Hivi vilishawahi nipataga kitambo ila vilipona vyenyewe sikutumia dawa yoyote ile mzee wala usiogopee ni reaction tu hiyo ya damu
Gonjwa HiloHabari zenu wana JF , samahani sana kwa usumbufu kama vile tujuavyo misemo ya wahenga kua mficha uchi azai.
Since mwezi wa nne nasumbuliwa na hili tatizo nimetumia dawa nyingi sana ant fungus kama zote za tube mpk za kopo ila bado tatizo linanisumbua.
Ninawashwa sana mwilini na vijipele vimetokea mkononi na sehemu za siri nimepima hospital kama BURHAN, Legency wanasema siumwi kitu ila hali yangu mimi naona inazidi kua mbaya.
MaJuzi nimepima hospital ya mtaani wakasema na syphilz nimeanza matibabu ya sindano zile nne za mwezi mpk sasa nishachoma sindano 2 ila bado hali iko vile vile tena ndo inazidi kabisa
Mwenye msaada naomba anisaidie nawashwa sana mwiliView attachment 1183912View attachment 1183913View attachment 1183915
Mkuu,,, kama nakuona vile hio dawa ilivyokua inakuunguza p**bu!!! Askwambie mtu bro moto wa ile dawa hauelezeki ,, pole sanaNiliwahi kuupata huu ugonjwa wakati nina 10yrs kuna dawa nilikuwa napaka ya majimaji pamoja na cream ilikuwa inaiunguza balaa utafikiri moto vilikuwa vinawasha hivyo vipele ukijikuna vinaongezeka mwisho vilipona
Ndyo uzur wa JF!Pole Mkuu kwa tatizo linalokusumbua kwa haraka haraka bila kupepesa utakuwa una ugonjwa unaoitwa Genital Herpes infection ambao husababishwa na Herpes simplex virus type 1 & 2 ila kwa upande wako naona ni type 2 ndio inakusumbua, maana nimejaribu kuangalia na hizo blister hapo katika mwili wako zimekaa kama za herpes plus ukijaribu kuvitumbua najua utakuwa unapata maumivu ya ajabu....
Hivyo basi ningependa uende maeneo ya pale sanitas mikocheni wachukue damu ili waweze kufanya analysis ya damu kwa Polymerase chain reaction (PCR) au hata Serological test ili ku confirm ugonjwa husika..
Kuhusu tiba incase ikagundulika una herpes infection wanatibu dalili husika, ila kwa hapo baadae utapata long life immunity amabyo itakuwezesha kutokupata huo ugonjwa tena.
NB: Ugonjwa huu madaktari wengi huhisi ni ugonjwa wa fangus, bacterial au ugonjwa wowote wa njia ya mkojo ambapo huwa ni uwongo...
Hivyo wahi kwenye hiyo hospitali kama wewe ni mkaaji wa dar es salaam uweze pata tiba kila la kheri boss.
Safi sana!Ndio Mkuu, Tahadhari tu angalia usishiriki tendo la ndoa bila kutumia kinga maana uko katika risk kubwa ya kupata magonjwa hatari hasa HIV.
Na Kwa kuongeza hapo kama nilivyokwisha tangulia kusema hapo mwanzo hakuna tiba ya huo ugonjwa kama ikithibitika unao. Hivyo kuna dawa utapewa ni kama zile za ukimwi mfano Ayclovir (zovirax) , famciclovir (famvir) au valacyclovir (Valtrex), hizi dawa zitakusaidia sana maana huwa zinazuia hao vizuri wasiendelee kuzaliana na pia kuepusha wewe kusambaza vizuri hivyo pale utakapokutana kimwili na mwanamke.
Na mara nyingi baada ya kutumia dawa hizi mgonjwa hupata nafuu na kupona kabisa ila ikitokea baada ya kutumia dawa hivyo viupele vikatokea tena basi utaendelea na dawa mpaka pale vitakavyokoma.
Na pia kuhusiana na hivyo vipele ni vyema ukawa unaosha kwa kusugua na maji ya uvuguuvugu yakiwa na chumvi ndani yake kipimo ni chukua kijiko cha chai weka chumvi nusu changanya na maji nusu lita sugua kwa kuosha na kwa maumivu amadogo madogo unaweza tumia dawa kama aspirin au acetaminophen utakuwa sawa mkuu..