Viongozi na wanachadema ni wakati wa kuchukua tahadhari

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Ni jambo la wazi kuwa sasa chadema ni tishio kwa ccm na kinazidi kuungwa mkono.Pamjo na hali hii mnnatakiwa kuwa makini ktk kauli na matendo yenu.Kauli ya Nassari na wenzake inaweza kuwa na makosa kisheria ila naamini inataka kukuzwa kwasababu za kisiasa.Hivi kweli Nassari na wenzake wanaweza kumzuia raisi asikanyage kanda ya kaskazini au kuweka mipaka kanda ya ziwa na mmoja akawa raisi na mweingine waziri mkuu?Kauli hizi zinaweza zikawa zina kasoro kisheria ila ni kawaida ya wanasiasa kutoa kauli za kupigana vijembe.Mbona hata spika wa bunge huwa anatoa kauli za utani kwa wapinzani na wote wanacheka.

Chadema mjiepusha na kauli na matendo ya aina hii kwani inaweza kutumiwa na wapinzani wenu kama propaganda kuwaharibia kisiasa na mkaonekana hamfai kuwa viongozi wa baadae wa taifa hili na bahati mbaya sana wenzenu ndio waneshika dola.Inawezekana kabisa kauli hii ingetolewa na wanachama wa vyama vingine vya upinzani visivyo na nguvu isngepewa uzito huu na siajabu ingeisha kimya kimya tu.
 
Mnakuza vi2 vidogo 4 political propaganda..magamba ham2pi shida.wachukulieni hatua wale wapemba wanaotaka kujitenga walojikatia jina liitwalo SABAOTI LAND DEFFENCE
 
Back
Top Bottom