Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 4,448
- 16,311
"Nilitumia miaka 15 kumlilia Mungu tupate mtu atakayeipenda Tanzania, atakayewapenda Watanzania, Mungu akakuleta Rais Magufuli." Mwingira Mbele ya JPM 2018.
"Nilinusurika kuuwawa mara tatu,awamu ile ilikuwa inadhulumu haki za watu na kupora uchaguzi." Mwingira chini ya Rais Samia 2021.
Hawa wanaojiita maaskofu na wana makanisa yao wengi sio wasafi kama tunavyofikiri. Maneno yao tuu yanawafunga, sembuse matendo? Wengi maneno yao yanalenga kujifanya kuendana na upepo wa serikali iliyopo madarakani, na wanapenda sana kubebwa hata kwenye mambo yasiyobebeka. Sasa wakikutana na kisiki kama JPM hawalalamiki, ila siku hiko kisiki kikitoka ndiyo wanaanza kujifanya kutoa ya moyoni.
Hawa maaskofu wachumia tumbo wakajifunze kwa mababa zao kina Askofu Shoo, Askofu Bagonza, Askofu Niwemugizi nk. Hawa hawajawahi kubadilisha nyeupe kuwa nyeusi kwenye maneno na vitendo vyao. Hawaogopi kuusema ule ukweli hata kama unakinzana na watawala.
Baada ya huyu Mwingira, tutegemee na Kakobe naye kuja na yake, maana hawa wote ni wachumia tumbo tuu.
"Nilinusurika kuuwawa mara tatu,awamu ile ilikuwa inadhulumu haki za watu na kupora uchaguzi." Mwingira chini ya Rais Samia 2021.
Hawa wanaojiita maaskofu na wana makanisa yao wengi sio wasafi kama tunavyofikiri. Maneno yao tuu yanawafunga, sembuse matendo? Wengi maneno yao yanalenga kujifanya kuendana na upepo wa serikali iliyopo madarakani, na wanapenda sana kubebwa hata kwenye mambo yasiyobebeka. Sasa wakikutana na kisiki kama JPM hawalalamiki, ila siku hiko kisiki kikitoka ndiyo wanaanza kujifanya kutoa ya moyoni.
Hawa maaskofu wachumia tumbo wakajifunze kwa mababa zao kina Askofu Shoo, Askofu Bagonza, Askofu Niwemugizi nk. Hawa hawajawahi kubadilisha nyeupe kuwa nyeusi kwenye maneno na vitendo vyao. Hawaogopi kuusema ule ukweli hata kama unakinzana na watawala.
Baada ya huyu Mwingira, tutegemee na Kakobe naye kuja na yake, maana hawa wote ni wachumia tumbo tuu.