Viongozi wa Juu wa CHADEMA kuongea na Wanahabari Novemba 25, 2020 Makao Makuu ya Chama, Kinondoni

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,199
217,157
Kesho Jumatano, Novemba 25, 2020, CHADEMA kupitia uongozi wa juu wa Chama, kitazungumza na Umma wa Watanzania kupitia waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, katika mkutano utakaofanyika Ofisi za Makao Makuu ya Chama, kuanzia saa 5 asubuhi. Asanteni.

Wote Mnakaribishwa.
 
Tupo siti za mbele. Tutafanya mabadiliko na ushawishi tukiwa ndani. Maana waTanzania wengi ni waoga, mbinu iliyobaki ni sisi wachache kuingia ndani huko huko kuendeleza mapambano huku tukiwaacha wengi wanaodai wanapenda mabadiliko wakiwa wamejifungia ndani ya maskani zao wakidhani watakuwa salama.
 
Kesho Ufipa
images.jpeg
 
Mngetulia kwanza mkajipanga, huku kukurupuka ili mradi kushindana na jamii ya mitandaoni ndo kutazidi kuwatoa relini.

Jana mzee wa Miga katoa tamko bila kuwasiliana na CHADEMA kujua kinachojiri.

Leo wanamama wameapishwa huku kiongozi wao akimtaja Mwenyekiti Mbowe. Kesho Makene au Mnyika atakurupuka kuongea, keshokutwa atakuja Mbowe kuwapongeza wanamama walioapishwa leo.

Wanachama mtabaki kila mtu ananena kwa lugha yake. Yote kwa yote mnaowaamini wanasiasa endeleeni, Ila hatutachoka kuwaambia sio Lissu, Mbowe, Mnyika wala nani wote wachumia matumbo tu.
 
Back
Top Bottom