Mkurugenzi wa organisation na mafunzo wa Chadema Taifa bwana Benson Kigaila na mratibu wa kinamama Chadema mkoa wa Dodoma Bi Kunti Yusuph leo wamepelekwa gereza la Isanga hapa Dodoma baada ya kukosa wadhamini katika kesi inayowakabili.
Hii ilitokana na aliyepewa jukumu la kuandaa wadhamini bwana Iddi Kizota ambaye ni katibu wa vijana mkoa wa Dodoma kutolewa nje ya mahakama na polisi kwa kitendo kilichodaiwa ni kudharau mahakama kwani alikuwa anataja majina ya wadhamini badala ya watuhumiwa wenyewe ambapo ilipelekea hakimu kuamuru atolewe nje ya mahakama na kupelekwa kituo cha polisi.
Kitendo hiki alichofanya katibu huyu wa vijana kilikuwa ni cha kizembe kwani alishauriwa kabla, kuwapa watuhumiwa majina ya wadhamini ili wawataje wenyewe mbele ya mahakama, hivyo ikapelekea watuhumiwa hawa wawili kati ya kumi na moja (11) kupelekwa Isanga hadi tarehe 08/11/2011 kesi itakapo tajwa tena.
Hata hivyo niliongea na diwani wa kata ya makulu Mh.Biringi akasema kesho watashughulikia remove order.
Makosa waliyotuhumiwa nayo ni pamoja na kufanya mkutano ambao haujaruhusiwa, kushawishi wananchi kufanya vurugu kwenye kitongoji cha njedengwa, kuwashawishi wananchi wa njedengwa kuwapiga askari kwa mishale ya sumu pamoja na kuvunja amani.
Naomba kuwasilisha.
Source nilikuwa mahakamani.
Hii ilitokana na aliyepewa jukumu la kuandaa wadhamini bwana Iddi Kizota ambaye ni katibu wa vijana mkoa wa Dodoma kutolewa nje ya mahakama na polisi kwa kitendo kilichodaiwa ni kudharau mahakama kwani alikuwa anataja majina ya wadhamini badala ya watuhumiwa wenyewe ambapo ilipelekea hakimu kuamuru atolewe nje ya mahakama na kupelekwa kituo cha polisi.
Kitendo hiki alichofanya katibu huyu wa vijana kilikuwa ni cha kizembe kwani alishauriwa kabla, kuwapa watuhumiwa majina ya wadhamini ili wawataje wenyewe mbele ya mahakama, hivyo ikapelekea watuhumiwa hawa wawili kati ya kumi na moja (11) kupelekwa Isanga hadi tarehe 08/11/2011 kesi itakapo tajwa tena.
Hata hivyo niliongea na diwani wa kata ya makulu Mh.Biringi akasema kesho watashughulikia remove order.
Makosa waliyotuhumiwa nayo ni pamoja na kufanya mkutano ambao haujaruhusiwa, kushawishi wananchi kufanya vurugu kwenye kitongoji cha njedengwa, kuwashawishi wananchi wa njedengwa kuwapiga askari kwa mishale ya sumu pamoja na kuvunja amani.
Naomba kuwasilisha.
Source nilikuwa mahakamani.