NewDawnTz
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 1,667
- 362
Amesema atakuja kuongea na nyie kuhusu mgawanyiko wa kidini uliokuwepo.
Sina uhakika kama mlishiriki nae kuunda huo udini kiasi cha kuja kuwauliza namna ya kuumaliza, maana kama hamkushiriki huenda hamjui sababu ya mgawanyiko wa udini na msiweze kumsaidia bali kuongeza mgawanyiko uliopo.....Nina wasiwasi juu ya hili.
Hata hivyo mwambieni anahitajika kufanya yafuatayo kati ya mengi,
(i) Kuwaomba radhi watanzania kwa yeye na mwenzake makamba kuasisi siasa za udini Tanzania. Kwa kuwa wote tunajua yeye na makamba ndio waasisi, wasipofanya hivi tutawaona wanafiki tu wakiendeleza unafiki wao wa ku-win mioyo ya wabongo ili 2015 watuletee bomu jingine
(ii) Kuomba radhi viongozi wa CHADEMA tena mbele ya umma uleule ambao waliwasingizia kuwa wanasiasa za udini jambo ambalo uthibitisho wake ni mfinyu maana unajengwa kwa akili za kuku wa kafara
(iii) Kuunda tume mpya ya uchaguzi itakayokuwa huru na isiyo mikononi mwake ili isendelee kubeba uchakachuaji
(iv) Katiba mpya itakayotoa mwanya wa kuwajibisha viongozi wasioingia madarakani kwa haki na wanaotumia madaraka yao vibaya
Kwa leo haya yanatosha labda kama wadau watawaongezea mengine viongozi wa dini
Bila haya hatutawaelewa, hata kama wewe ni askofu wangu au nani,
HII NI HATMA YA NCHI YANGU AMBAYO NI ZAIDI YA DINI YANGU
Sina uhakika kama mlishiriki nae kuunda huo udini kiasi cha kuja kuwauliza namna ya kuumaliza, maana kama hamkushiriki huenda hamjui sababu ya mgawanyiko wa udini na msiweze kumsaidia bali kuongeza mgawanyiko uliopo.....Nina wasiwasi juu ya hili.
Hata hivyo mwambieni anahitajika kufanya yafuatayo kati ya mengi,
(i) Kuwaomba radhi watanzania kwa yeye na mwenzake makamba kuasisi siasa za udini Tanzania. Kwa kuwa wote tunajua yeye na makamba ndio waasisi, wasipofanya hivi tutawaona wanafiki tu wakiendeleza unafiki wao wa ku-win mioyo ya wabongo ili 2015 watuletee bomu jingine
(ii) Kuomba radhi viongozi wa CHADEMA tena mbele ya umma uleule ambao waliwasingizia kuwa wanasiasa za udini jambo ambalo uthibitisho wake ni mfinyu maana unajengwa kwa akili za kuku wa kafara
(iii) Kuunda tume mpya ya uchaguzi itakayokuwa huru na isiyo mikononi mwake ili isendelee kubeba uchakachuaji
(iv) Katiba mpya itakayotoa mwanya wa kuwajibisha viongozi wasioingia madarakani kwa haki na wanaotumia madaraka yao vibaya
Kwa leo haya yanatosha labda kama wadau watawaongezea mengine viongozi wa dini
Bila haya hatutawaelewa, hata kama wewe ni askofu wangu au nani,
HII NI HATMA YA NCHI YANGU AMBAYO NI ZAIDI YA DINI YANGU