ARCHBISHOP
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 271
- 484
Ndugu zangu, salaam.
Binafsi nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa zawadi ya uhai.
Nilibahatika kukutana na video niliyoambatanisha na ilinikwaza nafsi yangu mpaka nikafikia kuandika humu labda itamfikia mhusika.
Kama mwanaume nimekuwa katika mausiano na mwenzangu kwa zaidi ya miaka 13 sasa. Katika kipindi chote hiki tukiwa wapenzi, baadae kuwa wanandoa, nilijiapiza kutofanya mahusiano nje ya ndoa na kutofanya mapenzi na mtu zaidi yake. Niliweka nadhiri hii na yeye, lakini zaidi niliiweka na nafsi yangu.
Siyo kwamba sikuwahi kupata matamanio au vishawishi katika kipindi hiki chote, isipokuwa niliamua kutoendeshwa na mwili, bari niendeshwe na akili pamoja na utashi.
Katika muda huu wote nimeishi maisha ya amani siyo na mke wangu pekee hata na nafsi yangu, huwa najisikia vizuri sana ninapomwambia "Nakupenda sana Mke wangu" huku ikitoka Moyoni bila makando kando.
Kukutana na video hii na nyingine zenye kujiapiza kwa haiwezekani mwanaume kuwa mtulivu kwa mke wake mmoja nikutukosea heshima tulio chagua kuwa wakweli kwa wenzetu. Binadamu ni dhaifu, mwenzio anaweza anza kukutilia mashaka pale unaposisitiza kuwa ni yeye tu katika nafsi yako.
Niwashauri wanaume wenzangu, hata kama inachekesha au kusema baadhi ya ukweli, tusiisambaze kwa mstakabari wa watoto wetu wa kiume tunaowalea.
Mwisho, tuwe wakweli kwa wake zetu na wapenzi wetu na tuwapende bila kutegemea chochote toka kwao na tutaishi kwa amani isiyokuwa na kipimo.
*HAIJALISHI YEYE ANAFANYA NINI, KAMA NAFSI YAKO NI NYEUPE, BASI WEWE NDIYE MSHINDI*
Binafsi nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa zawadi ya uhai.
Nilibahatika kukutana na video niliyoambatanisha na ilinikwaza nafsi yangu mpaka nikafikia kuandika humu labda itamfikia mhusika.
Kama mwanaume nimekuwa katika mausiano na mwenzangu kwa zaidi ya miaka 13 sasa. Katika kipindi chote hiki tukiwa wapenzi, baadae kuwa wanandoa, nilijiapiza kutofanya mahusiano nje ya ndoa na kutofanya mapenzi na mtu zaidi yake. Niliweka nadhiri hii na yeye, lakini zaidi niliiweka na nafsi yangu.
Siyo kwamba sikuwahi kupata matamanio au vishawishi katika kipindi hiki chote, isipokuwa niliamua kutoendeshwa na mwili, bari niendeshwe na akili pamoja na utashi.
Katika muda huu wote nimeishi maisha ya amani siyo na mke wangu pekee hata na nafsi yangu, huwa najisikia vizuri sana ninapomwambia "Nakupenda sana Mke wangu" huku ikitoka Moyoni bila makando kando.
Kukutana na video hii na nyingine zenye kujiapiza kwa haiwezekani mwanaume kuwa mtulivu kwa mke wake mmoja nikutukosea heshima tulio chagua kuwa wakweli kwa wenzetu. Binadamu ni dhaifu, mwenzio anaweza anza kukutilia mashaka pale unaposisitiza kuwa ni yeye tu katika nafsi yako.
Niwashauri wanaume wenzangu, hata kama inachekesha au kusema baadhi ya ukweli, tusiisambaze kwa mstakabari wa watoto wetu wa kiume tunaowalea.
Mwisho, tuwe wakweli kwa wake zetu na wapenzi wetu na tuwapende bila kutegemea chochote toka kwao na tutaishi kwa amani isiyokuwa na kipimo.
*HAIJALISHI YEYE ANAFANYA NINI, KAMA NAFSI YAKO NI NYEUPE, BASI WEWE NDIYE MSHINDI*