thereitis
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 297
- 41
Kuna tofauti kuu kati ya uongozi(Leadership) na utawala(administrator). Sifa kuu ya kiongozi ni uwezo wa kushawishi watu anaowaongozi kutenda jambo ambalo yeye kama kiongozi anaone lina manufaa kwa anaowaongozi. Mtawala hana sifa hiyo; majukumu yake makuu ni kuhakikisha mambo yanafanyika kwa kutumia mamlaka aliyonayo mfano kutumia askari kudhibiti wale wanaoenda kinyime na mipango ya utawala.
Siku za karibuni tumeshuhudia maandamano au vurugu za polisi dhidi ya raia wasio na silaha - Arusha, Mbeya, Mwanza na Dar ni baadhi ya maeneo ambapo vurugu zimetokea. Vurugu hizi zinadhihirisha nini? Je Viongozi wetu wamekosa ile sifa kuu ya kushawishi wananchi?
Siku za karibuni tumeshuhudia maandamano au vurugu za polisi dhidi ya raia wasio na silaha - Arusha, Mbeya, Mwanza na Dar ni baadhi ya maeneo ambapo vurugu zimetokea. Vurugu hizi zinadhihirisha nini? Je Viongozi wetu wamekosa ile sifa kuu ya kushawishi wananchi?