Viongozi wa CCM wajifunze kwa wenzao wa Jubilee ya Kenya

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Hivi leo huko Kenya wananchi wa Kenya wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo, ikiwemo kumchagua Rais wa nchi hiyo atakayedumu kwa kipindi cha miaka 4 hadi mwaka 2021.

Katika uchaguzi huo kuna mchuano mkali sana kati ya Uhuru Kenyatta wa Jubilee na Raila Odinga wa NASA.

Hata hivyo kuna kitu nilichokishuhudia leo ambacho huwa hakitokei huku kwenye uchaguzi wetu huku Tanzania.

Katika hotuba aliyoitoa asubuhi ya leo, Rais anayemaliza muda wake Uhuru Kenyatta alitoa hotuba ya hekima mno alipowahamasisha wakenya wote wenye haki ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi kwenye vituo vya kupigia kura na kuwachagua wagombea watakaowaona wanafaa kuliongoza Taifa lao kwa kipindi cha miaka 4 ijayo,na kilichoonyesha kuwa demokrasia ya Kenya imekua sana ni pale Uhuru Kenyatta aliposema kuwa atayapokea kwa mikono miwili matokeo yoyote yatakayopatikana kwenye uchaguzi wa leo, hata kama atakayeshinda ni mgombea toka chama cha NASA, Raila Odinga.

Vile vile nilimsikia pia Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto naye wakati anapiga kura kwenye kituo chake cha kuoigia kura, alipohojiwa na waandishi wa habari naye akasema atayapokea matokeo yoyote ya leo kutokana na matakwa ya wapiga kura wa Kenya, hata kama wananchi watakuwa wameamua kuchagua Muungano wa NASA.

Nasema hizo kauli za wagombea hao 2 kutoka chama kilichoko madarakani hivi sasa, ni lazima ziwe mfano na kuigwa na wenzao wa CCM.

Tulishuhudia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, wagombea wote 2 wa nafasi ya Urais, JPM na mwenzake
Shein wa Zanzibar, walipohojiwa na waandishi wa habari ili kueleza msimamo wao ikiwa watakubali matokeo iwapo watakuwa wameshindwa uchaguzi huo, waligoma kujibu kuwa watakubali matokeo hayo na badala yake wakasema wao ni lazima watashinda!

Tujuavyo ni kuwa watu wawili mnaposhindana ni lazima atapatikana mshindi na mshindwa.

Na vile vile kuna msemo unaosema asiyekubali kushindwa siyo mshindani.

Kwa hiyo kwa kitendo cha wagombea wote 2_kwa tiketi za CCM yule wa Urais wa Jamhuri na yule wa Zanzibar, kugoma kukiri kuwa watayapokea matokeo hata kama ikiwa wao watashindwa ni dhahiri kuwa kumbe CCM huwa wanashinda kwa goli la mkono kwa maana ya kuwa kura zinapokuwa hazijatosha huwa wanalazimisha zitoshe!

Ni vyema kwa mfano ulioonyeshwa leo na wagombea,wa Jubilee, Uhuru Kenyatta na Wiliiam Ruto kwa kutamka hadharani kuwa iwapo watashindwa kwenye uchaguzi wa leo watskabidhi kwa amani kwa viongozi watakaoshinda, mfano huo pia uonyeshwe na viongozi wa CCM watakaosimama kwenye uchaguzi wa 2020, yaani kwa Urais wa Jamhuri ya Tanzania na yule wa Zanzibar wakatamka kabla ya siku ya kupiga kura kuwa matokeo yoyote yatakayotokea watakuwa tayari kuyapokea na watakabidhi kwa amani kwa viongozi watakaokuewa na kupewa riidhaa na wananchi kuliongoza Taifa letu.
 
Kwa siku ya uchaguzi unategemea wangeongea nini? Mbona hata JPM aliongea ivoivo siku ya uchaguzi.
 
Ya wakenya yanatuhu ni sisi,, hata tukikuuliza wewe sisi uchaguzi wakenya unatuhusu nini
Na wakati Mungu kashatupa jembe letu JPM??
 
Kwa siku ya uchaguzi unategemea wangeongea nini? Mbona hata JPM aliongea ivoivo siku ya uchaguzi.
Wewe ulimsikia?

Hakujawahi kutokea hapa TZ katika chaguzi zote za mfumo wa vyama vingi tokea mwaka 1095, ambapo wagombea wa Urais kwa upande wa Jamhuri na yule wa Zanzibar kutoka CCM aliyewahi kutamka kuwa atayapokea matokeo hata kama atakayeshinda atatoka upinzani.

Kama una ushahidi wa mgombea yeyote wa Urais wa CCM aliyewahi kutamka hivyo weka clip humu jamvini....
 
Ya wakenya yanatuhu ni sisi,, hata tukikuuliza wewe sisi uchaguzi wakenya unatuhusu nini
Na wakati Mungu kashatupa jembe letu JPM??
Tunachosema ni kuwa washondanapo wawili ni lazima atajitokeza mshindi na mshindwa.

Sasa ni kwanini CCM huwa haiamini kuwa kuna kushinda na kushindwa?

Kwa hiyo maana yake ni kuwa wao CCM huwa wanategemea goli la mkono katika kupata ushindi wake!
 
Tunachosema ni kuwa washondanapo wawili ni lazima atajitokeza mshindi na mshindwa.

Sasa ni kwanini CCM huwa haiamini kuwa kuna kushinda na kushindwa?

Kwa hiyo maana yake ni kuwa wao CCM huwa wanategemea goli la mkono katika kupata ushindi wake!
Makuu usiwe unapoteza kumbukumbu, siku ya uchaguzo wagombea wote wanafanyaga ivovio.
Nyuma ya pazia wanajua wanachofanya, usiwaamini sana wanasiasa. ila inaonekana we mdogo sana kwenye uwanja wa siasa.
Angalia hapo ya Magufuli
 
Kenya iko mbali sana kidemokrasia na kiuchumi, ni ukweli usiofichika kua: KENYA IS THE ONLY DEMOCRATIC COUNTY IN EAST AFRICA.
Acha kudundanganya wewe. Haya uliyoyaandika hapa unayajua lakini?
Unakumbuka alichokifanya Kibaki mwaka 2007, unakumbuka mitambo ilivyovurugwa mwaka 2013? Unakumbuka jinsi meneja wa ICT - Msando alivyouwawa kinyama?
Unaongelea Democrasia ipi?
Pumbavu kabisa.
 
Kifo na usingizi. Jubilee wao wanajua kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi. Ccm wanajua kuna ufisadi na rushwa baada ya uchaguzi. Hawapo madarakani kwa ajili ya kuhudumia wananchi. Wapo madarakani kwa ajili ya matumbo yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo sahihi kati ya nchi zote 6 ni Kenya pekee.
Kati ya nchi za East & Central Africa, Kenya inaweza kuwa ndiyo the leading Nation kwa upande wa kuwa na demokrasia ya hali ya juu..
 
Kifo na usingizi. Jubilee wao wanajua kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi. Ccm wanajua kuna ufisadi na rushwa baada ya uchaguzi. Hawapo madarakani kwa ajili ya kuhudumia wananchi. Wapo madarakani kwa ajili ya matumbo yao

Sent using Jamii Forums mobile app
Very true.

Ndiyo maana hao CCM wanajiona katika nchi hii ndiyo wao tu wenye haki ya kufanya mikutano ya kisiasa...

Wakifanya mikutano wapinzani "wanaamrisha" Polisi wao wawakamate na kuwafungulia mashitaka ya uchochezi!

Kwa maana nyingine CCM wanaamini wao ndiyo wenye hati miliki ya kutawala nchi hii hadi mwisho wa dunia!
 
CCM wakiulizwa hawawezi kukiri kuyapokea matokeo na zaidi watakusisitizia tu kwamba ushindi kwetu ni lazima kwa njia yoyote. Mara nyingi humalizia kwa kusema CCM ni chama dola na wanasahau kwamba katika chaguzi zinazohusisha mfumo wa vyama vingi, vyama dola hubadilika ya uchaguzi utakavyoamua hivo maandalizi kadili ya kujadili nguvu yao ya dola yanaweza kuanza siku matokeo ya uchaguzi yanatangazwa na siku ya kuapishwa Rais mpya kutoka chama kingine ndio siku ambayo nguvu ya dola ya chama kilichokuwa kinatawala huisha rasmi.
 
Wewe ulimsikia?

Hakujawahi kutokea hapa TZ katika chaguzi zote za mfumo wa vyama vingi tokea mwaka 1095, ambapo wagombea wa Urais kwa upande wa Jamhuri na yule wa Zanzibar kutoka CCM aliyewahi kutamka kuwa atayapokea matokeo hata kama atakayeshinda atatoka upinzani.

Kama una ushahidi wa mgombea yeyote wa Urais wa CCM aliyewahi kutamka hivyo weka clip humu jamvini....

Kama ambavyo pia haijawahi kutokea Tanzania mmoa wa wataalam wa tume ya uchaguzi akauwawa kinyama siku chache kabla ya uchaguzi.Shilingi ina pande mbili ukiangalia upande mmoa geuza uangalie upande wa pili.

Tunawatakia amani Kenya,tusubiri matokeo na namna yao ya kuyapokea matokeo hayo.Sitamani hata kidogo yaliyotokea uchaguzi uliopita yatokee tena Kenya.Yeyote anayedhani tunayakujifunza kutoka Kenya kuhusiana na uchaguzi ninatofautiana naye mno.
 
Acha kudundanganya wewe. Haya uliyoyaandika hapa unayajua lakini?
Unakumbuka alichokifanya Kibaki mwaka 2007, unakumbuka mitambo ilivyovurugwa mwaka 2013? Unakumbuka jinsi meneja wa ICT - Msando alivyouwawa kinyama?
Unaongelea Democrasia ipi?
Pumbavu kabisa.
Mkuu mbona unaporomosha matusi?

Hapa tunajibizana kwa hoja, hatushindani kwa matusi.......

Matusi tuwaachie wenyewe akina Kibajaj na Mlinga.......
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom