Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
VIONGOZI sita wa madhehebu ya dini wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya nchini, wamejitokeza mbele ya Kamati ya Maadili ya Viongozi wa Dini na Haki za Jamii na kukiri kujihusisha na biashara hiyo kwa muda mrefu sasa.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, baada ya kuhojiwa, viongozi hao waliiomba Kamati hiyo kutowataja hadharani majina ama madhehebu yao kwa kuhofia kubezwa kwa madhehebu wanayoyaongoza.
Akizungumza mwishoni mwa ziara yao Zanzibar, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mchungaji William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekoste Tanzania, alisema mbali ya orodha hiyo, ipo pia ya watu 18 wakiwemo wafanyabiashara wakubwa na wanasiasa wanaojihusisha na biashara hiyo.
Alisema orodha zote zitafikishwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchini.
Mchungaji Mwamalanga alisema tatizo la ongezeko la dawa za kulevya, pia inazihusu nchi mbalimbali duniani na kwamba kamati hiyo itakutana na kamati nyingine kama hizo za nchi za Maziwa Makuu kuzungumzia ufumbuzi wa suala hilo.
Alisema mkutano huo pia utapendekeza kwa mabunge ya nchi hizo na Bunge la Afrika Mashariki kutunga sheria za kuwafilisi wote waliojilimbikizia mali kutokana na biashara za dawa za kulevya kwa nchi wanachama.
Hata hivyo, Kamati hiyo ya Maadili ya Viongozi wa Dini na Haki za Jamii ikiwa Visiwani, imesifu na kupongeza juhudi za Jeshi la Polisi kwa hatua zao za kukabiliana na ongezeko la dawa za kulevya.
Akizungumzia kero ya dawa za kulevya visiwani hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Aziz Juma Mohammed, alisema Jeshi hilo limekuwa likiwakamata wengi wa wafanyabiashara na watumiaji wa dawa za kulevya na kuwafikisha mahakamani.
Hata hivyo, Kamanda Aziz alitoa mwito kwa wananchi na wadau mbalimbali wa usalama kuendelea kusaidiana na Jeshi hilo kwa kutoa taarifa za wale wote wanaojihusisha na mtandao wa dawa hizo.
Kamanda Aziz alisema kama kila mwananchi atatoa taarifa za siri Polisi za kuwepo kwa mtu ama kundi la watu wanaojihusisha na biashara hiyo ama uhalifu mwingine wowote, ni wazi kuwa Polisi itawatia mbaroni.
Wiki iliyopita, watu wawili wakazi wa Dar es Salaam, wamekamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amaan Karume, Zanzibar kwa nyakati tofauti wakitokea Brazil, ambapo kila mmoja alipatikana na kiasi kikubwa cha dawa za kulevya aina ya kokeini.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, baada ya kuhojiwa, viongozi hao waliiomba Kamati hiyo kutowataja hadharani majina ama madhehebu yao kwa kuhofia kubezwa kwa madhehebu wanayoyaongoza.
Akizungumza mwishoni mwa ziara yao Zanzibar, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mchungaji William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekoste Tanzania, alisema mbali ya orodha hiyo, ipo pia ya watu 18 wakiwemo wafanyabiashara wakubwa na wanasiasa wanaojihusisha na biashara hiyo.
Alisema orodha zote zitafikishwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchini.
Mchungaji Mwamalanga alisema tatizo la ongezeko la dawa za kulevya, pia inazihusu nchi mbalimbali duniani na kwamba kamati hiyo itakutana na kamati nyingine kama hizo za nchi za Maziwa Makuu kuzungumzia ufumbuzi wa suala hilo.
Alisema mkutano huo pia utapendekeza kwa mabunge ya nchi hizo na Bunge la Afrika Mashariki kutunga sheria za kuwafilisi wote waliojilimbikizia mali kutokana na biashara za dawa za kulevya kwa nchi wanachama.
Hata hivyo, Kamati hiyo ya Maadili ya Viongozi wa Dini na Haki za Jamii ikiwa Visiwani, imesifu na kupongeza juhudi za Jeshi la Polisi kwa hatua zao za kukabiliana na ongezeko la dawa za kulevya.
Akizungumzia kero ya dawa za kulevya visiwani hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Aziz Juma Mohammed, alisema Jeshi hilo limekuwa likiwakamata wengi wa wafanyabiashara na watumiaji wa dawa za kulevya na kuwafikisha mahakamani.
Hata hivyo, Kamanda Aziz alitoa mwito kwa wananchi na wadau mbalimbali wa usalama kuendelea kusaidiana na Jeshi hilo kwa kutoa taarifa za wale wote wanaojihusisha na mtandao wa dawa hizo.
Kamanda Aziz alisema kama kila mwananchi atatoa taarifa za siri Polisi za kuwepo kwa mtu ama kundi la watu wanaojihusisha na biashara hiyo ama uhalifu mwingine wowote, ni wazi kuwa Polisi itawatia mbaroni.
Wiki iliyopita, watu wawili wakazi wa Dar es Salaam, wamekamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amaan Karume, Zanzibar kwa nyakati tofauti wakitokea Brazil, ambapo kila mmoja alipatikana na kiasi kikubwa cha dawa za kulevya aina ya kokeini.