Viongozi wawe mfano wa kupendabidhaa za ndani

Mtazamaji

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
5,937
1,437
  • Je ni wabunge wagapi wanavaa suti Made in or by Tanzaniam?
  • Je ni ni Viongozi wangapi wapo tayari kutengenezesha viatu vipya japo pair mbili kwa mkwa kwa mafudi wetu
  • Je ni viongozi wangapi majumbani kwao wanasisitiza wapatiwe maziwa fresh ya tanzania na sio ya Unga kutoka nje au ya packet kutoka zimbabwe na SA
  • Je ni viongozi wangapi asilimia kubwa ya mahitaji ya ndani ya familia zao wanayapata kutoka local market
Tusisingize ubora ,ubora utakuja baada ya wahusika kuonyesha uzalendo. Na wasomi wengine wajaribu kusppory bidhaa za ndani.

Lets play our part katika Kukukuza na kutenegza ajira,uchumi, wa mtaa, kitongoji jimbo, mkoa na nchi

Nawasilisha
 
Ofisi zote zimejaa fanicha mbovu za unga unga wa randa uliogundishwa. Tanzania tuna kila aina ya mbao imara ajabu, tuna vyuo vinavyofundisha vijana ufundi mbalimbali, lakini serikali inafuta ajira za hawa vijana kwa kukosa kazi ya kufanya baada ya soko kujazwa fanicha mbovu, ambazo hubadilishwa kila mwaka kwa gharama kubwa.
 
Umemsikia Nchimbi katoa amri lipatikane vazi la taifa ndani ya miezi sita, huku yeye kavaa suti.

Unaagiza vazi la taifa kama vile unaagiza machungwa.
 
Ofisi zote zimejaa fanicha mbovu za unga unga wa randa uliogundishwa. Tanzania tuna kila aina ya mbao imara ajabu, tuna vyuo vinavyofundisha vijana ufundi mbalimbali, lakini serikali inafuta ajira za hawa vijana kwa kukosa kazi ya kufanya baada ya soko kujazwa fanicha mbovu, ambazo hubadilishwa kila mwaka kwa gharama kubwa.

We angalia Muheshimiwa sita mkoa wake tabora una mbao imara za miti migumu. Lakini furnitre za ofisi ya mbunge wa jimbo la urambo ameagiza kutoka dar es-es-salaaam na Dar tumegiza kutoka china. Hata viti vya wageni ameshindwa kutoa tender kwa kiwanda kidogo au seremala wa Urambo au tabora. Wakiwa bungeni wanahubiri wanachi tununue bidhaa za ndani.



Umemsikia Nchimbi katoa amri lipatikane vazi la taifa ndani ya miezi sita, huku yeye kavaa suti.

Unaagiza vazi la taifa kama vile unaagiza machungwa.

Hahahahah hawa wanasiasa

Huwa najiuliza ni ajira ngapi zitatengenzwa kama bunge lingeweka japo ijumaa iwe siku ya wabunge kuvaa vazi lililobuniwa nchini. May be wanaume wkavaa mashati hata ya vitenge. etc.

Dress code ya suit kwa manufaa ya mtaliano au au mtanzania??? Mandela aliwai kuonyesha mfano nadhani vazi alilokuwa anapenda kuvaa lilitengeza ajira nyingi sana. Vazi lile lilikuwepo lakini kwa kuvaliwa naye mara kwa mara..........
 
Back
Top Bottom