Viongozi wanafiki, wakatili na wauaji wanaojipa matumaini giza juu ya misongomano ya dini kipindi hiki cha ugonjwa wa Corona

Thailand

JF-Expert Member
Nov 15, 2019
262
778
Unaweza kushangaa mpaka Leo taifa la Tanzania bado misongomano misikitini na makanisani bado inaruhusiwa. Duu Ni ajabu! Inamaana Hawa viongozi wetu wanaishi visiwani kwamba yote yanayotokea Ulimwenguni hawayasikii Wala kuyaona!

Inajulikana kabisa kwamba msongamano ndio njia rahisi kabisa ya kueneza virus vya COVID-19 lakini kwa Tanzania misongomano kwa baadhi ya maeneo bado inaruhusiwa.

Nchi za ulaya pia zilidhani huo ni ugonjwa wa wachina pekee Kama baadhi ya watanzania wanavyoamini ugonjwa huu Ni wawazungu pekee kitu ambacho Ni kibaya maana madhala yatakuwa makubwa zaidi.

Katika mitandao ya kijamii Kuna kaujumbe kanasambazwa kakimusifu rais wa nchi kutokuzuia misongomano ya ibadani pia mkuu wa mkoa wa dar es salaam hivi juzi ameitisha mkutano wa azara akiongelea suala Hilo Hilo la kutokuzuia misongomano ya ibadani eti kinafiki kwamba Mungu huyo huyo aliyewavusha kwenye majanga ya Ebola, matetemeko ya ardhi, tsunami n.k ndio huyo huyo atawavusha kwenye janga hili la Corona.

Duu! Naduwahaa!

Hivi ni lini mtu muovu, katili, mnafiki na yeye akajitapa kwamba anaamini katika Nguvu ya Mungu?

Ni lini Roho Safi ya Mungu ikaambatana na Roho chafu za wanadamu?
Viongozi hao wanaojionyesha leo Wana hofu ya Mungu ndio hao hao wanaongoza kwa mauaji, visasi, Roho mbaya na matendo yote ya kikatili kwa wanadamu wenzao.

Tafadhali enyi vipofu msimjaribu Bwana Mungu wenu.
ZUIENI MISONGOMANO YA IBADA MAKANISANI NA MISIKITINI kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu hatari kwa wana wa Mungu wasio na hatia.

Mnapozuia misongomano ya ibada makanisani na misikitini sio kwamba mmezuia Imani za watu Bali mnalida afya zao. Maana sio busara kujitumbukiza kwenye shimo na kujifariji kwa kusema Mungu atakuinua kutoka katika shimo Hilo.

Serikali isisitize Watu wazidi kusali na kutubu majumbani mwao (kifamilia) wakimulilia Mungu aiepushe dunia juu ya mipango ovu ya ibilisi na sio kudanganya watu kwamba Corona haiwezi kuwafikia kwa wao kuendelea kujazana makanisani na misikitini.
 
Aisee. Niliwaza sana nilipomuona Baba Mtakatifu Francis akiendesha ibada akiwa peke yake akisikilizwa kwa njia ya redio na mitandao. Niliwaza ni imani gani aliyo nayo Magufuli alipowatangazia waumini kanisani kuwa Korona haiingii kanisani.
Nikajiuliza kati ya Vatican na parokia ya Osterbay ni wapi pana utukufu wa kuzuia Korona?
Nilishangazwa sana na hii imani ya waafrika.
 
Mkuu usiende mbali sana umeona yale mapicha ya raisi akiwa milimani na kitaa akinywa kahawa na ile kauli tufanye kazi tusitishane basi leo jibu limepatikana kutoka kwa spika wa bunge kama tukiweka nchi lockdown wananchi watakufa njaa maana yake serikali awanauwezo wa kumudu garama cha muhimu mkuu tuombe mungu ili janga liishie huko huko
The enemy at the gate
 
Tanzania ni nchi yenye imani isiyotetereka, Magufuli alisema Ka - Corona kasitutishe ni kaugonjwa kadogo sana, baada ya hapo akaenda kulala kwenye mawe huko, sijui ndio alienda kutambika? na alipotoka alionekana Chato akinywa al kasusu bila wasiwasi.
Na funny enough hata Ka Corona kana sita sita kuingia Tanzania, So far kame mtungua mmoja tena kwa mbali, hivyo tuwape watanzania big up maana kweli hawajasitisha misongamano, na hakuna quarantine na Corona inasuasua, wananchi wanasonga mbele na wanapiga kazi.

Msiogope tutashinda na tutabaki salama, Corona itapita mbali kama NZIGE.
 
Acha watu waabudu,,we kwavile mpagani ndo unataka makanisa na misikiti vifungwe?
Acha fitina,

.suala la dini usiliguse kabisa,semea kwingine..

Yaan kwavile umeanza na hoja yako kwa kutaka makanisa na misikiti vifungwe tayar uzi wako umekosa radha..
 
Aisee. Niliwaza sana nilipomuona Baba Mtakatifu Francis akiendesha ibada akiwa peke yake akisikilizwa kwa njia ya redio na mitandao. Niliwaza ni imani gani aliyo nayo Magufuli alipowatangazia waumini kanisani kuwa Korona haiingii kanisani.
Nikajiuliza kati ya Vatican na parokia ya Osterbay ni wapi pana utukufu wa kuzuia Korona?
Nilishangazwa sana na hii imani ya waafrika.
Ndiyo maana tumeambiwa tuna rais wa ajabu!
 
Back
Top Bottom