Viongoz wa CCM tunalo la kujifunza, kwenda kumsalimia mgonjwa hatuombi ruhusa .

MWITONGO MAARIFA

JF-Expert Member
Aug 11, 2018
276
1,428
Nimejifunza umuhimu wa kuishi ukiwa huru, yapo matatizo ya kijamii yanatokea katika siku za hivi karibuni hasa UGONJWA, ajali na misiba. Wenzetu vyama pinzani wapo huru kuingia nyumba yoyote kutoa pole, wapo radhi waonekane wakitoa pole na hawaombi kibali wala ruhusa. Sisi Wana CCM kwanini tunashindwa kuungana na ndugu zetu kwenye shida tunabaki kupiga simu!

Kwann tunajifunza ubinadamu ukubwani badala tuzaliwe nao?Hawa ni baba zetu, shemeji zetu, wake zetu, watoto wetu, Watanzania wenzetu na mwisho binadamu wenzetu tusifundishwe kuchukiana. Inaleta faraja tukichangamana nao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimejifunza umuhimu wa kuishi ukiwa huru, yapo matatizo ya kijamii yanatokea katika siku za hivi karibuni hasa UGONJWA, ajali na misiba. Wenzetu vyama pinzani wapo huru kuingia nyumba yoyote kutoa pole, wapo radhi waonekane wakitoa pole na hawaombi kibali wala ruhusa. Sisi Wana CCM kwanini tunashindwa kuungana na ndugu zetu kwenye shida tunabaki kupiga simu!

Kwann tunajifunza ubinadamu ukubwani badala tuzaliwe nao?Hawa ni baba zetu, shemeji zetu, wake zetu, watoto wetu, Watanzania wenzetu na mwisho binadamu wenzetu tusifundishwe kuchukiana. Inaleta faraja tukichangamana nao

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba kueleweshwa, nini kimetokea?
 
Mkuu sijui kama umesoma baadhi ya wana chadema wanavyofurahi mtu wa CCM akipata matatizo,ila wanasikitika CCM wakifurahi matatizo ya kina Lissu.

always positive
 
Kwa mkanganyiko huu wa kangi lugola unaendaje kutoa pole
Screenshot_20190213-235231.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sijui kama umesoma baadhi ya wana chadema wanavyofurahi mtu wa CCM akipata matatizo,ila wanasikitika CCM wakifurahi matatizo ya kina Lissu.

always positive
Hakunq mtu mwenye akili timamu anaefurahiya matatizo ya wengine. Isipokuwa mmeanzisha wenyewe chuki tena toka moyoni kwa wanachadema. Mh Lema alipokuwa gerezani Wabunge wa ccm walipigwa stop kwenda kumjulia hali. Walioonyesha nia waliitwa wasaliti. Hali kadhalika kwa Mh Lissu. Rejea comments za wanaccm juu ya Mh Lissu.

Kama ninyi mnatutengenezea matatizo kisha mnayafurahiya, Mungu wetu anapokuwa upande wetu kwa kuwafinyeni nanyi mpate maumivu kwanini tusifurahiye?? Hivi mnavyowafurahiya Mh Mbowe na Matiko kuwa gerezani kwa mbinu zenu za kupika tena mkasahau kuwa wao ni wazazi wenye familia zao, tutaacha kufurahiya hata mnapopata malipo ya mnayoyapanda??

Mwasisi wa haya yote mnamjua lkn hamtaki abadilike kwakuwa wanaoumia ni jirani zenu. Bado tutaendelea kumuomba Mungu azidi kuwachapa viboko nasi tupate kushangilia kwa furaha.


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom