MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Jana Tarehe 18/09/2020 Mgombea wetu wa Urais Tundu Lissu alikuwa na ratiba ya kufanya Kampeni katika Mkoa wetu wa Katavi maeneo ya Majimoto katika jimbo la Kavuu Wilaya ya Mlele na Mpanda MJINI katika jimbo la Mpanda.
Hakika viongozi wetu (Musa Masanja Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Magharibi , Roda KUMCHELA Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Katavi, SEFU NTIJE, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mlele na GELARD PESAMBILI Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Mlele) walichomfanyia Lissu na sisi wanachama na wapenzi wa CHADEMA kwa ujumla hakikubaliki na kamwe hatuna imani tena na viongozi hawa.
Wananchi tuliokusanyika katika viwanja vya Mkuyuni Majimoto kuanzia saa mbili asubuhi tulisikitishwa sana majira ya saa 10:20 jioni kutangaziwa kuwa LISSU hatafika kwa sababu ambazo hazieleweki mara eti Mawasiliano na msafara wake hayapatikani mara msafara umepotea.
Baada ya kufuatilia sababu za LISSU kutofika Majimoto tulibaini kuwa Msafara wa LISSU ulipotea njia panda ya KIZI mpakani mwa Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa na Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi. Kwamba badala ya msafara wa LISSU kufuata Barabara ya Kibaoni Majimoto , ukafuata Barabara ya Sitalike kwenda Mpanda.
Tunajua kuwa LISSU alifanya mikutano CHALA na KIRANDO Wilayani Nkasi kabla hajaja Majimoto. Maswali tunayowauliza viongozi wetu ni:-
1. Walijua Msafara wa LISSU unajua Barabara ya kwenda Majimoto?
2. Kama msafara wa LISSU ulikuwa haujui njia kwanini viongozi wote wanaojua njia kuanzia Kanda, Mkoa na Wilaya Walitangulia Majimoto na kukimbilia kufanya Starehe GWAMBINA LOUNGE? Tunajua pesa zilizokuwa zikichangishwa kwenye mkutano wakipelekewa viongozi GWAMBINA kwa ajili ya kunywa bia.
3. Kama waliona ugumu kuusubiri msafara wa LISSU kwanini hawakuwaweka Vijana njia panda ya KIZI ili wauongoze msafara huo kuelekea majimoto?
Tukumbuke kuwa ni Viongozi hawahawa kupitia Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Mlele walitaka kutuaminisha kuwa kuna kundi lineandaliwa kwa ajili ya kuanzisha vurugu wakati wa Mkutano, kumbe walikuwa na mambo yao ikiwa ni pamoja na kujengea hofu Mhe. LISSU ili asifike kuongea na wana Majimoto ilimradi tu wagawane pesa zilizoandaliwa Kwa ajili ya Mkutano huo zikiwemo zile zilizochangishwa kutoka kwa Wananchi Mkutanoni hapo
Kwa Ujumla tukio hili limewakatisha tamaa Wananchi wa Majimoto na Mkoa wa Katavi kwa ujumla. kwani wanamuona LISSU na CHADEMA kwa ujumla ni wasanii na waongo.
Hakika viongozi wetu (Musa Masanja Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Magharibi , Roda KUMCHELA Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Katavi, SEFU NTIJE, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mlele na GELARD PESAMBILI Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Mlele) walichomfanyia Lissu na sisi wanachama na wapenzi wa CHADEMA kwa ujumla hakikubaliki na kamwe hatuna imani tena na viongozi hawa.
Wananchi tuliokusanyika katika viwanja vya Mkuyuni Majimoto kuanzia saa mbili asubuhi tulisikitishwa sana majira ya saa 10:20 jioni kutangaziwa kuwa LISSU hatafika kwa sababu ambazo hazieleweki mara eti Mawasiliano na msafara wake hayapatikani mara msafara umepotea.
Baada ya kufuatilia sababu za LISSU kutofika Majimoto tulibaini kuwa Msafara wa LISSU ulipotea njia panda ya KIZI mpakani mwa Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa na Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi. Kwamba badala ya msafara wa LISSU kufuata Barabara ya Kibaoni Majimoto , ukafuata Barabara ya Sitalike kwenda Mpanda.
Tunajua kuwa LISSU alifanya mikutano CHALA na KIRANDO Wilayani Nkasi kabla hajaja Majimoto. Maswali tunayowauliza viongozi wetu ni:-
1. Walijua Msafara wa LISSU unajua Barabara ya kwenda Majimoto?
2. Kama msafara wa LISSU ulikuwa haujui njia kwanini viongozi wote wanaojua njia kuanzia Kanda, Mkoa na Wilaya Walitangulia Majimoto na kukimbilia kufanya Starehe GWAMBINA LOUNGE? Tunajua pesa zilizokuwa zikichangishwa kwenye mkutano wakipelekewa viongozi GWAMBINA kwa ajili ya kunywa bia.
3. Kama waliona ugumu kuusubiri msafara wa LISSU kwanini hawakuwaweka Vijana njia panda ya KIZI ili wauongoze msafara huo kuelekea majimoto?
Tukumbuke kuwa ni Viongozi hawahawa kupitia Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Mlele walitaka kutuaminisha kuwa kuna kundi lineandaliwa kwa ajili ya kuanzisha vurugu wakati wa Mkutano, kumbe walikuwa na mambo yao ikiwa ni pamoja na kujengea hofu Mhe. LISSU ili asifike kuongea na wana Majimoto ilimradi tu wagawane pesa zilizoandaliwa Kwa ajili ya Mkutano huo zikiwemo zile zilizochangishwa kutoka kwa Wananchi Mkutanoni hapo
Kwa Ujumla tukio hili limewakatisha tamaa Wananchi wa Majimoto na Mkoa wa Katavi kwa ujumla. kwani wanamuona LISSU na CHADEMA kwa ujumla ni wasanii na waongo.