Viongozi wa dini madhara ya Katiba iliyopo mmeyaona, changieni kupata Katiba mpya

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Feb 19, 2021
3,086
4,881
Hakika inashangaza sana kwa viongozi wetu wa dini kukaa kimya juu ya suala la katiba mpya. Viongozi wa dini wameshuhudia matumizi mabaya ya katiba iliyopo yalivyofanywa na mwendazake.

Watu wengi wameumizwa sana na katiba hiyo kwani mwendazake aliweza kuitumia atakavyo. Hayati baba wa taifa aliwahi kusema katiba hii ukipata kiongozi mbaya atawaumiza wananchi na ndivyo ilivyotokea.

Tunawaomba viongozi wa dini zote mkishirikiana na viongozi wa vyama na asasii za haki za binadamu tuidai katiba mpya ili nchi iongozwe kwa haki bila upendeleo na kumfanya mtu mmoja anakuwa mungu mtu.

Nchi za jirani tumewashuhudia viongozi wa dini wakishiriki kuwapigania wananchi kupata katiba mpya mfano jamhuri ya kidemokrasia ya kongo n.K. Viongozi wa dini mtamwambia nini Mungu atakapowauliza kwanini hamkuwasaidia watu wangu wasiteswe na watawala?
 
Yani ile rasimu ya Warioba ni dawa kwa watanzania, na mimi ninayo hapa naisoma kila siku
 
Watu wengi wameumizwa sana na katiba hiyo kwani mwendazake aliweza kuitumia atakavyo. Hayati baba wa taifa aliwahi kusema katiba hii ukipata kiongozi mbaya atawaumiza wananchi na ndivyo ilivyotokea.

Tunawaomba viongozi wa dini zote mkishirikiana na viongozi wa vyama na asasii za haki za binadamu tuidai katiba mpya ili nchi iongozwe kwa haki bila upendeleo na kumfanya mtu mmoja anakuwa mungu mtu.
Inabidi kampeni hii iende sambamba na kubadili mind set ya watanzania wote
 
Viongozi wa dini Tanzania hii wapo 5 tu Bora tuwakumbushe wajibu wao Ila wengine wapigaji tu
 
Hivi viongozi wa Dini walikuwa wanataka nini kwenye Katiba yetu mpya (sidhani kama kutetea wanyonge ilikuwa ni muhimu sana kwao)

Wengine walidai siku zako za kuabudu ziwe siku ya mapumziko, wengine walidai kodi zisaidie kuendesha mambo ya Imani zao n.k. Nakubaliana na wewe wasaidie kutengeneza Katiba bora ila Ubora wa huo Katiba uwe mwendelezo wa kwamba serikali yetu haina dini wananchi wao ndio wana dini
 
Back
Top Bottom