hususani zile ambazo nyembe zake zinanolewa vizuri
3. Be selective. Wapi unanyoa je ni hair cutting salon au barber shop au chini ya mwembe kwa wazee wa zungu la unga na vitana
4. Chungua aina ya kemikali unazopaka baada ya kunyoa after shave liquids, lakini pia dawa za nywele kv blackening liquids nk unaweza kuwa allergic na moja ya hizo.
Credit: Kwa alienisimulia ilinisaidia nilisahau kitambo vipele vya ndevu na vya kwenye ncha za kichwani