Viongozi wa Dini wasibezwe kwa kutouliza mambo ya siasa kwani wao si wanasiasa

tatum

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
5,786
4,490
Ukipitia mitandao mingi ya kijamii mara baada ya kikao cha Rais na Viongozi wa Dini kumekuwa na lawama nyingi sana na kuwakosoa Viongozi wa Dini kuhusu hoja walizozitoa kwa Rais kuhusu masuala mazima ya ustawi wa watanzania na changamoto wanazopitia taasisi za dini na serikali ya Tanzania.

Viongozi wengi wa dini walitoa namna ambavyo wanatoa michango yao kustawisha jamii ya kitanzania kiroho na kimwili na changamoto wanazokumbana nazo namna ambavyo mahali pengine wanakwama kabisa na Rais amejaribu kuzipitia na baadhi kuzitolea ufafanuzi na zingine kuzichukua na kuahidi kuzifanyia kazi yeye na watendaji wake kwa kadri inavyofaa ili changamoto nyingi ziweze kutatuliwa kwa wakati.

baadhi ya michango mingi huku katika mitandao ni kama vile viongozi wa dini hawajauliza au kutoa hoja ambazo walitegemewa kuzitoa kwa maoni ya wanasiasa lakini ukiangalia mambo ya dini hayaingiliani na mambo ya kisiasa ingawaje yupo aliyejaribu kuuliza kuhusu demokrasia na Rais alilifafanua vizuri tu

Mambo mengi yameulizwa kuhusu afya,elimu,maji,maadili,mahusiano kati ya serikali na taasisi za dini,kodi,sheria,vyombo vya dola,watendaji wa serikali,masomo ya wanadini nje ya nchi,unyanyasaji wa wanadili pale uwanja wa ndege,mambo ya mirathi na ndoa kwa dini ya kiislamu kutambulika kisheria na mengine mengi tu kadha wa kadha.

Kwa mtazamo wangu viongozi wa dini hawawezi kuuliza mambo ya kisiasa kama ambavyo viongozi wa kisiasa wanataka na walitaka hivyo ikifika zao yao viongozi wa kiasiasa kuongea na Rais basi wauulize mambo yao ya kisaisa kwasababu kuna uwezekano mkutano wao na Rais kwa viongozi wa kisiasa unakuja kwa jinsi itakavyo mpendeza Rais.

Tuwaheshimu viongozi wetu wa dini kwa kuonyesha moyo wa unyenyekevu mbele ya Rais maana wanajua kuwa mamlaka zote hutoka kwa Mungu ukifika muda wa wanasiasa kuongea na Rais basi waulize hayo mambo yao ya kisiasa na si kuwatukana na kuwabeza viongozi wa dini.

Hata wadau wa madini hawakuuliza mambo ya kisiasa katika mkutano wao na Rais siku walipofanya mkutano naye.
 
Ukipitia mitandao mingi ya kijamii mara baada ya kikao cha Rais na Viongozi wa Dini kumekuwa na lawama nyingi sana na kuwakosoa Viongozi wa Dini kuhusu hoja walizozitoa kwa Rais kuhusu masuala mazima ya ustawi wa watanzania na changamoto wanazopitia taasisi za dini na serikali ya Tanzania.

Viongozi wengi wa dini walitoa namna ambavyo wanatoa michango yao kustawisha jamii ya kitanzania kiroho na kimwili na changamoto wanazokumbana nazo namna ambavyo mahali pengine wanakwama kabisa na Rais amejaribu kuzipitia na baadhi kuzitolea ufafanuzi na zingine kuzichukua na kuahidi kuzifanyia kazi yeye na watendaji wake kwa kadri inavyofaa ili changamoto nyingi ziweze kutatuliwa kwa wakati.

baadhi ya michango mingi huku katika mitandao ni kama vile viongozi wa dini hawajauliza au kutoa hoja ambazo walitegemewa kuzitoa kwa maoni ya wanasiasa lakini ukiangalia mambo ya dini hayaingiliani na mambo ya kisiasa ingawaje yupo aliyejaribu kuuliza kuhusu demokrasia na Rais alilifafanua vizuri tu

Mambo mengi yameulizwa kuhusu afya,elimu,maji,maadili,mahusiano kati ya serikali na taasisi za dini,kodi,sheria,vyombo vya dola,watendaji wa serikali,masomo ya wanadini nje ya nchi,unyanyasaji wa wanadili pale uwanja wa ndege,mambo ya mirathi na ndoa kwa dini ya kiislamu kutambulika kisheria na mengine mengi tu kadha wa kadha.

Kwa mtazamo wangu viongozi wa dini hawawezi kuuliza mambo ya kisiasa kama ambavyo viongozi wa kisiasa wanataka na walitaka hivyo ikifika zao yao viongozi wa kiasiasa kuongea na Rais basi wauulize mambo yao ya kisaisa kwasababu kuna uwezekano mkutano wao na Rais kwa viongozi wa kisiasa unakuja kwa jinsi itakavyo mpendeza Rais.

Tuwaheshimu viongozi wetu wa dini kwa kuonyesha moyo wa unyenyekevu mbele ya Rais maana wanajua kuwa mamlaka zote hutoka kwa Mungu ukifika muda wa wanasiasa kuongea na Rais basi waulize hayo mambo yao ya kisiasa na si kuwatukana na kuwabeza viongozi wa dini.

Hata wadau wa madini hawakuuliza mambo ya kisiasa katika mkutano wao na Rais siku walipofanya mkutano naye.
Kwahiyo shida waumini zao haziwahusu? Kwani wao siasa haiwaathiri kwa namna moja au nyingine? Acha kujitoa ufahamu? Siasa ni kila kitu, hata waumini wao kwenda Kanisani/Misikitini ni kwa vile siasa inaruhusu/hali ya siasa ni nzuri. Kukitokea civil war atakwenda nani?
 
Wroooong!Kwa Wakristu,Yesu alipambana na watawala wa enzi hizo(wakiwemo viongozi wa dini na serikali/siasa) ili kuwatetea wanyonge,wadhambi na waliostahili haki bila hofu ya kuulizwa uraia wake.Hawa wa leo wanamtetea nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hajitambui huyu Mkuu kakurupuka tu. Hashangai wale ambao waliandika waraka kwa dikteta March 2018 ambao pia humkoromea dikteta mara kwa mara kwanini hawakualikwa?

Kwahiyo shida waumini zao haziwahusu? Kwani wao siasa haiwaathiri kwa namna moja au nyingine? Acha kujitoa ufahamu? Siasa ni kila kitu, hata waumini wao kwenda Kanisani/Misikitini ni kwa vile siasa inaruhusu/hali ya siasa ni nzuri. Kukitokea civil war atakwenda nani?
 
Basi Ngoja tuusuburi mkutano wa Rais na Viongozi wa Devil Worshipers labda utazaa matunda.naona utafanyika Tarehe 6mwezi wa 6saa 6 kamili.
 
Kwahiyo shida waumini zao haziwahusu? Kwani wao siasa haiwaathiri kwa namna moja au nyingine? Acha kujitoa ufahamu? Siasa ni kila kitu, hata waumini wao kwenda Kanisani/Misikitini ni kwa vile siasa inaruhusu/hali ya siasa ni nzuri. Kukitokea civil war atakwenda nani?
siasa hapa nchini ina shida gani.....acha kukuza mambo ambayo hayapo unadhani dhani tu
 
Hajitambui huyu Mkuu kakurupuka tu. Hashangai wale ambao waliandika waraka kwa dikteta March 2018 ambao pia humkoromea dikteta mara kwa mara kwanini hawakualikwa?
wote wamealikwa kama mtu hakwenda ni yeye mwenyewe
 
Wroooong!Kwa Wakristu,Yesu alipambana na watawala wa enzi hizo(wakiwemo viongozi wa dini na serikali/siasa) ili kuwatetea wanyonge,wadhambi na waliostahili haki bila hofu ya kuulizwa uraia wake.Hawa wa leo wanamtetea nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
kazi ya viongozi wa dini ni kukufanya wewe utende mema na uende mbinguni siku ukiaga dunia hayo mengine ni ziada
 
Kwahiyo shida waumini zao haziwahusu? Kwani wao siasa haiwaathiri kwa namna moja au nyingine? Acha kujitoa ufahamu? Siasa ni kila kitu, hata waumini wao kwenda Kanisani/Misikitini ni kwa vile siasa inaruhusu/hali ya siasa ni nzuri. Kukitokea civil war atakwenda nani?
anzisha hiyo civil war...uone kitakachotekea.....usiongee vitu kwa hisia wakati havipo....
 
Characteristics za dikteta zote anazo ikiwemo kudharau katiba, bunge na mahakama. Kugomea chaguzi huru na za haki. Kutisha wananchi/vyama vya upinzani na kuminya uhuru na haki zao zilizomo ndani ya katiba, kuminya Uhuru wa habari na vyombo vya habari na kujiona yeye kama Mungu mtu na hivyo kutokubali kukosolewa.





hatuna dikteta tanzania
 
Back
Top Bottom