Viongozi wa CHADEMA mkoa wa Pwani wazuiwa na polisi kwa saa kadhaa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Viongozi na wanachama wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) mkoa wa Pwani wamezuiwa na jeshi la polisi kwa saa kadhaa wakati wakielekea mkoani Morogoro kuhudhuria mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha chama.

Viongozi hao kutoka mkoani Pwani wakiongozwa na katibu wa kanda ya Pwani wa chama hicho wamesema wamelazimika kusimamishwa na jeshi la polisi na kuhojiwa kwa saa kadhaa huku wakisindikizwa na jeshi hilo kutoka mkoani Pwani hadi Morogoro.

Akizungumza na wajumbe wa mafunzo hayo, mjumbe wa kamati kuu taifa ambaye pia ni mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Morogoro Suzan Kiwanga amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa chama hicho ambao wamekuwa wakiwadharau wanachama na kwamba kufanya hivyo kunahatarisha safari yao ya kushinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
chade23.jpg
 
Safi Sana maana wametoa escort ya maana kisa uoga nilishasema ni Wakati umefika wa kubadili uniforms za hawa polisi ziwe na rangi ya kijani na njano ili jeshi letu lifanye kazi kwa weledi zaidi
 
Hiki chama cha mapinduz kimesajiliwa kwa jina la jeshi la polisi kina tatizo sana.
 
Huku Mtaani kwetu (Kwa Mathias) Majangili yamevamia Nyumba za watu kiulaini kabisa kama yanaenda kwenye Sendoff wakati wenye dhamana ya kutulinda wametoa escort kwa Chama cha Siasa from Here to Moro
 
Huku Mtaani kwetu (Kwa Mathias) Majangili yamevamia Nyumba za watu kiulaini kabisa kama yanaenda kwenye Sendoff wakati wenye dhamana ya kutulinda wametoa escort kwa Chama cha Siasa from Here to Moro
Mkuu mi nipo kibondeni
 
Back
Top Bottom