IPECACUANHA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 3,216
- 1,906
Unapokua vitani nia ni kumshinda adui hata ikibidi kupitia kwa shangazi yake. Haya ni mawazo yangu tu. Sijibii mtu wala chamaHabari!
Mimi napenda kuwauliza viongozi wa CHADEMA. Je, uamuzi wa haraka wa kuwapokea na kuwapa nafasi haraka viongozi hawa wanaolipwa na kulindwa na serikali mpaka kifo chao mliotoa wapi?
Kwanini mliwapa nafasi ndani ya CHADEMA haraka? Mliamini ikulu mtaingia kupitia hawa? Mlitaka kuongeza ruzuku ndani ya chama mkiamini mtavuna wabunge wengi bila kujali matokeo ya mbeleni?
Je, mtakuwa tayari kuwaomba radhi wananchi kwa uamuzi wenu wa kukurupuka kwa kuwasajili Lowasa na wenzake ambao mliwaita mafisadi papa?
Niwawekee nukuu zenu za nyuma kuwakumbusha kuwa mnasahau haraka mnayoyasema majukwaani?
Je, mtakubali kuwa uwezo wenu wa kufanya reasoning ni mdogo na kwamba mna tatizo la akili?
Mwaka wa uchaguzi umefika, mtaletewa mamluki wengine; nanyi kwa tamaa ya pesa au uelewa mdogo mtawapokea kwa shangwe.