Viongozi wa CHADEMA mliwapokea Lowassa na Sumaye kwa ridhaa ya nani, na kwa manufaa ya nani?

Kwa nguvu ya wananchi ilibidi watangazww tu!
Halafu kwenye level ya ubunge,hawachezi rafu sana maana kupoteza jimbo sio issue sana kama kwenye urais!Kama Zanzibar ingekuwa jimbo basi maalimu angetangazwa mshindi maana alishinda mchana kweupe Jecha akafanya yake!
Hakuna tume huru,muulize Kafulila alivyopokonywa tonge,kura ukijumlisha alikuwa kashinda yeye yule mama mgawa papuchi akatangazwa mshindi!Akaambaa na kesi mahakamani,walivyoona inakuwa so,wakamwambia aunge mkono juhudi na atapewa ulaji kwa namna nyingine na aachane na ubunge!
Njaa ikaishinda akili ujanja,akachamgamkia fursa!
Unaandika insha ndefu ili iweje?
 
Sentensi moja inaweza kuwa na maana zaidi ya moja. Lakini mwenye kuandika ndiye anayejua maana iliyokusudiwa.

Nimesema wenyenyewe (Mwambe, Lowassa na Sumaye ) ndio waliosema wamerudi nyumbani kwao na sio akina Mghwira na Katambi uliowataja wewe! Au unabisha kwamba hawajasema hivyo?

Hata hivyo suala hapa ni wanachadema kupenda hela; yaani wako tayari kufanya lolote kwa ajili ya pesa. Wote uliowataja wameahamia ccm na kuisaliti vyama vyao kwa ajili ya vyeo na pesa. Au unabisha?
Kwahiyo unatambua kuwa wanahongwa ila kuhamia CCM?Yaani kunakuwa na makubaliano kabla ya kuhamia CCM ndio wote walipewa vyeo kabla ya dirisha kufungwa!Ni vema mkawahonga ili CDM ibaki na watu pure ambao ni majabali haswa haswa!
Sumaye inajulikana karudi kwasababu ya mashamba yake kutaifishwa,Mbowe ameshafanyiwa figisu sana mpaka mali zake na mashamba kuharibiwa lakini yuko imara!Tunataka CDM ibaki na viongozi mfano wa Mbowe!Hao chukueni,tena endeleeni ili wenye roho za tamaa waishe kabisa!
 
Jibu swali; je walikuwa bado wanahitajika ndani ya CDM kama wanachama eti kwavile hakuna chama kinachokataa wanachama?
Ndio na ndio maana hawakufukuzwa uanachama!Walikuwa wanachama mpaka walivyoamua kujitoa wenyewe!
CDM milango iko wazi kama hata wewe unahitaji uanachama!Na mimi nimekaa miaka mingi bila kuwa mwanachama wa chama chochote na naona mwaka huu ni sahihi nami nikachukua kadi ya CDM!
 
Kwahiyo unatambua kuwa wanahongwa ila kuhamia CCM?Yaani kunakuwa na makubaliano kabla ya kuhamia CCM ndio wote walipewa vyeo kabla ya dirisha kufungwa!Ni vema mkawahonga ili CDM ibaki na watu pure ambao ni majabali haswa haswa!
Sumaye inajulikana karudi kwasababu ya mashamba yake kutaifishwa,Mbowe ameshafanyiwa figisu sana mpaka mali zake na mashamba kuharibiwa lakini yuko imara!Tunataka CDM ibaki na viongozi mfano wa Mbowe!Hao chukueni,tena endeleeni ili wenye roho za tamaa waishe kabisa!
Unaona unavyojichanfanya! Huku unasema "waende zao, wabaki wenye msimamo" na kule unasema "walikuwa wanahitajika ndo maana hawakufukuzwaa bali wamejiondoa wenyewe". Kweli we ni CDM pure!
 
Habari!

Mimi napenda kuwauliza viongozi wa CHADEMA. Je, uamuzi wa haraka wa kuwapokea na kuwapa nafasi haraka viongozi hawa wanaolipwa na kulindwa na serikali mpaka kifo chao mliotoa wapi?

Kwanini mliwapa nafasi ndani ya CHADEMA haraka? Mliamini ikulu mtaingia kupitia hawa? Mlitaka kuongeza ruzuku ndani ya chama mkiamini mtavuna wabunge wengi bila kujali matokeo ya mbeleni?

Je, mtakuwa tayari kuwaomba radhi wananchi kwa uamuzi wenu wa kukurupuka kwa kuwasajili Lowasa na wenzake ambao mliwaita mafisadi papa?

Niwawekee nukuu zenu za nyuma kuwakumbusha kuwa mnasahau haraka mnayoyasema majukwaani?

Je, mtakubali kuwa uwezo wenu wa kufanya reasoning ni mdogo na kwamba mna tatizo la akili?

Mwaka wa uchaguzi umefika, mtaletewa mamluki wengine; nanyi kwa tamaa ya pesa au uelewa mdogo mtawapokea kwa shangwe.
Walaumu kwa ya sasa, kama watafanya.

Hayo ya zamani ni kama unatafuta kuwasuta na kuanzisha mtifuano kwa mambo yaliyokwishatokea.

Ulikuwa na miaka minne ya kuwauliza na kuyazungumzia hayo, kwa nini sasa ndipo uone umhimu mkubwa wa kuyaibua?

Ulishakuwa na kidonda, kinaelekea kupona, mara unasukumiza limti ndani yake ili likidonda lizidi kudorora, ni akili timamu hiyo?
 
Kama ni hivyo kwanini Sumaye aliambiwa sumu haionjwi kwa kulamba? Kwanini Mwambe aliangushwa vibaya kwenye uchaguzi wa ndani? Hivi sio kwamba Sumaye na Mwambe walikatiliwa ndani ya CHADEMA au bado walikuwa wanahitajika kama wanachama?
Hawakuwa chaguo LA wapiga kura,uamuzi wa kurudi nyumbani ni haki yao ila kuondoka baada ya kukosa uongozi ni udhaifu wao.
Inaonekana wangepata hizi nafasi walizokuwa wakigombea wangeweza kuwasaliti wenzao,bora waondoke.
 
Hawakuwa chaguo LA wapiga kura,uamuzi wa kurudi nyumbani ni haki yao ila kuondoka baada ya kukosa uongozi ni udhaifu wao.
Inaonekana wangepata hizi nafasi walizokuwa wakigombea wangeweza kuwasaliti wenzao,bora waondoke.

Kunywa soda nakuja kulipa, umeongea vizuri sana
 
Kunywa soda nakuja kulipa, umeongea vizuri sana
Nashukuru kwa kunilipia soda,ila siyo kipaumbele changu.Tunatakiwa kuendelea kuusema ukweli.
Ni wazi ya kuwa hawa viongozi hawapo kwa maslahi ya Wananchi, tunatakiwa kuwapima viongozi vigeugeu na tuwakatae wawe upinzani au watawala(CCM).
 
Nashukuru kwa kunilipia soda,ila siyo kipaumbele changu.Tunatakiwa kuendelea kuusema ukweli.
Ni wazi ya kuwa hawa viongozi hawapo kwa maslahi ya Wananchi, tunatakiwa kuwapima viongozi vigeugeu na tuwakatae wawe upinzani au watawala(CCM).

Absolutely
 
Kama ni hivyo kwanini Sumaye aliambiwa sumu haionjwi kwa kulamba? Kwanini Mwambe aliangushwa vibaya kwenye uchaguzi wa ndani? Hivi sio kwamba Sumaye na Mwambe walikatiliwa ndani ya CHADEMA au bado walikuwa wanahitajika kama wanachama?
We kwa akili yako sumaye anaweza shika nafasi gan chadema? Hana mvuto kisiasa na hayo ya sumu Sijui nn ni mlango wa kutokea tu hana jipya kifuata upepo. Kashindwa hata kwenye uenyekiti kanda afu anataja uenyekiti taifa? Huu ni uzwa zwa wa kiwango cha PhD

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabunge waliongezeka
Wabunge wa viti maalumu waliongezeka
Ruzuku ya chama iliongezeka
Hayo yote uoni kama ni faida?
Huo ni uchaguzi wa 2015; kama mafanikio hayo yalipatikana kutokana na uwepo wao, je tutarajie mafanikio hayo kupungua kwenye uchaguzi ujao kwavile hawapo tena CHADEMA? Je, nikisema umaarufu na uhai wa chama hiki kinategemea makada wanaohamia toka ccm nitakosea?
 
Huo ni uchaguzi wa 2015; kama mafanikio hayo yalipatikana kutokana na uwepo wao, je tutarajie mafanikio hayo kupungua kwenye uchaguzi ujao kwavile hawapo tena CHADEMA? Je, nikisema umaarufu na uhai wa chama hiki kinategemea makada wanaohamia toka ccm nitakosea?

Kila ambae yuko upinzani alikuwa ccm,
 
Back
Top Bottom