abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=2]Friday, November 30, 2012[/h][h=3][/h]
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd. Kushoto ni Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba.
Sheikh Abdallah Issa (kushoto), akiongoza dua ya kumuombea marehemu bibi Kisa Mohd nyumbani kwake Mikocheni Dar es Salaam.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali katika Makaburi ya Kisutu aliposhiriki mazishi ya bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiweka mchanga katika kaburi la marehemu bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd aliyezikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam. (Picha na Salmin Said, OMKR)
Na Hasssan Hamad OMKR
Viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali wameshiriki katika mazishi ya bibi Kisa Mohd ambaye ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
Mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya kisutu, yaliongozwa na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa UDP John Cheyo, Mwenyekiti wa ADC bw. Said Miraji na Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda.
Mwili wa marehemu huyo ulisaliwa katika msikiti Maamur ulioko maeneo ya Upanga na baadaye kupelekwa katika makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi.
Marehemu bibi Kisa Mohd alifariki Jumanne iliyopita baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Presha kwa muda mrefu, na kuzikwa Alkhamis tarehe 29/11/2012.
Akizungumza katika mazishi hayo, msemaji wa familia hiyo amewashukuru viongozi na wananchi waliojitokeza kushirikiana nao katika msiba huo, na kwamba familia imepoteza mtu muhimu ambaye pengo lake haliwezi kuzibika kwa kipindi kifupi.
Imewekwa na MAPARA at 9:19 AM
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd. Kushoto ni Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba.
Sheikh Abdallah Issa (kushoto), akiongoza dua ya kumuombea marehemu bibi Kisa Mohd nyumbani kwake Mikocheni Dar es Salaam.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali katika Makaburi ya Kisutu aliposhiriki mazishi ya bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiweka mchanga katika kaburi la marehemu bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd aliyezikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam. (Picha na Salmin Said, OMKR)
Na Hasssan Hamad OMKR
Viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali wameshiriki katika mazishi ya bibi Kisa Mohd ambaye ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
Mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya kisutu, yaliongozwa na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa UDP John Cheyo, Mwenyekiti wa ADC bw. Said Miraji na Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda.
Mwili wa marehemu huyo ulisaliwa katika msikiti Maamur ulioko maeneo ya Upanga na baadaye kupelekwa katika makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi.
Marehemu bibi Kisa Mohd alifariki Jumanne iliyopita baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Presha kwa muda mrefu, na kuzikwa Alkhamis tarehe 29/11/2012.
Akizungumza katika mazishi hayo, msemaji wa familia hiyo amewashukuru viongozi na wananchi waliojitokeza kushirikiana nao katika msiba huo, na kwamba familia imepoteza mtu muhimu ambaye pengo lake haliwezi kuzibika kwa kipindi kifupi.
Imewekwa na MAPARA at 9:19 AM