Viongozi wakuu wa CHADEMA wamaliza mgogoro Ruvuma

MZK

JF-Expert Member
Sep 13, 2012
223
303
VIONGOZI WAKUU WA CHADEMA WAMALIZA MGOGORO RUVUMA

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, ujio wa wajumbe wa kamati kuu ya CHADEMA katika mkoa wa Ruvuma wakiongozwa na makamo mwenyekiti wa chama Prof. Abdallah Safari, waziri mkuu mstaafu Mh. Edward Lowassa na naibu katibu mkuu visiwani Salum Mwalim wamefanikiwa kumaliza mgogoro wa kisiasa uliodumu kwa muda mrefu mkoani humo na hatimaye kamati tendaji ya chama hicho wilaya ya Songea mjini kukubali kuachia ngazi na kupisha wanachama wengine kushika nafasi hiyo.

Baada ya hatua hiyo ukumbi ulitawaliwa na nderemo na vifijo kuashiria mwanzo mpya wa uongozi katika chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Baadhi ya wanachama wamesikika wakitoa maoni yao na kupongeza viongozi hao wakuu wa chama kwa busara yao iliyotumika kumaliza mgogoro huo.

NB: Kwenye picha ni Viongozi wa wilaya ya Songea mjini wa CHADEMA waliokubali kujiuzulu, wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati kuu walioko mkoani Ruvuma katika ziara maalum ya kukijenga chama
 

Attachments

  • IMG-20161124-WA0019.jpg
    IMG-20161124-WA0019.jpg
    66.9 KB · Views: 55
Hapo sidhani kama wametatua mgogoro. Sababu kiongozi anaeamua kujiuzulu kutokana na mgogoro huwezi jua kwenye nafsi yake ana msimamo gani
 
Hawana uwezo wa kumaliza mgogoro wowote ...cheap popularity
 
Kumbe Lowasa ni kiongozi mkuu wa chadema! Ndio cheo gani kwenye katiba ya chadema?
 
Kumbe Lowasa ni kiongozi mkuu wa chadema! Ndio cheo gani kwenye katiba ya chadema?

Sehem gan umeona pameandikwa hvo kwamba Lowassa ni kiongoz mkuu wa chadema??

Kama huna cha kuchangia pita tu!!

Maana ametajwa kwa cheo chake cha zaman. Aliyekua waziri mkuu.
 
Sehem gan umeona pameandikwa hvo kwamba Lowassa ni kiongoz mkuu wa chadema??

Kama huna cha kuchangia pita tu!!

Maana ametajwa kwa cheo chake cha zaman. Aliyekua waziri mkuu.
Mi nimesoma Uzi wa mtoa mada na nikauliza kutokana na yaliyoandikwa ndani ya mada yake. Acha kutoa povu dogo
 
Back
Top Bottom