MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,975
Kama tukikubaliana na hoja ya ''kununuliwa'' ambapo viongozi wote wa Juu wa Balaza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) wanaweza ''kununuliwa'' basi kuna tatizo kubwa nala msingi ndani ya chama ambacho kwa sasa kingekuwa ni chama kilichokabidhiwa mali za Taifa zima wazilinde na kuziendeleza kama chama tawala!
Hawa sio viongozi ambao wameanza uongozi mwaka huu bali kuna wengine wamekuwa wabunge na Mawaziri vivuli katika Wizara mbali mbali kwa zaidi ya miaka 10. Kwa lugha nyingine kwa sasa wangekuwa ni Mawaziri katika serikali ya CHADEMA.
Kwa vyovyote vile utakavyoweka lakini huwezi kupuuza ukweli kuwa hawa viongozi ni wajumbe wa kikao muhimu na cha juu cha CHADEMA(Kamati Kuu) ambacho kinapanga mikakati ya kisiasa lakini pia ni viongozi waliokuwa wanaaminiwa sana ndani na nje ya chama mpaka wengine wakaitwa ''Iron Lady'' kutokana na misimamo yao ''isiyoyumba''.
Zamani tulikuwa tunaona kiongozi mmoja au wawili ndani ya CHADEMA wakituhumiwa ''kununuliwa/kusaliti'' lakini hili la uongozi wote wa jumuiya ''kununuliwa/kusaliti'' limevunja rekodi. Hii inatupa ujumbe kuwa kila kiongozi ndani ya CHADEMA ana bei na ukitaka ''kumnunua'' unamnunua!
Hili tukio limetoa maswali mengi kuhusu uaminifu wa viongozi wa CHADEMA sio ndani ya chadema peke yake bali kwa taifa.
Kama tukikubali hoja ya kuwa ''hawajanunuliwa'' bali wamefanya tu kinyume na maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu. Hili nalo pia lina uweka uongozi wa juu wa CHADEMA katika maswali mengi kuhusu suala zima la uongozi ndani ya chama.
Huwezi kuwa na wajumbe wa Kamati Kuu wazoefu zaidi ya watano wanafanya maamuzi makubwa kama haya bila ''ruhusa'' ya Kamati Kuu.
Hawa sio kwamba wameibuka tu siku moja na kumaliza kila kitu. Ni lazima Kamati Kuu yote ilikuwa inajua kinachoendelea lakini inawezekana baadhi ya wajumbe hawakujua kilichokuwa kinaendelea kwa undani zaidi.
Hoja za msingi;
Je, Mwenyekiti wa Taifa alijua kinachoendelea na kama alijua alichukua hatua gani kabla ya tukio halijafikia lilipofikia?
Je, ofisi ya Mtendaji Mkuu wa chama(Katibu Mkuu) ilijua kinachoendelea na kama ilijua ilichukua uamuzi gani?
Kama ofisi za Mwenyekiti wa Taifa na Katibu wa Taifa hawakujua kinachoendelea basi viongozi wake watakuwa hawajui kazi zao kitu ambacho naamini sivyo kutokana na uzoefu wao kisiasa nchini.
Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa uongozi wote wa Juu wa Balaza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) ndio ulioapishwa kuwa wabunge wa viti maalum ''bila ridhaa'' ya vikao vya CHADEMA.
Viongozi wa BAWACHA kitaifa wanaotuhumiwa ambao wameapishwa kuwa wabunge wa viti maalum ni hawa:-
1) Mwenyekiti wa BAWACHA - Halima Mdee.
2) Makamu Mwenyekiti wa BAWACHA - Hawa Subira Mwaifunga
3) Katibu Mkuu wa BAWACHA - Grace Tendega
4) Naibu Katibu Mkuu BAWACHA (Bara) - Jesca Kishoa
5) Naibu Katibu Mkuu BAWACHA (Zanzibar) - Asia Mwadin Mohamed.
6) Katibu Mwenezi BAWACHA - Agnesta Lambat Kaiza
Hata Balaza la vijana (BAVICHA) nalo halikukosa kiongozi katika kundi hilo, Katibu wake Mkuu wa BAVICHA, Nusrat Hanje pia aliapishwa.
Hawa ni wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wanaoingia kwenye vikao kwa sababu ya vyeo vyao.
Wamo pia wengine katika kundi hilo la Ujumbe wa Kamati Kuu ambao waliapishwa;
1) Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Serengeti na Mjumbe wa Kamati Kuu - Esther Matiko
2) Ester Bulaya
Wamo pia viongozi wa mikoa ikiwamo:-
1) Mwenyekiti wa Chadema Mkoani Mtwara - Tunza Malapo.
Hawa sio viongozi ambao wameanza uongozi mwaka huu bali kuna wengine wamekuwa wabunge na Mawaziri vivuli katika Wizara mbali mbali kwa zaidi ya miaka 10. Kwa lugha nyingine kwa sasa wangekuwa ni Mawaziri katika serikali ya CHADEMA.
Kwa vyovyote vile utakavyoweka lakini huwezi kupuuza ukweli kuwa hawa viongozi ni wajumbe wa kikao muhimu na cha juu cha CHADEMA(Kamati Kuu) ambacho kinapanga mikakati ya kisiasa lakini pia ni viongozi waliokuwa wanaaminiwa sana ndani na nje ya chama mpaka wengine wakaitwa ''Iron Lady'' kutokana na misimamo yao ''isiyoyumba''.
Zamani tulikuwa tunaona kiongozi mmoja au wawili ndani ya CHADEMA wakituhumiwa ''kununuliwa/kusaliti'' lakini hili la uongozi wote wa jumuiya ''kununuliwa/kusaliti'' limevunja rekodi. Hii inatupa ujumbe kuwa kila kiongozi ndani ya CHADEMA ana bei na ukitaka ''kumnunua'' unamnunua!
Hili tukio limetoa maswali mengi kuhusu uaminifu wa viongozi wa CHADEMA sio ndani ya chadema peke yake bali kwa taifa.
Kama tukikubali hoja ya kuwa ''hawajanunuliwa'' bali wamefanya tu kinyume na maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu. Hili nalo pia lina uweka uongozi wa juu wa CHADEMA katika maswali mengi kuhusu suala zima la uongozi ndani ya chama.
Huwezi kuwa na wajumbe wa Kamati Kuu wazoefu zaidi ya watano wanafanya maamuzi makubwa kama haya bila ''ruhusa'' ya Kamati Kuu.
Hawa sio kwamba wameibuka tu siku moja na kumaliza kila kitu. Ni lazima Kamati Kuu yote ilikuwa inajua kinachoendelea lakini inawezekana baadhi ya wajumbe hawakujua kilichokuwa kinaendelea kwa undani zaidi.
Hoja za msingi;
Je, Mwenyekiti wa Taifa alijua kinachoendelea na kama alijua alichukua hatua gani kabla ya tukio halijafikia lilipofikia?
Je, ofisi ya Mtendaji Mkuu wa chama(Katibu Mkuu) ilijua kinachoendelea na kama ilijua ilichukua uamuzi gani?
Kama ofisi za Mwenyekiti wa Taifa na Katibu wa Taifa hawakujua kinachoendelea basi viongozi wake watakuwa hawajui kazi zao kitu ambacho naamini sivyo kutokana na uzoefu wao kisiasa nchini.
Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa uongozi wote wa Juu wa Balaza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) ndio ulioapishwa kuwa wabunge wa viti maalum ''bila ridhaa'' ya vikao vya CHADEMA.
Viongozi wa BAWACHA kitaifa wanaotuhumiwa ambao wameapishwa kuwa wabunge wa viti maalum ni hawa:-
1) Mwenyekiti wa BAWACHA - Halima Mdee.
2) Makamu Mwenyekiti wa BAWACHA - Hawa Subira Mwaifunga
3) Katibu Mkuu wa BAWACHA - Grace Tendega
4) Naibu Katibu Mkuu BAWACHA (Bara) - Jesca Kishoa
5) Naibu Katibu Mkuu BAWACHA (Zanzibar) - Asia Mwadin Mohamed.
6) Katibu Mwenezi BAWACHA - Agnesta Lambat Kaiza
Hata Balaza la vijana (BAVICHA) nalo halikukosa kiongozi katika kundi hilo, Katibu wake Mkuu wa BAVICHA, Nusrat Hanje pia aliapishwa.
Hawa ni wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wanaoingia kwenye vikao kwa sababu ya vyeo vyao.
Wamo pia wengine katika kundi hilo la Ujumbe wa Kamati Kuu ambao waliapishwa;
1) Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Serengeti na Mjumbe wa Kamati Kuu - Esther Matiko
2) Ester Bulaya
Wamo pia viongozi wa mikoa ikiwamo:-
1) Mwenyekiti wa Chadema Mkoani Mtwara - Tunza Malapo.