Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,236
Kunukuliwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akisema kuwa anapokuwa amesimama yeye basi anakuwa amesimama Mungu, kumeleta mfadhaiko miongoni mwa watu wenye akili timamu wanaojua nini inamaanishwa inaposemwa neno "Mungu". Lakini kauli hiyo pia imezifedhehesha dini zote zilizoko duniani.
Kila watu wakienda wanakoabudu wanaambiwa wanamuabudu "Mungu", halafu anasimama mtu na kusema akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu, hili ni dharau kwa waabudu Mungu. Makonda anataka kusema yeye ni Mungu ama ni Mwakilishi wa Mungu?
Kama waislamu wanasema "hakuna apaswaye kuabudiwa ila ni Mungu pekee..." nao ndugu zao Wakristo wanasema "Mungu ni mwenye wivu.." inakuwaje wanakaa kimya mtu mwingine anapojifananisha na Mungu? Au viongozi wa dini nao wanaamini anaposimama Makonda anakuwa amesimama Mungu?
Ukimya wa viongozi wa dini juu ya kauli ya Makonda kuhusu Mungu unapalilia ile dhana kwamba viongozi wa dini Tanzania wana Shirika na viongozi wa Serikali wanaotokana na CCM. Maana kuna wakati watu waliuliza inakuwaje viongozi wa vyama vya upinzani huwa hawaalikwi kwenye yale matamasha ya "amani"? Kumbe inawezekana waandaji labda huwa wanaogopa kumuudhi Mungu kwa kuwaalika Mashetani.
Hata kama aliahidi kusaidia kujenga Makao Makuu ya BAKWATA ama alimtembelea Kadinali Pengo Ofisini kwake, ni lazima Makonda aonywe na akemewe hadharani kwa tendo lake la kujilinganisha na Mungu. Viongozi wa dini huo ukereketwa wenu wa CCM unawaondolea sifa ya kuwa viongozi wa dini kwani sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa dini ni kuzuia Mungu KUDHIHAKIWA!!
Kila watu wakienda wanakoabudu wanaambiwa wanamuabudu "Mungu", halafu anasimama mtu na kusema akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu, hili ni dharau kwa waabudu Mungu. Makonda anataka kusema yeye ni Mungu ama ni Mwakilishi wa Mungu?
Kama waislamu wanasema "hakuna apaswaye kuabudiwa ila ni Mungu pekee..." nao ndugu zao Wakristo wanasema "Mungu ni mwenye wivu.." inakuwaje wanakaa kimya mtu mwingine anapojifananisha na Mungu? Au viongozi wa dini nao wanaamini anaposimama Makonda anakuwa amesimama Mungu?
Ukimya wa viongozi wa dini juu ya kauli ya Makonda kuhusu Mungu unapalilia ile dhana kwamba viongozi wa dini Tanzania wana Shirika na viongozi wa Serikali wanaotokana na CCM. Maana kuna wakati watu waliuliza inakuwaje viongozi wa vyama vya upinzani huwa hawaalikwi kwenye yale matamasha ya "amani"? Kumbe inawezekana waandaji labda huwa wanaogopa kumuudhi Mungu kwa kuwaalika Mashetani.
Hata kama aliahidi kusaidia kujenga Makao Makuu ya BAKWATA ama alimtembelea Kadinali Pengo Ofisini kwake, ni lazima Makonda aonywe na akemewe hadharani kwa tendo lake la kujilinganisha na Mungu. Viongozi wa dini huo ukereketwa wenu wa CCM unawaondolea sifa ya kuwa viongozi wa dini kwani sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa dini ni kuzuia Mungu KUDHIHAKIWA!!