Viongozi wapya wa CHADEMA 2014-2019

Mbona na wote ni wakristo mkuu? Hawa ni viongozi wa siasa au wa kanisa?[/QUOT

Kasurumbayi,Mtoi na safari hawa si wakristo,then ndani ya CDM tunaangalia perfomance na dini wala kabila la mtu,kma ingekuwa hivyo leo CDM nzima ingekuwa imejaza waislamu ili kumaliza propaganda za udini za MACCM
 
Hapo kwenye uongozi wa Bavicha amepatia sana mwandishi huyu,ukitaja jina la Jesca Kishoa tu,Migulu roho inataka kumchomoka
 
Hahah ....
Eti Profesa Safari awe Mwenyekiti wa CDM Zanzibar....

Tatizo wakiristo (CHADEMA) wanafikiri Kila Muislamu ni Mza-Zanzibari
 
Mbona na wote ni wakristo mkuu? Hawa ni viongozi wa siasa au wa kanisa?

Wewe akili yako imejaa matope.....kwani haujaona majina ya kiislamu huku? halafu Profesa baregu dini yake ni ipi? kama ni mkristo mbona aliapa kwa kuweka mikono yake kifuani badala ya kushika biblia kipindi anateuliwa kuwa mjumbe wa tume ya katiba? Utawashwa sana mwaka huu. Mimi nadhani jamaa kaandika ya kwake na chama kitachagua wahusika.
 
mbona umemsahau Ben Saanane? na kazi yooote anayofanya kumbe hana dhaman?
 
Mbona na mie simo sasa we uliandika ni msaliti nasema ni MSALITIIIIIIIIIIIIIIIIIIIJ lazima tukuondoee harakaa
 
Mungu wangu mbona Yericko nyerere haumo na ya G minja duuu
Ndio mkome kuongelea taasis za watuu
 
Haki ya nani, mleta uzi naye anaungana na waraka wa mabadiliko wa akina MM, M1,M2 na M3. Mnawapinga wa kina ZZK lakini kimoyoni mnataka mabadiliko. Haya sasa Ngoja LEMA aje na Tofali lake utakoma.....Mchg Msigwa umemtupilia mbali, Tundu Lissu naye hayupo...........weeeeeeeeeee hawatakubali.
 
Mbona post yote umeipigia mistari. Mimi sijaisoma kwa kuwa inaumiza macho sana. Sijui umeandika nini, nakutakia kila lakheiri katika hayo uliyoandika

Hii nimeitoa kwenye facebook ya kamanda wetu mtajwa hapo chini,tusome

Mtazamo wangu
huku makamanda wa CDM tukiwa tunaelekea kwenye chaguzi mbalimbali za ndani ya chama napenda kutoa mtazamo wangu juu ya nani anafaa wapi na kwa nafasi gani.
1: Dr. Willibrord Slaa,mwenyekiti wa chama hii ni kutokana ni ukweli kwamba dk Slaa bado anafaa kugombea nafasi nyeti ya urais waJMHT hapo mwaka 2015,hivyo anahitaji kupumzika kutoka kwenye shughuli ngumu ya ukatibu mkuu,ambayo kimsingi ni nafasi ya kiutendaji zaidi,hivyo inahitaji mtu ambaye anaweza kuzunguka zaidi maeneo mbalimbali nchini na kuimarisha chama nafasi hiyo inafaa kuchukuliwa na kijana,na dk akabakia kama msimamizi mkuu wa mambo ya chama,then hii italeta heshima zaidi na itaendana na mtazamo wa jamii na vyama vya siasa kwamba mwenyekiti wa chama ndiye mala nyingi huchaguliwa kupeperusha bendera ya chama kwa nafasi ya urais,angalia mfano huu,ndani ya CCM mwenyekiti ndiye huwa rais ama mgombea urais,vilevile CUF na baadhi ya vyama,pia kuwa mwenye kiti itamsaidia katika kupunguza maadui wa ndani na nje ya chama,kwa mfano kwa nafasi yake ya sasa kma mtendaji mkuu wa chama ndiye husimamia maamuzi ya vikao vyote na kuhakikisha yanatekelezwa,mfano sakata la Zitto Kabwe,Mtela MwampambaJuliana Shonza Chagulani AdamsHabib Mchange na wengine ambao walichukuliwa hatua mbalimbali na chama wamekuwa ama wao wenyewe ama wafuasi wao wamekuwa wakimnyoshea kidole na hata wengine kumtukana kwa madai kwamba yeye ndo amesababisha wafukuzwa ama wasimamishwe,hii inamwongezea maadui wanaomshambulia kila mahala misri ya mbwa mwitu,na hata kwa nafasi yake ya ukatibu mkuu inawapa wapinzani wetu kutoka CCM kumwandama sana mitandaoni na huko mitaani wakiamni yeye ndo sababu ya CCM kuchukiwa,akiwa mwenyekiti itapunguza msuguano huu.
2:profesa Baregu,makamu mwenyekiti,huyu kwangu mimi amekuwa mwanasiasa anayefanya siasa za taratibu na zisizo sukumwa na hisia(emotion)akiwa makamu mwenyekiti kwa kusaidiana na mwenyekiti wake dk Slaa,watakiinua sana chama kutokana na busara zao pevu na wavumilivu,huyu pia atakuwa nguzo ya kuongeza wasomi zaidi wa kada yake.
3:John Mnyika,huyu anafaa kuwa katibu mkuu wa chama chetu,hii inatokana na kuwa anakubalika zaidi miongoni mwa vijana wa CDM mbali na Zitto Zuberi Kabwe,anachomshinda Zitto yeye hana makundi mengi ya wazi ama ya siri ndani na nje ya chama kama vijana wengine,hii itakisaidia chama kwa kuwaonganisha vijana na kuwaongoza katika kuikomboa nchi hii kutoka kwa CCM "(black colonialist)pia Mnyika amekuwa mfano bora miongoni mwa wabunge vijana nchini kwa kuibua hoja mbalimbali bungeni na zinafika mwisho,pia kwa nafasi yake ya kiongozi wa kurugenzi ya habari na uenezi ya chama ameitendea haki sana nafasi yake kabla na baada ya kuwa mbunge,wamekuwa imara kukisemea chama na kujibu mambo mbalimbali kwa haraka na kutoa majibu mujarabu kwenye hoja husika,pia kutokana na umri wake ana nafasi kubwa ya kukitumikia chama zaidi ,hivyo akiwa katibu mkuu wa chama atakipeleka chama mbele zaidi.
4:Kasulumbayi (mbunge)huyu ameweza sana wakati wa kampeni za Igunga japo tulichakachuliwa,na amekuwa na ushawishi sana kanda ya ziwa zaidi ana misimamo thabiti na isiyoyumba wala kutekeleka,huyu atakuwa kete nzuri sana kwa watu wa rika la kati na hivyo kuongeza viti na kura nyingi kanda ya ziwa.
5:Mohamedi Mtoi,huyu ataweza sana kuvaa viatu vya Mnyika kuuongoza kurugenzi ya Habari na uenezi ya chama mbali ameibuka juzijuzi ndani ya siasa za CDM bt ameonesha kuweza sana kukitetea chama hivyo akiaminiwa na chama na kupewa nafasi anaweza sana.
6:pastrobasi Pascal,mwenyekiti wa BAVICHA taifa,huyu jamaa ni graduate wa LLM SAUT na pia amewahi kuongoza tawi la CDM SAUT hapo kwa mafanikio kipindi chake cha uongozi,pia amekuwa na ushawishi kisiasa kanda ya ziwa hasa kwa vijana,huyu jamaa anaweza sana kumpokea kamanda John Heche kijiti hicho,jamaa hana jazba na anajua kuchambua mambo kwa kina na kwa sasa ndo mwanasheria na HR wa SAHARA COMPANY ya bwana Diaro huku akiibuka mwanafunzi bora wa sheria mwaka aliohitimu,atatuunganisha sana vijana coz hana makundi ,hivyo kuelekea 2015 atatufaa kiutendaji ndani ya chama.
7:Halima James Mdee,huyu anafaa sana kuwa mwenyekiti wa BAWACHA,Kwanza ni mwanamke jasiri na shujaa sana ndani ya chama na nje ya chama,kama mtakumbuka ndo alimtoa jasho Mbatia kuwa mbunge wa Kawe,mpaka aliposubiri huruma ya rais Jk,kwa nafasi hiyo atawashawishi wanawake wengi kujiunga nasi na hatimaye kutwaa nchi 2015,
8Jesca Kishoa,katibu BAWACHA ,ni binti mdogo kiumri na ndo kwanza amemaliza chuo mwaka huu,bt ameweza sana kufanya siasa jimboni Iramba kiasi cha kumtisha naibu katibu mkuu CCM Mwigulu Nchemba na kukimbilia kutoa vitisho kwenye mitandao ya kijamii hasa JF,kwa kusaidiana na mkomavu Mdee,wanawake wengi zaidi watajiunga na chama na hivyo kuharakisha kifo cha CCM na hivyo kuikomboa nchi hii kutoka kwenye lindi la umasikini.
9:professa Abdalah Safari,huyu anafaa kuwa mwenyekiti wa CDM Zanzibar,huyu ni mwanazuoni anaeweza sana siasa za kutulia na atatusaidia sana kuongeza wanachama kutoka huko visiwani Zanzibar,mbali na kuwa mwanasheria lakini ni mtaalamu sana wa siasa za kimataifa hivyo atatuunganisha kimataifa kwa kushirikiana na Baregu.hivyo kuleta changamoto mpya visiwani Zanzibar,ambayo kwa kipindi kirefu ilitawaliwa na vyama viwili CUF na CCM.
Zitto akifanikiwa kuvuka salama kwenye hili sakata lake atulie tu ndani ya chama asiwanie nafasi yoyote mpaka 2019,kwani kwa sasa atakigwa chama zaidi kutokana na makundi hasimu yanayosigana ndani ya chama ambayo kwa namna moja ama nyingine yamekuwa yakimhisisha,pia kma katiba itamruhusu kufanya hivyo hasa ikizingatiwa anamajukumu mengi ya kikamati ya bunge na pia mwenyekiti wangu wa chama japo katiba inampa nafasi bt aseme inatosha hapa chama alipokifikisha awaachie wengine na abakie kma mshauri tu wa chama,kwa leo naomba niishi hapa nisiwachoshe sana na huu mtazamo wangu hasa kwa kuzingatia kwamba watanzania c wapenda kusoama vitu virefu kama hivi.
by Nicholaus Kirunga 4m Kibondo Kigoma TZ
0754926271
email,nickkilunga@yahoo.com
nakaribisha maono na ukosoaji wa kistaarabu


my take:jamaa kachambua vizuri hivyo tuweke makundi kando


  • A%20S%20tongue.gif
 
Back
Top Bottom