BAOBAO
JF-Expert Member
- Oct 12, 2012
- 1,874
- 547
- Wakuu,mimi naona ni haki yao viongozi wa dini kuwakemea viongozi wa serikali katika ngazi yeyote ile.Pale,Viongozi wa dini wanapoacha au kushindwa kusimamia viongozi wa serikali;tangu katika mimbari za miskiti au madhabahu za makanisa wanayoongoza kwa kushindwa kukemea dhambi au makosa ya viongozi wa serikali;kumeleta mmomonyoko wa maadili kwa baadhi yao.Na viongozi wa serikali wakikosa watu wa kuwaonya na kuwakemea;wanaweza kutenda yasio haki na kuleta machukizo kwa jamii[MITHALI 16;12]. Lawama zangu ni kwa viongozi wa dini kabla ya viongozi wa serikali.
- Mtawala yeyote anaweza kutenda dhambi au kosa pasipo kukusudia jambo ambalo Mungu amezuilia,kwani si ajabu kama tujuavyo sote [MAMBO YA WALAWI 4:22,26;5:17].
- Nabii Nathani alimwambia wazi mtawala wa nchi kuwa ametenda dhambi ya kuua kwa siri,Mume wa mtu na kumchukua mkewe na kuzaa naye mtoto.[2 SAMWELI 12:1-15].
- Mfalme alikiri na kutubu dhambi yake;na kuwapa mfano viongozi wetu wa kukubali kukumewa na watumishi wa Mungu.
- Na Yesu Kristo aliomba msamaha kwa kosa ambalo alifanya msaidizi wake Simon Petro;la kumkata mtu sikio {LUKA 22:49-51}. Je,si vema viongozi wa dini nao kuiga mfano wa Yesu;kuomba msamaha kwa makosa ya waumini wao waliofanya kwenye jamii?
- Je,leo kuna viongozi wa dini nchini waliojaa ujasiri kukemea uovu bila kujali chanzo cha kosa kama nabii Nathani na wengine huko duniani ?Nawakilisha.