Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Vinyago vya kuchonga vimekuwapo tangu zama za historia na vimechukuliwa kama utamaduni wa nchi nyingi za Bara hili la Afrika, ikiwemo Tanzania.
Tanzania imejijengea sifa kubwa ya kuwa na utamaduni wa vinyango vinavyochongwa na Wamakonde kutokana na mti wa mpingo (blackwood), aina ya miti ambayo hapa duniani inapatikana katika sehemu za kusini mwa Tanzania pekee.
Vinyago hivyo -- ambavyo vingi huwa ni sura au umbile la mtu mweusi vimetokea kuwa vivutio vikubwa kwa watalii na hivyo kuwa biashara kubwa inayoingizia taifa fedha za kigeni.
Lakini hapa inafaa kujiuliza kidogo: Vinyago hivi hunuuliwa na hao Wazungu na kuvipeleka kwao ambako hufanywa mapambo ktk sitting room zao.
Kwa maoni yangu, matumizi haya ya mwisho ya vitu hivyo yamekuwa yanatudhalilisha sisi watu weusi. Kuna rafiki yangu mmoja aliyewahi kuishi Denmark alinieleza kuwa watoto wanaozaliwa na kukulia ktk nyumba hizo huambiwa na wazazi wao kuwa watu weusi wameumbwa kama vilivyo vinyago hivyo.
Aidha wageni wao wanaotembelea nyumba hizo zenye mapambo ya vinyago nao huambiwa hivyo hivyo.
Hali hii inawafanya watu weusi daima kuwa ktk kudhalilishwa mbele ya mataifa ya Wazungu yanayoendelea, kitu ambacho daima hutuendeleza kuwa wanyonge mbele yao. Matokeo ni kwamba daima wanatudharau.
Kwa maoni yangu nadhani biashara hii ingeanza kupigwa vita, Tanzania hapa na kwingineko Barani Afrika, potelea mbali kama inatuingizia kipato.
Naamini kabisa ingekuwa nia wao Wazungu wasingekubali kufanyiwa kitu cha namna hii.
Tanzania imejijengea sifa kubwa ya kuwa na utamaduni wa vinyango vinavyochongwa na Wamakonde kutokana na mti wa mpingo (blackwood), aina ya miti ambayo hapa duniani inapatikana katika sehemu za kusini mwa Tanzania pekee.
Vinyago hivyo -- ambavyo vingi huwa ni sura au umbile la mtu mweusi vimetokea kuwa vivutio vikubwa kwa watalii na hivyo kuwa biashara kubwa inayoingizia taifa fedha za kigeni.
Lakini hapa inafaa kujiuliza kidogo: Vinyago hivi hunuuliwa na hao Wazungu na kuvipeleka kwao ambako hufanywa mapambo ktk sitting room zao.
Kwa maoni yangu, matumizi haya ya mwisho ya vitu hivyo yamekuwa yanatudhalilisha sisi watu weusi. Kuna rafiki yangu mmoja aliyewahi kuishi Denmark alinieleza kuwa watoto wanaozaliwa na kukulia ktk nyumba hizo huambiwa na wazazi wao kuwa watu weusi wameumbwa kama vilivyo vinyago hivyo.
Aidha wageni wao wanaotembelea nyumba hizo zenye mapambo ya vinyago nao huambiwa hivyo hivyo.
Hali hii inawafanya watu weusi daima kuwa ktk kudhalilishwa mbele ya mataifa ya Wazungu yanayoendelea, kitu ambacho daima hutuendeleza kuwa wanyonge mbele yao. Matokeo ni kwamba daima wanatudharau.
Kwa maoni yangu nadhani biashara hii ingeanza kupigwa vita, Tanzania hapa na kwingineko Barani Afrika, potelea mbali kama inatuingizia kipato.
Naamini kabisa ingekuwa nia wao Wazungu wasingekubali kufanyiwa kitu cha namna hii.