Vipaumbele vya bajeti mwaka wa fedha 2017/2018 vitabadilisha maisha ya Watanzania?

Wa ndugu naleta kwenu vipaumbele vya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 ambavyo vimetajwa na waziri wa fedha. Vipaumbele hivyo ni.
1.Ujenzi wa Reli
2.Kuhuisha ATCL
3.Ununuzi wa ndege
4.Mradi wa Liganga
5.Kuhamia Dodoma
6.Kuanzisha kanda maalumu za kiuchumi.
Je kwa vipaumbele hivi maisha ya mtanzania yatabadilika ukilinganisha na hali ilivyo sasa??!
Mkuu kwa uelewa wangu, kazi ya serikali ni kujenga mazingira mazuri mfano miundo mbinu, miradi ya kilimo, sera mbalimbali nk na kinachofuata ni mtu mmoja mmoja kutumia hizo fursa kujiletea maendeleo. Mfano, ndege zitaleta wageni, Liganga italeta wawekezaji, ajira nk ujenzi wa reli utarahisisha usafirishaji kwa bei nafuu, cement ambayo inauzwa kigoma mf 20,000 ikiletwa na kwa reli cement hiyohiyo usishangae ikauzwa kwa sh 15,000/= Maana yake ni nini ? ni kuwa kwa kutumia fursa hizi na ww upambane ujikwamue, ujenge nyumba nzuri, upate tiba na madawa, usafirishe mazao yako toka huko kijijini kwenda mjini, hayo ndio maendeleo, au nikuulize ww unadhani unapoambiwa maisha yatabadilika unategemea kuona mabadiliko gani ?
 
Mkuu kwa uelewa wangu, kazi ya serikali ni kujenga mazingira mazuri mfano miundo mbinu, miradi ya kilimo, sera mbalimbali nk na kinachofuata ni mtu mmoja mmoja kutumia hizo fursa kujiletea maendeleo. Mfano, ndege zitaleta wageni, Liganga italeta wawekezaji, ajira nk ujenzi wa reli utarahisisha usafirishaji kwa bei nafuu, cement ambayo inauzwa kigoma mf 20,000 ikiletwa na kwa reli cement hiyohiyo usishangae ikauzwa kwa sh 15,000/= Maana yake ni nini ? ni kuwa kwa kutumia fursa hizi na ww upambane ujikwamue, ujenge nyumba nzuri, upate tiba na madawa, usafirishe mazao yako toka huko kijijini kwenda mjini, hayo ndio maendeleo, au nikuulize ww unadhani unapoambiwa maisha yatabadilika unategemea kuona mabadiliko gani ?


Usitake kusema kwamba Afya, na upatikanaji wa maji safi na salama ni jukumu la mwananchi kujitafutia baada ya reli kujengwa na ndege kuletwa.

Hili swala la Afya na Maji safi nchini ni kilio cha muda mrefu sana, na ni jukumu linaloihusu serikali moja kwa moja, hana la kukwepa juu ya hili.
 
ni kweli ukilitazama moja kwa moja hauwezi kuona kama ndege zinamsaidia maskini lakini zinamsaada mkubwa sana kwake kwa njia moja au nyingine na hasa tukiangalia huko nyuma sekta ya usafiri ilikuwa inaongoza kwa uchangiaji mkubwa kwa pato la taifa.
wakati mwingine kuna vitu tunavihitaji si kwa sababu vinaumuhimu sana kwetu lakini kwa kuwa muda umefika kuwa navyo. mfano mtu wa kawaida kabisa wa kijijini haitajisana simu ya mpanguso ukilinganisha na mahitaji yake lakini ikizingatiwa hana umeme na muda wa kutumia simu kwa muda mrefu.
hivyo wacha tuwe nazo zinaweza kuchangia kukuza hata utalii siku zijazo
 
Vipi
Elimu & Afya
Au mnafikiri watu wakiwa fa fa fa fa fa vichwani na wagonjwa tutafikia malengo yetu
 
Afya out
Elimu out
Kilimo out
Watumishi out
Awamu hii tutalimia meno hakyanani.

Sijui kama serikali hii inaamini katika maendeleo ni watu (afya zao, elimu, ajira n.k) naona wamewekeza zaidi katika vitu (tunajenga hiki, tunanunua kile n.k).
 
Hakuna kitu hapo serikali inachumia tumbo tu mfano unafamilia kazi unayofanya kwa siku unaingiza elfu tano hela unayoiacha nyumbani kwajili ya chakula na matumizi mengine elfu tano tena inazidi hela ya maendeleo unategemea ukope ndiyo ufanye maendeleo tena kwa riba kubwa na hapo hapo unamadeni kibao mikakati ya kujikwamua haieleweki ni sawa na hakuna kunamaendeleo kweli hapo?
 
Mkuu kwa uelewa wangu, kazi ya serikali ni kujenga mazingira mazuri mfano miundo mbinu, miradi ya kilimo, sera mbalimbali nk na kinachofuata ni mtu mmoja mmoja kutumia hizo fursa kujiletea maendeleo. Mfano, ndege zitaleta wageni, Liganga italeta wawekezaji, ajira nk ujenzi wa reli utarahisisha usafirishaji kwa bei nafuu, cement ambayo inauzwa kigoma mf 20,000 ikiletwa na kwa reli cement hiyohiyo usishangae ikauzwa kwa sh 15,000/= Maana yake ni nini ? ni kuwa kwa kutumia fursa hizi na ww upambane ujikwamue, ujenge nyumba nzuri, upate tiba na madawa, usafirishe mazao yako toka huko kijijini kwenda mjini, hayo ndio maendeleo, au nikuulize ww unadhani unapoambiwa maisha yatabadilika unategemea kuona mabadiliko gani ?

Uko sawa na sahihi kwa upande huo, lakini napata mashaka pale unaposema ndege ZITALETA WAGENI, Liganga ITALETA WAWEKEZAJI. Sio kwamba sipendi wageni na wawekezaji, la hasha! Ila je, ni lini tutainua uwezo wa wananchi wetu kumiliki uchumi, tunainuaje wazawa kuwa ndio wawekezaji ? Tunajengaje mazingira ya watu wetu wengi waweze kupanda hizo ndege ?. Ni lazima tuinue hali zao, serikali inalazimika kuendeleza watu wake.

Ifikie wakati sasa serikali ifanye mambo in proportion, kuwepo na balance kati ya maendeleo ya vitu (kununua ndege, kujenga reli, barabara, bandari, fly overs na miundombinu mingine) na maendeleo ya watu (afya, elimu hasa mikopo, ajira, kuwajengea wananchi uwezo kiuchumi na mengineyo) ili hali ya wananchi iende sanjari na uhalisia wa maendeleo ya nchi. Naona kama serikali hii imesahau sana maendeleo ya watu. Tunajenga tu, hebu ona hivyo vipaumbele hapo.
 
Mkuu kwa uelewa wangu, kazi ya serikali ni kujenga mazingira mazuri mfano miundo mbinu, miradi ya kilimo, sera mbalimbali nk na kinachofuata ni mtu mmoja mmoja kutumia hizo fursa kujiletea maendeleo. Mfano, ndege zitaleta wageni, Liganga italeta wawekezaji, ajira nk ujenzi wa reli utarahisisha usafirishaji kwa bei nafuu, cement ambayo inauzwa kigoma mf 20,000 ikiletwa na kwa reli cement hiyohiyo usishangae ikauzwa kwa sh 15,000/= Maana yake ni nini ? ni kuwa kwa kutumia fursa hizi na ww upambane ujikwamue, ujenge nyumba nzuri, upate tiba na madawa, usafirishe mazao yako toka huko kijijini kwenda mjini, hayo ndio maendeleo, au nikuulize ww unadhani unapoambiwa maisha yatabadilika unategemea kuona mabadiliko gani ?

Kwa akili hz za kibashite nchi haiwezi kusonga.
 
Wa ndugu naleta kwenu vipaumbele vya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 ambavyo vimetajwa na waziri wa fedha. Vipaumbele hivyo ni.
1.Ujenzi wa Reli
2.Kuhuisha ATCL
3.Ununuzi wa ndege
4.Mradi wa Liganga
5.Kuhamia Dodoma
6.Kuanzisha kanda maalumu za kiuchumi.
Je kwa vipaumbele hivi maisha ya mtanzania yatabadilika ukilinganisha na hali ilivyo sasa??!


mambo hayo yote mbona ni discretionary?

nadhani mambo ya afya na hifadhi ya jamii ni mambo ya msingi sana katika bajeti.
 
Ooohhhh kilimo kwanza!!!!! Ohhh kiliiiimmmmoooo kwanza, kili kili kili mooo kwanzaaaaaa!!!!!

Asilimia 80% ya watanzania ni WAKULIMA
Chakula cha watanzania kinategemea WAKULIMA
Wanaoipigia CCM kura kwa wingi ni WAKULIMA
Kipimo cha maisha bora kwa watanzania kinategemea kipato cha WAKULIMA
Lakini katika vipao mbele vya bajeti waliopuuzwa ni WAKULIMA

Ohhhh WAKULIMA, ohh WAKULIMA tumemkosea nini Mungu WAKULIMA?

Haya sasa Hamorapa mistari hiyo, kazi kwako kuimba. Basata watakukamata lakini mkuu atakutoa.
 
Kulalamika imekuwa Tabia ya watanzania
kila kitakacho fanywa lazima watu wa lalamike.
Lakini Hakuna namnw
tumeamua Tanzania iende itaenda
huo mradi wa Liganga utaisaidia nchi kwenye uchumi sehemu kubwasana
Ununuzi wa ndege ni kwa lengo la Kuongeza watalii nchi
hili pia litakuza uchumi pia
Sioni jambo la kupinga hapo,
zaidi tunapaswa kutoa ushauri
jinsi gani Vipaumbele hivyo vita tekelezwa.
 
nilidhani kwa vile serikali haija ajiri kwa miaka 2 sasa, basi kuajiri na kupanua wigo wa ajira serikalini ingekuwa kipaumbele? Yani huku Mbeya tunanunua sukari 3000/= kweli kabisa!!!!
 
Back
Top Bottom